Samia ataka wanawake wajipange Urais 2025
HomeHabari

Samia ataka wanawake wajipange Urais 2025

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanawake kujipanga kuhakikisha wanaweka Rais mwanamke katika Uchaguzi Mkuu ujao. Vilevile, amehoji kil...

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanawake kujipanga kuhakikisha wanaweka Rais mwanamke katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Vilevile, amehoji kilichoandikwa na moja ya gazeti nchi kwamba hana nia ya kuwania urais mwaka 2025, akiuliza 'nani kawaambia?'

Rais Samia alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya Siku ya Demokrasia Duniani yaliyohudhuriwa na taasisi mbalimbali na wasichana 50 ambao waliokolewa kwenye biashara ya usafirishaji wa binadamu.
 
Katika maadhimisho hayo, Rais Samia alikabidhiwa tuzo tatu, moja ikitolewa na Mwenyekiti wa Azaki ya Wanawake Tanzania (Ulingo), Anna Abdallah, ya pili kutoka kwa watoto waliookolewa katika udhalilishaji wa kimaisha na nyingine kutoka kwa masista wa St. Joseph.
 
Akizungumza katika maadhimisho hayo, Rais Samia alisema, “Leo (jana) mmempa tuzo Rais wenu, Rais mwanamke, kwa bashasha na furaha kubwa, lakini ninataka niwaambie wanawake bado hatujaweka Rais mwanamke.
 
Rais Samia alifafanua kuwa Rais huyo mwanamke amekaa kwa sababu ya kudra ya Mwenyezi Mungu na matakwa ya Katiba.
 
“Tulichokichangia sisi na dada zetu na mama zetu na Mama Anna Abdallah ni ile kusukuma mpaka mwanamke akawa Makamu wa Rais, ule ndio mchango mkubwa ambao tumeufanya wanawake.
 
"Kama isingekuwa mpango wa Mungu, ingekuwa ngumu, tungefikia hapo kila mwaka tunakwenda ni hapo, ni hapo," alisema.
 
Rais Samia aliwaeleza kuwa Rais mwanamke watamweka mwaka 2025.
 
“Mwaka 2025 wanawake tukifanya vitu vyetu vizuri, kushikamana, tukimweka Rais wetu, tutakutana hapa kwa furaha kubwa sana. Wameanza kutuchokoza, wameanza kutuchokoza kuandika kwenye vigazeti 'Samia hatasimama', nani kawaambia?
 
“Fadhila za Mungu zikija mikononi kwako usiziachie, hizi ni fadhila za Mungu ndugu zangu, wanawake tumefanya kazi kubwa kuleta uhuru wa nchi hizi, wanawake tumefanya kazi kubwa kujenga siasa za nchi, tumebeba sana wanaume katika siasa za nchi hizi.
 
"Leo Mungu ametupa baraka mikononi, tukiiachia Mungu atatulaani," alisema huku ukumbi ukilipuka kwa shangwe.
 
Machi 19, mwaka huu, Samia ambaye alikuwa Makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais wa nchi kutokana na kifo cha Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, suala hilo lilifanyika kwa mujibu wa Katiba.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Samia ataka wanawake wajipange Urais 2025
Samia ataka wanawake wajipange Urais 2025
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQAdkGC8hqw-uzFfmmMEijDBOGczXKbXQiAG359Lxi55ob8zYGawtz96mpjGT3LCWNgONK32zPS9qZpAaSI-6b3HrBGTZnco8ea8FbswdRP9K2waOAMvWnkaknXtThI_gYoGsr6wl2q23z/s0/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQAdkGC8hqw-uzFfmmMEijDBOGczXKbXQiAG359Lxi55ob8zYGawtz96mpjGT3LCWNgONK32zPS9qZpAaSI-6b3HrBGTZnco8ea8FbswdRP9K2waOAMvWnkaknXtThI_gYoGsr6wl2q23z/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/samia-ataka-wanawake-wajipange-urais.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/samia-ataka-wanawake-wajipange-urais.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy