Waziri Ummy Atoa Maamuzi Magumu Ujenzi Wa Makao Makuu Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe
HomeHabari

Waziri Ummy Atoa Maamuzi Magumu Ujenzi Wa Makao Makuu Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe

Na. Angela Msimbira NJOMBE Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Ummy Mwalimu amebariki maamuzi ya Baraz...


Na. Angela Msimbira NJOMBE
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Ummy Mwalimu amebariki maamuzi ya Baraza la madiwani kuhusu ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Walaya ya Njombe kujengwa katika Kijiji Kidegembye Kata ya Kidegembye, Halmashauri ya wilaya Njombe, Mkoani Njombe.

Akiongea na Viongozi wa Mkoa wa Njombe, Wilaya, Baraza la Madiwani na Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Waziri Ummy amesema amebariki maamuzi hayo kufuatia mvutano wa muda mrefu uliokuwepo wa eneo la ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri hiyo ambao umedumu tangu mwaka 2019.

Waziri Ummy amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kuhakikisha ujenzi unaanza mara moja kwa kuwa fedha zaidi ya shilingi milioni 900 zimetolewa na Serikali hivyo kazi ya ujenzi iendelee bila kuchelwa.

Waziri Ummy amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Njombe kunaza taratibu za kuomba fedha shilingi bilioni moja ambazo zimetengwa na Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi.

Ameendelea kusema kuwa kwa sasa mjadala kuhusu ujenzi wa Makao Mkuu umefungwa kinachotakiwa ni kujenga mahusiano mazuri katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kuwataka madiwani kusimamia ujenzi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.

Amemuagiza Afisa Mipango Miji wa Halmashauri wa Wilaya kuhakikisha wanapanga mpango wa kabambe wa eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Makao Makuu ili iwe kama “satellite City”

Vilevile amewaagiza Halmashauri hiyo kuhakikisha wanabuni mkakati utakaoifanya Hospitali ya Matembwe inafanyakazi ya kutoa huduma za afya kwa wananchi

Aidha amewataka baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kusimamia ukusanyaji ya mapato ya ndani ya Halmashauri na kuhakikisha yanatekeleza kutatua kero za wananchi na kuwataka wakuu wa Idara kuhakikisha wanatenga asilimia 40 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Ummy Atoa Maamuzi Magumu Ujenzi Wa Makao Makuu Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe
Waziri Ummy Atoa Maamuzi Magumu Ujenzi Wa Makao Makuu Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjXPSlXVEfOcRZ0ExuG_RQ4-lODypSMqc5DWzZi8GwMlW3DmrXMlJwCg-WZ_bFr99EOXRhvu0-ByEglQkBx1NuX7_d0qwExsP2VgeNZdZF2RgMkvoTwscr2p7BDKtocH3dgEaWu341RSha0/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjXPSlXVEfOcRZ0ExuG_RQ4-lODypSMqc5DWzZi8GwMlW3DmrXMlJwCg-WZ_bFr99EOXRhvu0-ByEglQkBx1NuX7_d0qwExsP2VgeNZdZF2RgMkvoTwscr2p7BDKtocH3dgEaWu341RSha0/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/waziri-ummy-atoa-maamuzi-magumu-ujenzi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/waziri-ummy-atoa-maamuzi-magumu-ujenzi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy