JK ashuhudia Nyusi akikabidhiwa Msumbiji
HomeMatukio

JK ashuhudia Nyusi akikabidhiwa Msumbiji

RAIS Jakaya Kikwete jana alikuwa miongoni mwa marais walioshuhudia Felipe Nyusi akiapishwa kuwa Rais wa Tano wa Msumbiji. Nyusi aliapish...

KUTANA NA MTAALAMU ALIYEFANIKIWA KUANZISHA REDIO YAKE MWENYEWE
BREAKING NEWS: WATU 10 WAFARIKI DUNIA BAADA YA BASI LA NGORIKA NA RATCO KUGONGANA USO KWA USO
INASIKITISHA: WA 3 WALIOFUNGIWA NDANI MIAKA 10 NA MAMA YAO MMOJA AFARIKI DUNIA
Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji akiapaRAIS Jakaya Kikwete jana alikuwa miongoni mwa marais walioshuhudia Felipe Nyusi akiapishwa kuwa Rais wa Tano wa Msumbiji.
Nyusi aliapishwa kwa kula kiapo cha kulitumikia taifa hilo mbele ya Mwenyekiti wa Baraza la Katiba, Heremegildo Gamito, mbele ya umati wa viongozi wa mataifa mbalimbali na wananchi wa Msumbiji.
Sherehe hizo zilipambwa kwa shamrashamra mbalimbali ikiwa ni pamoja na burudani za kwaya, halaiki na gwaride rasmi, lililoandaliwa kwa ajili ya Rais huku baadhi ya makundi ya wananchi wakiwa na fulana zenye maneno ya Frelimo na picha za Rais Nyusi wakiimba na kucheza pembeni.
Mara baada ya kuapa, Rais Nyusi alitia saini kitabu maalumu, kisha alikabidhiwa bendera na vitendea kazi, ambavyo aliwaonesha wananchi na wageni waliohudhuria kuashiria kuwa amekabidhiwa rasmi nchi.
Rais Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi kutoka nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na wanaotoka katika nchi zinazozungumza Kireno, waliohudhuria sherehe hizo.
Ujumbe kutoka Tanzania pia uliwakilishwa na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohammed Aboud Mohammed.
Mbali na viongozi wa Tanzania, wengine ni kutoka nchi za Swaziland, Afrika Kusini, Malawi, Zambia, Lesotho, Zimbabwe na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Rais Nyusi ameingia madarakani akimrithi Rais Armando Guebuza baada ya kujinyakulia kura kwa asilimia 57 na kumwangusha mpinzani wake na Kiongozi wa chama cha Renamo, Alfonso Dhlakama aliyepata kura asilimia 36.6 katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 15 mwaka jana.
Hata hivyo, pamoja na ushindi huo, Rais Nyusi amepata asilimia chache za kura ukilinganisha na wakati wa Rais Guebuza kwenye uchaguzi wa mwaka 2009, ambapo alipata asilimia 75.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: JK ashuhudia Nyusi akikabidhiwa Msumbiji
JK ashuhudia Nyusi akikabidhiwa Msumbiji
http://www.habarileo.co.tz/images/jacinto.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/jk-ashuhudia-nyusi-akikabidhiwa-msumbiji.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/jk-ashuhudia-nyusi-akikabidhiwa-msumbiji.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy