Naibu Waziri Dkt Mabula Ahimiza Uhakiki Kwa Wamiliki Wa Ardhi
HomeHabari

Naibu Waziri Dkt Mabula Ahimiza Uhakiki Kwa Wamiliki Wa Ardhi

 Na Munir Shemweta, BUKOMBE Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wamiliki wa wa ardhi kujitok...

Serikali Yakamilisha Mifumo Ya Kidigitali Ya Usajili Na Utoaji Wa Vibali Kwa Wasanii
Waziri Mulamula Apokea Nakala Za Hati Za Utambulisho Za Balozi Wa Malawi
Habari Katika Magazeti ya Leo March 16

 Na Munir Shemweta, BUKOMBE
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wamiliki wa wa ardhi kujitokeza katika zoezi la uhakiki linaloendelea katika ofisi zote za ardhi nchini.

Alisema, uamuzi wa wizara yake kufanya uhakiki wa wamiliki wa ardhi ni kutaka kuwatambua wamiliki kwa majina yanayosomeka kwenye vitambulisho vya NIDA.


‘’Tumachotaka ni kukutambua kama wewe ni mmiliki wa kiwanja kilichopo Bukombe au Sumbawanga kwa majina yale yale yanayosomeka katika kitambulisho cha NIDA’’ alisema Dkt Mabula.

Akizungumza na viongozi pamoja na watumishi wa sekta ya ardhi katika wilaya ya Bukombe  mkoani Geita tarehe 15 Sept 2021 Naibu Waziri Mabula alisema, hatua ya kufanya uhakiki itaisaidia Wizara ya Ardhi kama serikali kupata kumbukumbu nzuri za watanzania wanaomiliki ardhi na kusisitiza kuwa hakuna ukomo kwenye umiliki na mtu mmoja anaweza kumiliki viwanja zaidi ya ishirini.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, kumekuwa na sintofahamu kuhusiana na zoezi hilo la uhakiki ambao baadhi ya watu wanasita na kufikiri serikali inataka kuwanyang’anya viwanja ambapo alisisitiza kuwa, lengo ni kutaka kuwatambua wamiliki kwa majina yao.  na kubainisha kwamba kama kuna majina ya watoto basi yatatenganishwa  vya kwako na vya watoto

‘’Tunachotaka ni kuondoa wamiliki bandia ambao hata ukiwatafuta huwapati kwa kuwa jina aliloandika siyo la kwake, na kama kuna majina ya watoto basi yatenganishwe na ya kwako’’ Dkt Mabula

Aidha,  alisema kuwa uhakiki unaoendelea utasadia pia kwenye masuala mazima ya mirathi hasa pale mmiliki atakapofariki huku akiwa hakutumia majina yake kwenye umiliki wa viwanja vyake na kuongeza kuwa, ikitokea mmiliki amefarikia basi familia yake ijue rasilimali zake.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Bukombe mkoani Geita Said Nkumba alimshukuru Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Angeline Mabula kwa kuitembelea wilaya hiyo na kukutana na viongozi pamoja na watumishi wa sekta ya ardhi ambapo alisema ujio wake utasiadia sana wilaya yake kujipanga katika masuala mazima ya ardhi hasa kwenyematumizi bora ya ardhi.

Nkumba pia aliunga mkono wazo la Naibu Waziri wa Ardhi kutaka halmashauri ya wilaya ya Bukombe kuangalia namna ya kuwakopesha viwanja watumishi wa serikali waliopo kwenye wilaya hiyo ili waweze kujikwamua katika masuala ya makazi.

‘’Kama huwezi kukopa basi hata kukopa kiwanja? Na nafikiri suala la kukopa viwanja ni jambo jema na ni vizuri tukaanza na watumishi kwa kuwa unalipa kidogokidogo na huwezi kujua unaweza kukaa hapa Bukombe mpaka unastaafu na sisi tunaona ni jambo jema’’ alisema Mkumba.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Naibu Waziri Dkt Mabula Ahimiza Uhakiki Kwa Wamiliki Wa Ardhi
Naibu Waziri Dkt Mabula Ahimiza Uhakiki Kwa Wamiliki Wa Ardhi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgORMYvwBgJ5zzhGANi-IMPL34ynquO6n8GwtMZ1Yufu-_0q_ZzyD-IjXHhloekKNY21uvZWKZ4hU7vZpDPxMevpijvT35ar4yOMOY0T_tGch2uf-y_KKsyXJ_m5fHLUS0hyphenhyphenABD3QJumMEx/s0/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgORMYvwBgJ5zzhGANi-IMPL34ynquO6n8GwtMZ1Yufu-_0q_ZzyD-IjXHhloekKNY21uvZWKZ4hU7vZpDPxMevpijvT35ar4yOMOY0T_tGch2uf-y_KKsyXJ_m5fHLUS0hyphenhyphenABD3QJumMEx/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/naibu-waziri-dkt-mabula-ahimiza-uhakiki.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/naibu-waziri-dkt-mabula-ahimiza-uhakiki.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy