KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA
HomeMichezo

KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA

 CEDRIC Kaze, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa kama angekuwa bado ndani ya benchi la ufundi angewafunga Simba kwenye mchezo wa m...

Simba ina imani na Kopunovic
Mchezaji wa zamani kuwania urais Fifa
Copa del Rey: Fernando Torres double sends Atletico through after aggregate win over Real Madrid

 CEDRIC Kaze, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa kama angekuwa bado ndani ya benchi la ufundi angewafunga Simba kwenye mchezo wa mzunguko wa pili.

Kaze alifutwa kazi Machi 7 baada ya kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Polisi Tanzania kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Yanga ilikuwa kwenye mwendo wa kusuasua ndani ya mzunguko wa pili ambapo ilicheza jumla ya mechi sita na kushinda moja, sare nne na ilipoteza mchezo mmoja kwa kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga ilikuwa Machi 4.

Kocha huyo amesema kuwa kwenye mchezo wa kwanza ambao alikiongoza kikosi hicho kusaka pointi tatu mbele ya Simba ndani ya Ligi Kuu Bara aliambulia sare ya kufungana bao 1-1 na kugawana pointi moja.

Mchezo wao wa mzunguko wa pili unatarajiwa kuchezwa Mei ambapo hatakuwa kwenye benchi la ufundi kwa kuwa ameshafungashiwa virago.

"Ingekuwa bado ningekuwa ndani ya benchi la ufundi la Yanga kuelekea kwenye mchezo wetu dhidi ya Simba Mei, ninaamini kwamba ningewafunga wapinzani wetu.

"Ninajua kwamba wengi hawawezi kuamini ila huo ni ukweli kwa sababu ninawajua wapinzani wetu vizuri na kwa namna ambavyo walikuwa bora walishindwa kuchukua pointi tatu kwetu.

"Mchezo wangu wa kwanza nilikuwa nina nafasi ya kupata pointi tatu ila aina ya wachezaji wangu walizidiwa mbinu mwishoni lakini kwa namna ambavyo nilikuwa nimewasoma basi mchezo wetu wa pili ningewafunga,"  anasema Cedric Kaze, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA
KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJ_aV5aBf6Ubp3OQheIEbaECUTkc7AujyTOqs3d5fqyjGWklx7_5F9u4JE6_Yg1QYT7o2GG6i5Ru7Aa8VxgCIV2B7KDUFwbvfFe-7pihdWsIYjvSEiipftTFt2uz3CWgntlTVnuQ-YnovO/w640-h453/Onyango+na+Ntiba.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJ_aV5aBf6Ubp3OQheIEbaECUTkc7AujyTOqs3d5fqyjGWklx7_5F9u4JE6_Yg1QYT7o2GG6i5Ru7Aa8VxgCIV2B7KDUFwbvfFe-7pihdWsIYjvSEiipftTFt2uz3CWgntlTVnuQ-YnovO/s72-w640-c-h453/Onyango+na+Ntiba.JPG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kaze-ningekuwa-kwenye-benchi-la-ufundi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kaze-ningekuwa-kwenye-benchi-la-ufundi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy