Mkutano Wa Dharura Wa Kamati Ya Mawaziri Wa Sadc Kufanyika Nchini Afrika Kusini
HomeHabari

Mkutano Wa Dharura Wa Kamati Ya Mawaziri Wa Sadc Kufanyika Nchini Afrika Kusini

Mkutano wa Dharura wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Extra-Ordinary M...

Umoja Wa Afrika Kuipatia Tanzania Chanjo Milioni 17 Za Corona
Watendaji Tekelezeni Maagizo Ya Serikali
Waziri Ummy Atoa Maamuzi Magumu Ujenzi Wa Makao Makuu Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe


Mkutano wa Dharura wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Extra-Ordinary Ministerial Committee of the Organ) ambao utahusisha pia Jamhuri ya Msumbiji na Nchi Zinazochangia Vikosi katika Misheni ya SADC iliyopo Msumbiji (SAMIM) utafanyika Pretoria, Afrika Kusini tarehe 03 Aprili 2022.

Mkutano huo ambao umetanguliwa na Mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu (Senior Officials meeting), unalenga pamoja na mambo mengine Kupokea na Kujadili Ripoti ya Maendeleo ya Misheni ya SADC nchini Msumbiji (SAMIM) pamoja na Mapendekezo mbalimbali kutoka kwa Makatibu Wakuu.

Itakumbukwa kuwa, wakati wa Mkutano wa dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC ulichofanyika jijini Maputo, Msumbiji mwezi Juni 2021, uliridhia kupelekwa kwa Misheni ya SAMIM (SADC Mission in Mozambique) nchini Msumbiji kwa ajili ya kuisaidia nchi hiyo kupamabana na ugaidi na vitendo vya unyanyasaji kwa wanawake na watoto vilivyokuwa vinaendelea kwenye baadhi ya Wilaya zilizopo kwenye Jimbo la Cabo Delgado.

Misheni hiyo ambayo ilianza kazi rasmi mwezi Julai 2021, inajumuisha Nchi Wanachama kumi (10) za SADC ambazo ni Tanzania, Angola, Malawi, Lesotho, Namibia, Afrika Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Botswana, Zimbabwe na Zambia.

Lengo kuu la misheni hiyo ni kukomesha matishio ya ugaidi, kuimarisha hali ya ulinzi na usalama, kurejesha utawala wa sheria kwenye maeneo yaliyoathirika kwenye Jimbo la Cabo Delgado na kuisadia Msumbiji kwa kushirikiana na Mashirika yanayotoa misaada ya kibinadamu ili kuyawezesha kutoa misaada kwenye maeneo yaliyoathirika na vitendo vya kigaidi ikiwemo kuwasaidia watu walioyakimbia makazi yao.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utaongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe. Viongozi wengine kutoka Tanzania watakaoshiriki Mkutano huo ni pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Meja Jenerali (Mst) Gaudence Milanzi na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mkutano Wa Dharura Wa Kamati Ya Mawaziri Wa Sadc Kufanyika Nchini Afrika Kusini
Mkutano Wa Dharura Wa Kamati Ya Mawaziri Wa Sadc Kufanyika Nchini Afrika Kusini
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpnQpD4Xc_UCMvo8__gP6NOJ3kXw08o-dql43BugEdfBdzs7KPOkFB9DoglvRCUoqSwVPZrFwC1ViNdVldt3h_zcag2-pSyF8K4Bp3A-jrfw-cuEFJGFPF4KCAlo0FQoVKzYXGcc0qdE6BwNKfNifqzwTU-dasVREfFdng3tZKnzm2Mhi5paIcuvA_xQ/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpnQpD4Xc_UCMvo8__gP6NOJ3kXw08o-dql43BugEdfBdzs7KPOkFB9DoglvRCUoqSwVPZrFwC1ViNdVldt3h_zcag2-pSyF8K4Bp3A-jrfw-cuEFJGFPF4KCAlo0FQoVKzYXGcc0qdE6BwNKfNifqzwTU-dasVREfFdng3tZKnzm2Mhi5paIcuvA_xQ/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/mkutano-wa-dharura-wa-kamati-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/mkutano-wa-dharura-wa-kamati-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy