Waziri Nape: Hakuna Wizi Mabando Ya Simu
HomeHabari

Waziri Nape: Hakuna Wizi Mabando Ya Simu

Serikali imetoa maelezo kuhusiana na kuwapo kwa malalamiko ya wizi wa ‘bandle’ la simu. Maelezo hayo yametolewa na Waziri wa habari, Mawa...

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo January 6, 2024
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo January 5, 2024
“Dirisha la makadirio ya Kodi kwa mwaka 2025 lafunguliwa Wafanyabiashara Mkoa wa Tanga wakumbushwa”


Serikali imetoa maelezo kuhusiana na kuwapo kwa malalamiko ya wizi wa ‘bandle’ la simu. Maelezo hayo yametolewa na Waziri wa habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari, Nape Nnauye bungeni.

Nape alisema kwamba kutokana na malalamiko ya watumiaji wa ‘bandle la simu, serikali ilifanya tathmini, ambayo imebainisha kwamba hayana ukweli, bali zinakwisha kutokana na simu za kisasa wanazotumia watu.

Akijibu hoja mbalimbali za wabunge na kamati ambao wamelalamika kwa wizi wa bandle, Nape , alisema uwezo wa Mamlaka ya Mawasilinao Tanzania (TCRA), kufuatilia miamlaka mbalimbali umeongezeka.

“Tunaendelea kuchambua taarifa mbalimbali juu ya mamalamiko ya matumizi ya bandle kwenye simu zetu, hoja kwamba kuna zinazowekwa zinatumika bila mtumiaji kuzitumia, yamekuwapo malalamiko yamefikishwa kwenye mamlaka husika na uchambuzi umefanyika,” alisema na kuongeza:

“Matokeo ya uchambuzi yanaonyesha hakuna wizi uliotokea isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa, yamejikita kwenye simu za kisasa baadhi ya ‘application’ zinatumia ‘bandle’ bila mwenye simu kujua, nyingine simu hizo unaweza kuweka bandle na kuwasha ‘data’ kupitia ‘hot sport; ambayo inatumiwa na mtu mwingine.”

“Kuna watu wamechunguzwa ikabainika kuna watu wametumia bandle zao.”

Alisema suluhisho lililoletwa ni kupitia Baraza la Watumiaji wa Huduma za Simu ambao wametengeneza ‘application’ ya mtumiaji wa simu kufuatilia matumizi yake na ataweza kuzima baadhi ya ‘application’ zinazotumia mtandao wake.

“Tunafanya majaribio ya ‘application hiyo na itakapokuwa tayari watumiaji watapewa na kufuatilia. Pia tunatoa elimu ya matumizi ya simu za kisasa ili watu wasiingie kwenye gharama kwa kutokujua,” alisema Nape.

Aidha, alisema utafiti umeonyesha shida kubwa ni kwenye matumizi badala ya wizi na kwamba hadi sasa hawajakamata wizi wowote.

“Jambo hili limekuwa kubwa na linazungumzwa muda mrefu, ni rahisi kudhani kuna wizi na tukawahukumu watoa huduma lakini TCRA, malalamiko yoyote hakuna lalamiko limethibitisha kuna wizi, bado yanaendelea kupokelewa,”alisema.

Awali, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso, alisema wanaishauri serikali iisimamie TCRA kukutana na wadau na watoa huduma, ili kuona chanzo cha kupungua kwa miamala ya simu kwa lengo la kutatua changamoto hizo.

“Kamati ilibaini kupungua kwa miamala ya simu, jambo linalokinzana na matarajio ya kisera katika sekta. Kupungua kwa miamala hiyo ya simu ni ishara ya changamoto ya shughuli za umma za udhibiti na uendeshaji wa sekta ya mawasiliano, hali inayohitaji kurekebishwa mapema,”alisema.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Nape: Hakuna Wizi Mabando Ya Simu
Waziri Nape: Hakuna Wizi Mabando Ya Simu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjvChE1tpP2duor69X_dEWIrCLJI2CJ89OF6Xf_p_RIf_rlu57JKp-cz2zXgo6Keenqi3VYltoo6YSiYvfIO-135253UPqnc3Yek9zR-lzTPIpmEavpBhihwCI5wui3TDU_6T8_3NpOaoMoXKs6ZTEZfLNFGGTmlUG5ILuw1r_yofl0hzA_B7OicCBZ6A=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjvChE1tpP2duor69X_dEWIrCLJI2CJ89OF6Xf_p_RIf_rlu57JKp-cz2zXgo6Keenqi3VYltoo6YSiYvfIO-135253UPqnc3Yek9zR-lzTPIpmEavpBhihwCI5wui3TDU_6T8_3NpOaoMoXKs6ZTEZfLNFGGTmlUG5ILuw1r_yofl0hzA_B7OicCBZ6A=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/waziri-nape-hakuna-wizi-mabando-ya-simu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/waziri-nape-hakuna-wizi-mabando-ya-simu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy