Waziri Kabudi Awataka Watumishi Wa Wizara Yake Kushiriki Katika Majukumu Na Kutathmini Utekelezaji Wake
HomeHabari

Waziri Kabudi Awataka Watumishi Wa Wizara Yake Kushiriki Katika Majukumu Na Kutathmini Utekelezaji Wake

Na mwandishi maalum, Morogoro. Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi amewataka watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria ku...

Bajeti Ya EAC Mwaka 2022/2023 Kuwa Usd Milioni 91.6
Hakuna uhaba wa mafuta nchini -Waziri Makamba
Prof. Makubi Asisitiza Ushirikiano Katika Uhamasishaji Wa Kuchangia Damu Salama.


Na mwandishi maalum, Morogoro.
Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi amewataka watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria kushiriki katika utekelezaji wa majukumu ya wizara na kutathmini mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu hayo kwa pamoja ii kuleta tija na ufanisi ndani  ya Wizara.

Prof.Kabudi alikuwa akizungumza na watumishi hao alipokuwa akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo lililofanyika mkoani Morogoro.

“Ni vyema kila mtumishi akashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa pamoja kama timu na kutathmini mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya Wizara,” alisema.

Prof. Kabudi pia amewataka watumishi hao kuhakikisha wanasoma na kuielewa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 -2025 na kupanga kuitekeleza, kufahamu vipaumbele vya serikali ya Awamu ya Sita na jinsi vinavyopaswa kutekelezwa, kujitambua, kutambua nafasi  na majukumu yao ndani ya Wizara na kuwa na  utendaji kazi wa pamoja kama timu.

Prof Kabudi pia ametaka kila mtumishi  wa Wizara  kushiriki katika utendaji kazi wa pamoja na kushiriki katika ujengaji wa taswira ya Wizara ili kuwa na taswira inayoendana na mabadiliko ya nchi inavyokwenda ikiwa ni pamoja na kuongeza kasi ya kutangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara ili umma upate kufahamu.

Amewataka watumishi hao kuhakikisha wanazingatia na kufuata sheria, taratibu na kanuni za Serikali kuwa waadilifu katika mawasiliano na kuongeza na kuimarisha mawasiliano na mashauriano ya kazi ndani ya Wizara ili kumfanya kila mtumishi kuelewa mambo yanayotekelezwa.

Prof. Kabudi pia amewapongeza watumishi hao kwa kutembelea ili kujionea kwa pamoja utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali ya ujenzi wa Bwawa la kufua Umeme wa Mwalimu Julius Nyerere huko Rufiji mkoani Pwani na Ujenzi wa Reli ya Kisasa kutokea  mkoani Morogoro – Kilosa hadi Dodoma na kuwasihi wawe mabalozi wazuri kuelezea yanayoendelea katika miradi hiyo na kuendelea kuiunga mkono Serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria walitembelea miradi ya ujenzi wa Bwawa la kufua Umeme wa Mwalimu Julius Nyerere huko Rufiji mkoani Pwani na walipokuwa njiani kurejea jijini Dodoma walitembelea Ujenzi wa Reli ya Kisasa unaoendelea kutokea Morogoro – Kilosa hadi Dodoma


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Kabudi Awataka Watumishi Wa Wizara Yake Kushiriki Katika Majukumu Na Kutathmini Utekelezaji Wake
Waziri Kabudi Awataka Watumishi Wa Wizara Yake Kushiriki Katika Majukumu Na Kutathmini Utekelezaji Wake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidMVnFHZpnvNYc9BEzBgxHFYAGDYwaWXIs6X8OC-aafC-h4DDCck4shPyI0gZ288mzvrQEhg4XLevqrHsO8WYiat1VvP2w-GQLLXDENmaRwcJE9_ir1WbH0TR6iT96ahFiwV8-Ae9OQr5W/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidMVnFHZpnvNYc9BEzBgxHFYAGDYwaWXIs6X8OC-aafC-h4DDCck4shPyI0gZ288mzvrQEhg4XLevqrHsO8WYiat1VvP2w-GQLLXDENmaRwcJE9_ir1WbH0TR6iT96ahFiwV8-Ae9OQr5W/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/waziri-kabudi-awataka-watumishi-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/waziri-kabudi-awataka-watumishi-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy