YANGA WAFUNGUKIA UJIO WA MANJI
HomeMichezo

YANGA WAFUNGUKIA UJIO WA MANJI

  W AKATI aliyekuwa  Mwenyekiti wa  Yanga, Yusuf Manji akitajwa  kurejea kwenye klabu hiyo,  wachezaji wa zamani wa  timu hiyo wamefunguka...

PILATO WA MCHEZO WA AL AHLY V SIMBA KWA KADI ZA NJANO HAJAMBO
YANGA YATEMBEZA KICHAPO, YASHINDA MABAO 3-0 DHIDI YA AFRICAN LYON
JURGEN KLOP ALIA NA MWAMUZI WAKATI WAKICHAPWA 3-1

 WAKATIaliyekuwa Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji akitajwa kurejea kwenye klabu hiyo, wachezaji wa zamani wa timu hiyo wamefunguka kuhusiana na ujio wake.

Hiyo ikiwa ni siku chache tangu taarifa zisambae za ujio wa bosi huyo aliyeifanyia Yanga mengi makubwa kipindi cha utawala wake akiwa mwenyekiti.

 

Manji amezua hofu kwa mashabiki wa Simba kutokana na ujio wake huku akiwa na rekodi kubwa ya kuchukua ubingwa mara tatu mfululizo 2014–15, 2015–16 na 2016–17.


Nahodha wa zamani wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema kuwa, kwake amezipokea kwa furaha taarifa za ujio wa Manji ndani ya Yanga.

 

Cannavaro amesema kuwa lipo wazi kati ya viongozi waliopita kuiongoza timu hiyo, Manji ni mmoja wapo kutokana na utawala bora aliokuwa nao.


“Hizo taarifa sidhani kama ni kweli, kama ni kweli basi ninaamini ile Yanga ya vikombe inakuja katika misimu ijayo na hilo linawezekana kwake.

 

“Manji alitengeneza kikosi bora kilichochukua ubingwa wa ligi mara tatu mfululizo na Ngao ya Jamii katika utawala wake tukiwafunga Azam FC pale Uwanja wa Mkapa.

 

“Na mafanikio yake yametokana na usajili bora aliokuwa anaufanya katika timu, kiukweli taarifa hizo nimezipokea kwa mikono miwili na nitampigia simu kuthibitisha hilo kwani namba yake ninayo,” amesema Cannavaro.

 

Alipotafutwa kiungo wa zamani wa timu hiyo, Athumani Idd ‘Chuji’ kuzungumzia hilo, alisema kuwa: “Kwangu naona faraja kubwa kwa Wanayanga waliokuwa wenye ndoto za timu yao kuchukua ubingwa.

 

“Sijajua lini anakuja huyo Manji, lakini kwa mimi ninayemjua basi Wanayanga watarajie kuona usajili bora wa kisasa ukifanyika utakaoendana na hadhi ya Yanga.

 

“Mimi ninamfahamu vizuri Manji, kwani katika utawala wake nilikuwa sehemu ya wachezaji tegemeo, vitu vyake alikuwa akifanya kwa uwazi na siyo mgumu kutoa fedha yoyote ya usajili ili afanikishe usajili pamoja kambi nzuri," .


Naye mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo, Mohammed Hussein ‘Chinga One’ alisema kuwa: “Sijajua Manji atakuja kukaa nafasi gani, uongozi, mwanachama au vipi, lakini kwangu ninamkaribisha Yanga.


“Ninaamini kama akija ataungana na wadhamini wengine katika kufanikisha mengi mazuri, hakuna asiyemjua Manji kutokana na kukumbukwa na mengi.”



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: YANGA WAFUNGUKIA UJIO WA MANJI
YANGA WAFUNGUKIA UJIO WA MANJI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwYHE1VloM5krG5cXmTAKJUx6wxzyNkS8UT-F3K_XPFAJG3JFj_X22y8ttD3BB1ReEX1tBv0kUR7jne79VplfPHibfsJ0XwkIGTQnjmxDJ47fVl5PPMWJeIAcXB99zJhMxLTGaT4dbxZoB/w640-h480/Manji.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwYHE1VloM5krG5cXmTAKJUx6wxzyNkS8UT-F3K_XPFAJG3JFj_X22y8ttD3BB1ReEX1tBv0kUR7jne79VplfPHibfsJ0XwkIGTQnjmxDJ47fVl5PPMWJeIAcXB99zJhMxLTGaT4dbxZoB/s72-w640-c-h480/Manji.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/yanga-wafungukia-ujio-wa-manji.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/yanga-wafungukia-ujio-wa-manji.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy