Wenyeviti Mabaraza Ya Ardhi Watakiwa Kuepuka Mazuio Yasiyo Na Tija
HomeHabari

Wenyeviti Mabaraza Ya Ardhi Watakiwa Kuepuka Mazuio Yasiyo Na Tija

 Na Munir Shemweta, WANMM SENGEREMA Serikali imewataka Wenyeviti wa Mbaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kujiepusha na tabia ya uwekaji...

Habai Zilizopo Katika Magazeti ya Leo January 7
BREAKING: Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, amejiuzulu
Kutana Na Shariff Ally Mtaalam Wa Tiba Asili Tanzania


 Na Munir Shemweta, WANMM SENGEREMA

Serikali imewataka Wenyeviti wa Mbaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kujiepusha na tabia ya uwekaji mazuio yasiyo na tija dhidi ya  uuzaji wa nyumba za wadaiwa wa benki.

Akizungumza wakati wa kuzindua Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Sengerema tarehe 21 Machi 2022 jijini Mwanza, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alisema, baadhi ya mazuio huwekwa na kisha shauri hupangiwa tarehe ya mbali  bila sababu ya msingi.

‘’Jambo hili halikubaliki hata kidogo kwani linarudisha nyuma shughuli za kimaendeleo na kukuza uchumi wan chi yetu ‘’ alisema Dkt Mabula.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kutoa kipaumbele katika kuyawezesha Mabaraza ya Ardhi kufanya kazi vizuri na tayari imeanza kufanya maboresho ya muundo wa wizara utakaowezesha kila mkoa kuwa na Msajjili Msaidizi wa Mabaraza kwa ajili ya usimamizi wa karibu wa utendaji kazi wa Mabaraza.

Vile vile, kwa mujibu wa Dkt Mabula Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ambapo katika kuboresha mazingira ya utendaji kazi imefanya mabadiliko ya sheria ili kuwawezesha Wenyeviti wa Mabaraza kuwa na ajira za kudumu.

Aliwakumbusha watumishi wote wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya nchini kutimiza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozi iliyopo na ile itakayokuwa ikitolewa ili kuboresha utoaji huduma ya utatuzi wa migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi.

Pia Waziri wa Ardhi Dkt Mabula aliwataka Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi kuwafuata wananchi kwa kutembelea mabaraza mapya ili kusikiliza mashauri kwenye wilaya husika wakati Wizara ikiendelea kukamilisha taratibu za ajira za wenyeviti wa mabaraza hayo.

Kwa upande wake Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya Stella Tullo alisema, ofisi yake imejipanga na kuhakikisha migogoro ya ardhi inapofika kwenye Mabaraza inasikilizwa kwa haki na kwa haraka na kusisitiza kuwa, hawatopenda kuchelewesha mashauri bila sababu za msingi.

‘’Sisi tunataka shauri linapofika kwenye Baraza liweze kuanza kusikilizwa mapema baada ya taratibu za awali za kisheria kukamilika  ili tuweze kukamilisha kwa wakati’’ alisema Stella

Uzinduzi wa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Sengerema uliwakilisha pia uzinduzi wa mabaraza mengine mapya katika wilaya za Nachingwea, Ruangwa, Liwale, Kilwa, Serengeti, Kongwa , Kishapu na Mlele.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Wenyeviti Mabaraza Ya Ardhi Watakiwa Kuepuka Mazuio Yasiyo Na Tija
Wenyeviti Mabaraza Ya Ardhi Watakiwa Kuepuka Mazuio Yasiyo Na Tija
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaLDPQNcQOa6v7XoYJC6DRdAJMVWmpbXLJ434af_hwiSiCoZ_Js8qP4vlhUUG_GQZu3SZ1A6rom9eb934hfQdSXufGGPg_rHRD1xcWON1dRHnbsEo2b23MDUnPCVDwJagOhl-kki-t1s7ryGc8I9Ecf8daEL16uoi0gAwwab0cvJng92yOd6xCdReWoQ/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaLDPQNcQOa6v7XoYJC6DRdAJMVWmpbXLJ434af_hwiSiCoZ_Js8qP4vlhUUG_GQZu3SZ1A6rom9eb934hfQdSXufGGPg_rHRD1xcWON1dRHnbsEo2b23MDUnPCVDwJagOhl-kki-t1s7ryGc8I9Ecf8daEL16uoi0gAwwab0cvJng92yOd6xCdReWoQ/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/wenyeviti-mabaraza-ya-ardhi-watakiwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/wenyeviti-mabaraza-ya-ardhi-watakiwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy