Waziri Makamba Asisitiza Kuongeza Kasi Ya Uzalishaji Wa Vifaa Vya Umeme, Akipongeza Kiwanda Cha Africab
HomeHabari

Waziri Makamba Asisitiza Kuongeza Kasi Ya Uzalishaji Wa Vifaa Vya Umeme, Akipongeza Kiwanda Cha Africab

KATIKA kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji na umeme katika vitongoji vyote nchini Waziri wa Nishati, January Makamba amewataka wawekezaji...

Maendeleo ni makubwa nchini, Watanzania tumuunge mkono Rais Samia-Mathias Canal
Habari kubwa Magazetini Kenya leo September 20, 2024
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 20, 2024


KATIKA kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji na umeme katika vitongoji vyote nchini Waziri wa Nishati, January Makamba amewataka wawekezaji kuendelea kujitokeza na kuwekeza katika viwanda vya vifaa vya kuunganisha umeme ili kufanikisha lengo la Serikali la kutumia bidhaa za ndani katika utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.

Akizungumza baada ya kutembelea kiwanda cha nyaya cha Africab kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam, akiwa ameambatana na Naibu Waziri Stephen Byabato Makamba amesema viwanda vya namna hiyo ni muhimu na vinahitajika zaidi ili kupunguza utegemezi wa vifaa kutoka nje ya nchi.

Aidha amesema mpango wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inasambaza umeme katika vitongoji vyote nchini na hiyo ni baada ya kufanikiwa kupeleka umeme kwenye vijiji.

“Tuna vitongoji 64000 kati ya hivyo 37,000 bado havijafikiwa na huduma ya umeme......Tumedhamiria katika kipindi cha miaka minne chini ya uongozi thabiti wa Rais Samia Suluhu Hassan vitongoji hivyo lazima vifikiwe na huduma hiyo, na kwa kufanikisha hilo inatupasa tuhakikishe tuna vifaa vya kutosha vyenye ubora, nimefarijika baada ya kutembelea kiwanda hiki kinafanya kazi nzuri sana.''

Waziri Makamba amesema zinahitajika nyaya zenye kukidhi kilomita 340,000 kwa vitongoji vyote pamoja na vifaa vingine kama mita, transfoma na vifaa vingine vya umeme.

Vilevile Waziri Makamba amesema, zitahitajika transoma 38, 000 zaidi na kutumia wasaa huo kuwakaribisha wawekezaji wengi zaidi kuja na kuwekeza zaidi kwenye eneo hilo ili kuhakikisha vifaa vinapatikana nchini pamoja na kutengeneza ajira kwa wazawa.

“Nimeshuhudia uzalishaji unaoendelea hapa ila bado tunahitaji kuongeza, nimefurahi kuna mpango wa kuongeza kiwanda na niwaombe wawekezaji wengine wasisite kujitokeza na kuwekeza katika sekta hii ya Nishati.'' Amesema.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Africab, David Tarimo amesema kiwanda hicho kina uwezo mkubwa wa kuzalisha vifaa na kwa kutambua ukubwa wa uhitaji wameongeza uwekezaji kwa kufungua kiwanda kingine katika eneo la Kimbiji.

“Kuna kiwanda kingine tumeanzisha kule Kimbiji ili kuongeza uzalishaji na tutaendelea kuhakikisha tunazalisha bidhaa zetu katika ubora unaohitajika sokoni pamoja na kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania.''

Tarimo ameishukuru Serikali kwa kuendelea kushirikiana nao na kuiomba iendelee kuweka mkazo wa matumizi ya bidhaa za ndani hasa katika kuhakikisha ubora wa utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa kuwa Tanzania kwa sasa ina uwezo na hakuna sababu ya kuruhusu bidhaa nyingi ziingie kutoka nje ya nchi.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Makamba Asisitiza Kuongeza Kasi Ya Uzalishaji Wa Vifaa Vya Umeme, Akipongeza Kiwanda Cha Africab
Waziri Makamba Asisitiza Kuongeza Kasi Ya Uzalishaji Wa Vifaa Vya Umeme, Akipongeza Kiwanda Cha Africab
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEie2cMm0qqs41Po734Fj-VvAoXsAv1tj8p5RWSgkcyFP533_bp-50yh2XRnbabnF5qBjDixI-J2Lco1Je3YbSPs7OMPU_--GctCs9UGfgEYyc5_bl6oByKwDQr_hP5_BA1sDcWdmDfHLz0ufksD2vyKy74csiIdw_Fv-cCmcPhmyl0vKkFd0z-Gu9Qs2A=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEie2cMm0qqs41Po734Fj-VvAoXsAv1tj8p5RWSgkcyFP533_bp-50yh2XRnbabnF5qBjDixI-J2Lco1Je3YbSPs7OMPU_--GctCs9UGfgEYyc5_bl6oByKwDQr_hP5_BA1sDcWdmDfHLz0ufksD2vyKy74csiIdw_Fv-cCmcPhmyl0vKkFd0z-Gu9Qs2A=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-makamba-asisitiza-kuongeza-kasi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-makamba-asisitiza-kuongeza-kasi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy