Wananchi Mkoani Mbeya Watakiwa Kusalimisha Silaha Kwa Hiari
HomeHabari

Wananchi Mkoani Mbeya Watakiwa Kusalimisha Silaha Kwa Hiari

TANGAZO LA USALIMISHAJI WA SILAHA KWA HIARI. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anapend...

Rais Samia : Madini yetu yataongezwa thamani hapa nchini
Ajali yaua watu tisa Iringa na kujeruhi watatu
Rufaa ya Ole Sabaya kuanza kusikilizwa Februari mwakani


TANGAZO LA USALIMISHAJI WA SILAHA KWA HIARI.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anapenda kuwatangazia wananchi wote wa Mkoa wa Mbeya kuwa zoezi la kusalimisha silaha kwa hiari limeanza tangu tarehe 01 Novemba, 2021 na litafanyika hadi tarehe 30 Novemba, 2021 kwa kuzingatia tangazo la serikali namba 774 la tarehe 29 Oktoba, 2021 lililotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.GEORGE SIMBACHAWENE.

Silaha hizo zitasalimishwa katika vituo vya Polisi, Ofisi za serikali za mitaa na ofisi za watendaji wa Kata kila siku kuanzia majira ya saa 02:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.

Mtu yeyote ambaye anamiliki silaha kinyume cha sheria ikiwa atasalimisha silaha hiyo katika kipindi kilichotangazwa atapewa msamaha na hatashitakiwa kutokana na uamuzi wake wa kusalimisha silaha hiyo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wananchi wote wa mkoa wa Mbeya kwa yeyote anayemiliki silaha kinyume cha sheria kusalimisha kwa hiari katika maeneo yaliyotajwa.

Aidha kwa yeyote anayemiliki silaha ya mtu aliyefariki au aliyepoteza sifa za kumiliki silaha hiyo afike kituo cha Polisi kwa ajili ya kufuata taratibu za kisheria na kuomba kumiliki silaha hiyo kihalali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya anatoa rai kwa viongozi wote wa serikali, viongozi wa dini zote, viongozi wa mila, machifu, MUJATA, wazee mashuhuri, viongozi wa kisiasa kwa ujumla wao wakiongozwa na viongozi wa chama cha mapinduzi kutoa ushirikiano wa dhati kwa mustakabali wa amani ya nchi yetu.

Mara baada ya muda uliotangazwa kupita, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, viongozi wa serikali za mitaa na kata litaendesha msako mkali nyumba kwa nyumba dhidi ya mtu/watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria na hatua kali za kisheria zitachukuliwe dhidi ya yeyote atakayekamatwa anamiliki silaha kinyume cha sheria.
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Wananchi Mkoani Mbeya Watakiwa Kusalimisha Silaha Kwa Hiari
Wananchi Mkoani Mbeya Watakiwa Kusalimisha Silaha Kwa Hiari
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgioWwoZz8NlIkJweNigSVhTyvPStKbsJGXapCvWd27YJnIPS9W2kteWZbC6mHILNeFoPc8vw_yET5VCsUBtze5gdRgMRQafaDQxXezA0yTAf2ooQ4t43N2mcFoSUBq0SM5ODvgmqeelB6_Y1PPh8LmLS-lSCLYdD36b-xszne5RYlX8AmucTvFgFIKJA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgioWwoZz8NlIkJweNigSVhTyvPStKbsJGXapCvWd27YJnIPS9W2kteWZbC6mHILNeFoPc8vw_yET5VCsUBtze5gdRgMRQafaDQxXezA0yTAf2ooQ4t43N2mcFoSUBq0SM5ODvgmqeelB6_Y1PPh8LmLS-lSCLYdD36b-xszne5RYlX8AmucTvFgFIKJA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/wananchi-mkoani-mbeya-watakiwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/wananchi-mkoani-mbeya-watakiwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy