ISHU YA FAINI KUTOKA CAF, YANGA YAGOMEA YAKATA RUFAA
HomeMichezo

ISHU YA FAINI KUTOKA CAF, YANGA YAGOMEA YAKATA RUFAA

  SHIRIKISHO la Soka Afrika, (Caf) limeipiga rungu ya faini ya milioni 11 Yanga kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kufanya fujo kwenye m...

JESHI LA SIMBA LINALOPEWA NAFASI KUWAVAA WAARABU KESHO
KOCHA KAZE AWAJIBU WALE WANAOBEZA UWEZO WAKE
WAARABU WA SIMBA WALIA NA JOTO LA DAR

 


SHIRIKISHO la Soka Afrika, (Caf) limeipiga rungu ya faini ya milioni 11 Yanga kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kufanya fujo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Rivers United pamoja na kuingiza mashabiki kwenye mchezo huo.

Ikumbukwe kwamba Septemba 12, Uwanja wa Mkapa baada ya dakika 90 kwenye mchezo wa awali ubao ulisoma Yanga 0-1  Rivers United, ilielezwa kuwa wapinzani hao wa Yanga walipeleka malalamiko Caf kuwa walifanyiwa vurugu pamoja na uwepo wa mashabiki kwenye mchezo ambao haukupaswa kuwa na mashabiki.

Taarifa kutoka Caf imeeleza kuwa Yanga walishindwa kujibu taarifa za tuhuma hizo za kuwafanyia fujo watu waliokuwa kwenye msafara wa Rivers United ya Nigeria pamoja na kubaini uwepo wa mashabiki uwanjani.

Akizungumza na Championi Jumatano,Mkuu wa Idara ya Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli aliweka wazi kuwa walipata barua hiyo ila wameshangazwa na hukumu hiyo jambo ambalo limewafanya wakate rufaa.

“Tulipokea barua Oktoba 5 na tulipaswa kuijibu, kabla hatujaijibu adhabu imetolewa, sababu ambazo zimetajwa tunaona kwamba ni suala la mashabiki hilo lipo chini ya Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) sisi Yanga hatuhusiki na kwa upande wa vurugu ilikuwa ni stewart ambao wanasimamia hivyo tumewaandikia barua Caf kukata rufaa juu ya suala hilo,” alisema Bumbuli.




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: ISHU YA FAINI KUTOKA CAF, YANGA YAGOMEA YAKATA RUFAA
ISHU YA FAINI KUTOKA CAF, YANGA YAGOMEA YAKATA RUFAA
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjnac2S4yD_bgtx24jnrBUq2siCG09qlTUeryfpl-92PHR08d_ADJvI-2yh6EwEhDniLGI-ZrWnUbz4-dDp3zTbmtgVO2anB1lzUbJuXIK1UN6LGPi6PdU-ElVgJOPVU_WEv-n3RGXkfJVljq0m4ZUd_kig7sZj2bJdXV_M1WhHaMlVb0GrwU75-RF7Bg=w640-h426
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjnac2S4yD_bgtx24jnrBUq2siCG09qlTUeryfpl-92PHR08d_ADJvI-2yh6EwEhDniLGI-ZrWnUbz4-dDp3zTbmtgVO2anB1lzUbJuXIK1UN6LGPi6PdU-ElVgJOPVU_WEv-n3RGXkfJVljq0m4ZUd_kig7sZj2bJdXV_M1WhHaMlVb0GrwU75-RF7Bg=s72-w640-c-h426
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/ishu-ya-faini-kutoka-caf-yanga-yagomea.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/ishu-ya-faini-kutoka-caf-yanga-yagomea.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy