Balozi Wa Uingereza Nchini Tanzania Aridhishwa Na Utendaji Kazi Wa Rais Samia.
HomeHabari

Balozi Wa Uingereza Nchini Tanzania Aridhishwa Na Utendaji Kazi Wa Rais Samia.

BALOZI wa Uingereza nchini, amesifu uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia  demokrasia hapa nchini ikiwa ni mwaka mmoja tangu ...


BALOZI wa Uingereza nchini, amesifu uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia  demokrasia hapa nchini ikiwa ni mwaka mmoja tangu aingie madarakani.

Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Mwanza, Balozi David Concar, alisema nchi yake inaridhishwa na hali ya siasa inavyoendelea kwa sasa hapa nchini.

Alisema suala la kuwapo demokrasia limeimarika ndani ya mwaka mmoja  na kwamba wataendelea kuunga mkono juhudi hizo.

Alisema nchi yake itaendelea kushirikiana  na Tanzania katika nyanja mbalimbali  za kiuchumi kwa manufaa ya  nchi hizo mbili.

Aliongeza kuwa  kwa sasa uhuru wa vyombo vya habari umeimarika ndani ya mwaka mmoja wa utawala wa Rais Samia, huku akishauri waandishi wa habari mkoani Mwanza  (MPC) kuweka mpango kazi ili kuandika habari zinazohusu wanawake na watoto.

''Ni vyema MPC  kwenye mpango kazi wenu ikaweka jukumu la kuripoti habari zinazohusu usawa wa kijinsia na haki za wanawake na watoto,'' alisema balozi huyo.

Kuhusu mzozo wa nchi za Ukraine na Urusi, alisema nchi itaendelea kujikita kutoa misaada ya kibinadamu na inaamini kwamba uvamizi huo haukuwa wa haki.

Kutokana na hali hiyo, balozi Concar alisema mataifa mengi yalipaza sauti zao kupinga Urusi kuvamia Ukraine  na kumtaka Rais Vladmir Putin kusitisha vita hiyo.

Kwa upande wao, baadhi ya waandishi wa habari mkoani Mwanza, walimshukuru, balozi huyo kwa nchi yake kuwa na programu maalum ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Balozi Wa Uingereza Nchini Tanzania Aridhishwa Na Utendaji Kazi Wa Rais Samia.
Balozi Wa Uingereza Nchini Tanzania Aridhishwa Na Utendaji Kazi Wa Rais Samia.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjL0X6259QRuFA6s2fF4ipws7QKZdsZIAWkZIfMnWkR3-gh6BIl69yHWDUGnHQH-DqLrecJu6GzAaOYCFhrMtZEjBlTIwojBBSFQJcnKGIUShiYxPyBXlA1pbwphtoDvr18dRhUMAHTYacB2S9RVRoB3IXHzbzjXaoYBFAivxMnYUH4woogUeRZ3c9oEA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjL0X6259QRuFA6s2fF4ipws7QKZdsZIAWkZIfMnWkR3-gh6BIl69yHWDUGnHQH-DqLrecJu6GzAaOYCFhrMtZEjBlTIwojBBSFQJcnKGIUShiYxPyBXlA1pbwphtoDvr18dRhUMAHTYacB2S9RVRoB3IXHzbzjXaoYBFAivxMnYUH4woogUeRZ3c9oEA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/balozi-wa-uingereza-nchini-tanzania.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/balozi-wa-uingereza-nchini-tanzania.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy