Burundi Yaiomba Tanzania Kuisemea Kimataifa
HomeHabari

Burundi Yaiomba Tanzania Kuisemea Kimataifa

Burundi imeiomba Tanzania kuendelea kuisemea nchi hiyo katika majukwaa ya Kimataifa ili iweze kuondolewa vikwazo vya kiuchumi ilivyowekew...

Serikali Haitavumilia Vitendo Vya Rushwa Ya Ngono Katika Taasisi Za Elimu-Prof. Ndalichako
Camon 18 Yavunja Rekodi Baada Ya Kuingia Sokoni
Mahakama yatupilia mbali ombi kukamatwa shahidi kesi ya Sabaya


Burundi imeiomba Tanzania kuendelea kuisemea nchi hiyo katika majukwaa ya Kimataifa ili iweze kuondolewa vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa na Jumuiya ya Ulaya jambo linalozorotesha  maendeleo ya kiuchumi kwa nchi hiyo.

Ombi hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimaendeleo wa Burundi, Mhe. Isidore Ntirampeba wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Sita wa Tume ya Pamoja ya Kudumu kati ya Tanzania na Burundi unaofanyika kwa ngazi ya wataalam mjini Kigoma tarehe 3 na 4 Machi 2021.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge amesema Tanzania itaendelea kuisemea Burundi katika majukwaa ya Kimataifa ili Burundi iondolewe vikwazo vyote vya kiuchumi ilivyowekewa ili kuipa nafasi nchi hiyo kuendelea na jitihada za kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Pamoja na hilo Balozi Ibuge ameihakikishia Burundi kuwa, Tanzania itaendelea na jitihada zake za kuisadia nchi hiyo kuingia katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ili iweze kuungana na nchi za ukanda huo katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

“Tanzania na Burundi zimeendelea kushirikiana kwenye Nyanja za Kimataifa na Kikanda kupitia Jumuiya za EAC, ICGLR, AU na Umoja wa Mataifa (UN). Ni kupitia ushirikiano huu, Tanzania itaendelea kuisemea Burundi katika majukwaa ya kimataifa ili iondolewe vikwazo vyote vya kiuchumi ilivyowekewa. Na kwa mara nyingine na uhakikishia ujumbe wa Burundi kwamba Tanzania itaendelea kuunga mkono ombi la nchi hiyo la kuwa mwanachama wa SADC” alisema Balozi Ibuge.

Katika hatua nyingine, Balozi Ibuge alieleza kwamba Mkutano wa Sita wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ni fursa nzuri ya kujadili masuala mbalimbali yenye manufaa kwa nchi zote mbili na kuwataka wajumbe wa mkutano huo kujipanga kutekeleza kikamilifu yale yote yatakayokubalika katika mkutano huo.

Mkutano huu umeanza kwa ngazi ya wataalam na utamalizika kwa ngazi ya Mawaziri tarehe 5 Machi 2021 ambapo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa AFrika Mashariki ataongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Burundi Yaiomba Tanzania Kuisemea Kimataifa
Burundi Yaiomba Tanzania Kuisemea Kimataifa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkdc15D9X_SBlkOALJPm7LsncWc2jr5_uj8BCMiagvhQtncU0fxwMVm1_T5paPc7QIfsDIlT3-NxZMK1bI3sF551R7fazmpbBPpxpbLj3y5zI73k4ang4pdp7vOYGX95DnC-ikBe2EVUDA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkdc15D9X_SBlkOALJPm7LsncWc2jr5_uj8BCMiagvhQtncU0fxwMVm1_T5paPc7QIfsDIlT3-NxZMK1bI3sF551R7fazmpbBPpxpbLj3y5zI73k4ang4pdp7vOYGX95DnC-ikBe2EVUDA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/burundi-yaiomba-tanzania-kuisemea.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/burundi-yaiomba-tanzania-kuisemea.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy