Umoja Wa Afrika Kuipatia Tanzania Chanjo Milioni 17 Za Corona
HomeHabari

Umoja Wa Afrika Kuipatia Tanzania Chanjo Milioni 17 Za Corona

Umoja wa Afrika umeitengea Tanzania dozi milioni 17 za chanjo za UVIKO- 19 kupitia mpango wa Umoja huo wa kuzisaidia Nchi wanachama kupa...

Jeshi la Polisi latoa taarifa kwa vyombo vya habari
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo April 13
Tangazo La Nafasi Za Masomo Chuo Kikuu Kishiriki Cha Kumbukumbu ya Stefano Moshi (SMMUCo) Kwa Mkupuo Wa April 2022/2023


Umoja wa Afrika umeitengea Tanzania dozi milioni 17 za chanjo za UVIKO- 19 kupitia mpango wa Umoja huo wa kuzisaidia Nchi wanachama kupata chanjo kwa ajili ya Wananchi wake.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameyasema hayo Addis Ababa Nchini Ethiopia alipokutana kwa mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania waishio Nchini Ethiopia (Diaspora) waliotaka kufahamu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kupambana na UVIKO -19 ikiwa ni pamoja na suala la chanjo.

Aidha Balozi Mulamula amewataka Watanzania wanaofanya kazi katika Mashirika na Taasisi mbalimbali za Kimataifa kusaidia upatikanaji dozi nyingine za chanjo ya UVIKO 19 ili kuwawezesha Watanzania wengi  kupata chanjo hiyo kutokana na  mwamko wa Watanzania kuongezeka mara  baada ya kuzinduliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika tukio jingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Ethiopia Mhe Sahle – Work Zewde Addis Ababa nchini Ethiopia ambapo Tanzania na Ethiopia zimekubalina kuendelea kutumia ndege za shirika la Ethiopia kutangaza vivutio na kusafirisha Watalii kutoka mataifa mbalimbali kuja Tanzania.

Aidha Balozi Mulamula amemhakikishia Rais Sahle – Work Zewde kuwa Tanzania itaendelea kutekeleza maeneo yote ya ushirikiano ambayo Rais Zewde alikubaliana na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa ziara ya Rais huyo Chato nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na suala la kuwarejesha Nchini Ethiopia wahamiaji wanaoshikiliwa katika magereza mbalimbali.

Kwa upande wake Rais wa Ethiopia  Mhe. Sahle – Work Zewde amesisitiza kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Nchi hiyo hususani katika kutatua changamoto zinazozuia maendeleo miongoni mwa Mataifa hayo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Umoja Wa Afrika Kuipatia Tanzania Chanjo Milioni 17 Za Corona
Umoja Wa Afrika Kuipatia Tanzania Chanjo Milioni 17 Za Corona
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhP1Khto1Zwt5_kWZy7tslCQWRpnLTD8F2132wc1q0symfEzMQOz54EXfCYird_vufG1T8xPt2U-mGGHXHx7OyCh3sx0DWFI2_aclXjZy6i-6LTLmhMpJZ8cZl3iUJw8j58Sq_Duz2uj2H-/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhP1Khto1Zwt5_kWZy7tslCQWRpnLTD8F2132wc1q0symfEzMQOz54EXfCYird_vufG1T8xPt2U-mGGHXHx7OyCh3sx0DWFI2_aclXjZy6i-6LTLmhMpJZ8cZl3iUJw8j58Sq_Duz2uj2H-/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/umoja-wa-afrika-kuipatia-tanzania.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/umoja-wa-afrika-kuipatia-tanzania.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy