MFARANSA ATAKA MPIRA WA PASI KUWAMALIZA WATANI ZAKE WA JADI
HomeMichezo

MFARANSA ATAKA MPIRA WA PASI KUWAMALIZA WATANI ZAKE WA JADI

KUELEKEA kwenye mchezo wa Kariakoo Dabi unaotarajiwa kuchezwa Mei 8, Uwanja wa Mkapa, Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, raia wa Ufaransa ...

MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMANNE
KOCHA BARAZA WA BIASHARA UNITED AMTAKA BANDA KIKOSINI
MITAMBO 11 YA KAZI INAYOKUBALIKA KWA GOMES NDANI YA SIMBA

KUELEKEA kwenye mchezo wa Kariakoo Dabi unaotarajiwa kuchezwa Mei 8, Uwanja wa Mkapa, Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes, raia wa Ufaransa amekuwa akiwahimiza wachezaji wake kucheza mpira wa pasi fupifupi na kufunga pale wanapokaribia kwenye lango la wapinzani.

Simba imekuwa na mtindo wa kucheza pasi nyingi pale ambapo inawakabiri wapinzani wake katika uwanja, rekodi zinaonyesha kwamba walipocheza na Mtibwa Sugar, Uwanja wa Mkapa na kufunga jumla ya mabao 5-0 walikuwa wakipigiana pasi 10 mpaka 15 pale wanapopata mpira mpaka kufika lilipo lango la wapinzani.

Mchezo wao wa mwisho kucheza Uwanja wa Mkapa kabla ya kuvaana na Yanga, Simba ilicheza na Kagera Sugar na ilishinda mabao 2-1 kwenye Kombe la Shirikisho hatua ya 16 bora.

Ikumbukwe kuwa watani hao wa jadi walipokutana kwenye mzunguko wa kwanza Uwanja wa Mkapa, waligawana pointi mojamoja baada ya ubao kusoma Yanga 1-1 Simba.

Kwenye mchezo huo mbinu za Simba zilikuwa mikononi mwa Kagera Sugar kipindi cha kwanza kwa kuwa zile pasi zao zilikuwa zinakwama kupena kwenye ngome ya David Luhende.

Gomes amesema:"Nahitaji kuona wachezaji wanaweza kuwa kwenye kasi na kujiamini kwani mchezo wetu dhidi ya Yanga hautakuwa mwepesi kutokana na ushindani uliopo pamoja na nafasi.

"Kikubwa ambacho ninakiona kwamba kwenye mechi zetu ambazo zimepita tumepata matokeo mazuri hivyo inaongeza kwetu hali ya kujiamini na mpira wa pasi pamoja na kushambulia ni mbinu ambayo ipo kwa walimu wote," amesema.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza ya Gomes kuiongoza Simba na kukutana na Yanga kwenye Kariakoo Dabi kwa kuwa ile ya mzunguko wa kwanza, Kocha Mkuu alikuwa ni Sven Vandenbroeck.

Pia hata Nassredine Nabi naye itakuwa ni mara ya kwanza kumenyana na Simba kwenye Kariakoo Dabi kwa kuwa ule mchezo wa kwanza alikuwa yupo Mrundi, Cedric Kaze.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MFARANSA ATAKA MPIRA WA PASI KUWAMALIZA WATANI ZAKE WA JADI
MFARANSA ATAKA MPIRA WA PASI KUWAMALIZA WATANI ZAKE WA JADI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQy_0t6kGmf7QiNotWZzwBBe51wHu6VFiAAJNUqvXGR6CFSgFfo5GFl6HVvvCkcdr1jO02J8yC38ibgH6fVzrQda_A_57YLqKm0aEJ0a7rXxmErCSmoLv1kqqzqHcd81wWoYtbuDLhVwu_/w640-h516/Gomes+bana.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQy_0t6kGmf7QiNotWZzwBBe51wHu6VFiAAJNUqvXGR6CFSgFfo5GFl6HVvvCkcdr1jO02J8yC38ibgH6fVzrQda_A_57YLqKm0aEJ0a7rXxmErCSmoLv1kqqzqHcd81wWoYtbuDLhVwu_/s72-w640-c-h516/Gomes+bana.JPG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/mfaransa-ataka-mpira-wa-pasi-kuwamaliza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/mfaransa-ataka-mpira-wa-pasi-kuwamaliza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy