Viongozi wa serikali washauriwa kuzima magari kubana matumizi ya mafuta
HomeHabari

Viongozi wa serikali washauriwa kuzima magari kubana matumizi ya mafuta

Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amewataka Mawaziri na Naibu Mawaziri pamoja na viongozi wengine kuzima magari yao wanapokuw...


Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amewataka Mawaziri na Naibu Mawaziri pamoja na viongozi wengine kuzima magari yao wanapokuwa hawayatumii/hawamo ndani ya magari ili kuunga serikali mkoano katika jitihada za kubana matumizi.

Amesema hayo bungeni jijini Dodoma akieleza kwamba kumekuwepo na utaratibu usio sahihi wa baadhi ya magari ya viongozi wanapokuwa bungeni wanayaacha yanaunguruma kwa muda wote wa vikao, jambo ambalo linaiongezea serikali mzigo wa gharama za mafuta.

“Tunatamani tuone magari ya kiongozi, yakishamshusha kiongozi, sio tu hapa bungeni, nchi nzima, awe ni mwenyekiti wa halmashauri, awe ni meya, awe ni katibu mkuu, ukiacha viongozi ambao kwa itifaki magari yao inabidi yaendelee kuwaka, magari mengine yakishamshusha kiongozi yazimwe na dereva ashuke,” amesema Dkt. Tulia.

Ameeleza kuwa gharama za mafuta zinaendelea kuwa kubwa kwa sababu ya kuacha magari yakiwaka hata yasipotumika wakati mwingine hadi kwa saa.

“Tunatamani tuone mabadiliko kwenye hilo eneo,” amesema Dkt. Tulia akieleza kwamba mtu anapokuwa anaendesha gari lake akiwa kwenye foleni anazima, sasa kwanini gari la serikali aliache linaunguruma wakati halitumiki.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Viongozi wa serikali washauriwa kuzima magari kubana matumizi ya mafuta
Viongozi wa serikali washauriwa kuzima magari kubana matumizi ya mafuta
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXSMv2_txqjqlIvyUh-blotTxJ504W5gGrOBMZF-1CBxBM7QnX9THTSL0JA5IvfdhiGGeJZ7hbVgu1Rl729STTAPYfwOLNCKJAgAd2z4k6I5JzpcJ0-0RK-Mj8Q5UiPRCPs3IM2vkG4ygkzsOvUvpr3xSiNyrk5hRHLzTmj9lxtbbFWhJObfxbSmvpog/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXSMv2_txqjqlIvyUh-blotTxJ504W5gGrOBMZF-1CBxBM7QnX9THTSL0JA5IvfdhiGGeJZ7hbVgu1Rl729STTAPYfwOLNCKJAgAd2z4k6I5JzpcJ0-0RK-Mj8Q5UiPRCPs3IM2vkG4ygkzsOvUvpr3xSiNyrk5hRHLzTmj9lxtbbFWhJObfxbSmvpog/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/viongozi-wa-serikali-washauriwa-kuzima.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/viongozi-wa-serikali-washauriwa-kuzima.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy