Serengeti Festival yaanza kwa Full Shangwe Dodoma, Show Kamili leo, Wasanii 70+ Jukwaa moja
HomeHabari

Serengeti Festival yaanza kwa Full Shangwe Dodoma, Show Kamili leo, Wasanii 70+ Jukwaa moja

Na Mwandishi Wetu- MAELEZO Kama uko Dodoma, Iringa, Singida, Manyara, Morogoro au hata Dar maana Shabiby lipo hadi saa tisa alasiri kam...

Siku ya UKIMWI: CBE Mwanza Campus World AIDS Day
Wananchi Mkoani Mbeya Watakiwa Kusalimisha Silaha Kwa Hiari
Majaliwa: Wakazi Waishio Maeneo Ya Viwanda Wapewe Kipaumbele Cha Ajira



Na Mwandishi Wetu- MAELEZO

Kama uko Dodoma, Iringa, Singida, Manyara, Morogoro au hata Dar maana Shabiby lipo hadi saa tisa alasiri kama hautafika Dodoma leo usinilaumu!!!!

Sasaaaa, sikiliza jana usiku wa kuamkia leo Jumamosi Februari 6, 2021, dunia ilisimama, burudani ilitambulishwa na wanaojua burudani waliburudika.

Hiyo ilikuwa show kabla ya shughuli yenyewe  leo (kwa lugha ya Shilole wanaita Serengeti Royal Pre-Party), ambapo wasanii 10 tu, kati ya zaidi ya 70 watakaotumbuiza leo, jana walitoa burudani ya kipato cha kati.

Kutoka kumbukumbu ya Awena ya Kassim Mganga, Mama Amina ya Marioo, Taabasamu ya Mr. Blue mpaka Number One ya Nandera aka Nandy, Serengeti Festival linakwenda kuwa Tamasha Number One nchini.

"Sasa kilichofanyika jana ni tone tu watu waje Jamhuri Stadium leo "walisema wasanii kadhaa waliopanda jukwaani.

Hiyo jana Shamra shamra za tamasha hilo zilitanguliwa na michezo miwili iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri  jijini Dodoma kushamirisha tamasha lenyewe linakalofanyika leo.

Mechi zote mbili ziliisha kwa sare ya kutokufungana (0-0) kwa timu za mashabiki wa timu za Simba na Yanga pamoja na timu za Wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao watatumbuiza na kushamirisha tamasha la Serengeti pamoja na timu inayoundwa na Viongozi wa Serikali ya wanachuo kutoka vyuo vikuu vilivyopo mkoa wa Dodoma.

Mechi ya kwanza ilihusisha timu iliyoundwa na mashabiki wa timu za Simba na Yanga ambao ni madereva waendesha bodaboda na bajaji jijini Dodoma ambapo timu ya mashabiki wa Yanga waliibuka kidedea kwa kuwafunga mashabiki wa timu ya Simba kwa mikwaju ya penati 8-7 baada ya timu hizo kutoshana nguvu kwa kutokufungana (0-0).  

Wakati mechi ya pili ilihusisha timu za Wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao watatumbuiza na kushamirisha tamasha la Serengeti dhidi ya timu inayoundwa na Viongozi wa Serikali ya wanachuo kutoka Vyuo Vikuu vilivyopo mkoa wa Dodoma ambapo timu ya Wasanii imeibuka kidedea kwa kushinda penati 3-2 huku mlinda mlango wa timu ya wasanii Khalid Ramadhan (Tundaman) alipangua penati moja.

Hivyo basi, leo usipange kukosa kwa mtonyo wa buku tatu (3000/) utapata burudan ya kipato cha kati yenye wasanii zaidi ya 70 kuanzia saa 10: 00 jioni.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serengeti Festival yaanza kwa Full Shangwe Dodoma, Show Kamili leo, Wasanii 70+ Jukwaa moja
Serengeti Festival yaanza kwa Full Shangwe Dodoma, Show Kamili leo, Wasanii 70+ Jukwaa moja
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUMtFi5vAbRjkWHKeGLbnUOVR0BS_CukvthWS0DompJuuo8XS0GLKrip0RntHKs0FOaullzmk6YIbyqIo0Gi1lpxTy9sRwxATToEcVViTHMbWgGJc0G-e0H4R8-pkg99CLMOOjQrWGWTrF/s16000/1.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUMtFi5vAbRjkWHKeGLbnUOVR0BS_CukvthWS0DompJuuo8XS0GLKrip0RntHKs0FOaullzmk6YIbyqIo0Gi1lpxTy9sRwxATToEcVViTHMbWgGJc0G-e0H4R8-pkg99CLMOOjQrWGWTrF/s72-c/1.png
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/serengeti-festival-yaanza-kwa-full.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/serengeti-festival-yaanza-kwa-full.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy