Wananchi Lupembe wapunguziwa adha ya kukodi usafiri kwa ajili ya wagonjwa 
HomeHabariTop Stories

Wananchi Lupembe wapunguziwa adha ya kukodi usafiri kwa ajili ya wagonjwa 

Wananchi wa kata tano za Jimbo la Lupembe wilayani Njombe, wanatarajia kuondokana na adha ya kukodi usafiri kwa gharama kubwa pamoja na kupa...

Wananchi wa kata tano za Jimbo la Lupembe wilayani Njombe, wanatarajia kuondokana na adha ya kukodi usafiri kwa gharama kubwa pamoja na kupandisha wanawake wajawazito kwenye boda boda wanapofuata huduma kwenye hospitali kubwa mara baada ya serikali kuwaletea gari la kubebea wagonjwa.

 

Wakizungumza baada ya kukabidhiwa gari hilo katika kituo cha afya Mtwango na Mbunge wa Jimbo la Lupembe Edwin Swalle hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali.

 

Wananchi hao wamesema wanaishukuru serikali kwa kuhakikisha tatizo la kukosekana kwa gari la wagonjwa linaondoka ili kuwasaidia kuondokana na adha hiyo.

 

Mmoja wa wananchi hao akiwemo Sara Kaduma amesema wanayo furaha kuletewa gari la wagonjwa kwa ajili ya kuwawezesha usafiri pindi wanapopewa rufaa ya kufuata matibabu katika maeneo mengine.

 

“Ni kweli hospitali zipo, vituo vya afya vipo lakini pindi tunapotakiwa kwenda mbele zaidi labda mtu anatakiwa kujifungua anapandishwa kwenye boda boda mpaka anafika hospitali mtoto anakuwa amepata changamoto kwa hiyo vifo vingi vya mara kwa mara vya watoto vimetokea,” alisema Sara.

 

Awali Mbunge wa Jimbo la Lupembe Edwin Swalle alisema gari hilo linakwenda kuwaondolea wananchi adha kwa kiasi kikubwa na kueleza kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amewapendelea kwa kutatua changamoto za afya katika jimbo hilo.

 

“Kuwa na gari la wagonjwa, kuwa na zahanati, vituo vya afya maana yake ni kwamba serikali na viongozi wenu wanapigania kuongeza umri wa kuishi wa watanzania. Tumpongeze sana mh Rais Samia kwa sababu tusipokuwa na afya bora, tusipokuwa na madawa kama hakuna magari ya kuwahisha watu hospitali ilikuwa uishi mwaka mmoja miwili unaondoka mapema,” alisema Swalle.

 

Swalle alisema wanawake wengi wajawazito wamepoteza maisha kutokana na kukosekana gari la wagonjwa kwa ajili ya kuwapeleka katika hospitali kubwa na kwamba walifia njiani wakiwa kwenye boda boda.

 

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe,Valentino Hongoli alishukuru kwa kuletewa gari hilo na kueleza kuwa mbunge huyo amekuwa akifanya maendeleo bila ya kuangalia ukanda.

 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Christopher Sanga alisema walikuwa na kata tano ambazo zilikuwa zinakosa huduma ya gari la wagonjwa na kwamba uwepo wa gari hilo litasaidia wananchi kuondokana na adha hiyo.

 

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mtwango, Beno Makero alisema walikuwa wanapata shida kwa sababu ya kukosekana kwa gari ya kubebea wagonjwa hivyo wakati mwengine walilazimika kukodi gari za watu binafsi ili kuwapeleka wagonjwa kwenye hospitali kubwa.

 

The post Wananchi Lupembe wapunguziwa adha ya kukodi usafiri kwa ajili ya wagonjwa  first appeared on Millard Ayo.



from Millard Ayo https://ift.tt/hjtc7Lg
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Wananchi Lupembe wapunguziwa adha ya kukodi usafiri kwa ajili ya wagonjwa 
Wananchi Lupembe wapunguziwa adha ya kukodi usafiri kwa ajili ya wagonjwa 
https://millardayo.com/wp-content/uploads/2025/01/IMG-20250101-WA0021-950x633.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2025/01/wananchi-lupembe-wapunguziwa-adha-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2025/01/wananchi-lupembe-wapunguziwa-adha-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy