CCM Yaanza Mchakato Wa Kupata Mrithi Wa Kiti Cha Spika Wa Bunge
HomeHabari

CCM Yaanza Mchakato Wa Kupata Mrithi Wa Kiti Cha Spika Wa Bunge

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kuanza mchakato wa kumsaka mrithi wa nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, J...

Jeshi la polisi Mkoa wa Simiyu Lakamata vifaa vya mradi wa umeme wa Rea vyenye thamani ya tsh27,984,244 vilivyokuwa vimeibiwa.
Internship Opportunities - Geita Gold Mining Ltd ....Bofya Hapa Kutuma Maombi-( 30 Posts ) .
Ole Sabaya Aanza Kujitetea Mahakamani

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kuanza mchakato wa kumsaka mrithi wa nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ambaye alijiuzulu tarehe 6 Januari mwaka huu.
 
Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 9 Januari, 2022 Visiwani Zanzibar, Katibu wa NEC- Itikadi Uenezi CCM, Shaka Hamidu Shaka amesema mchakato huo utaanza kuanzia tarehe 10 hadi 30 Januari mwaka huu.
 
Amesema hatua hiyo imekuja baada ya Ndugai kuandika barua kwa hiari yake na kuwasilisha kwa Katibu Mkuu wa CCM jijini Dodoma.
 
Amesema kufuatia hilo CCM kinawatangazia wanachama wake wote kwamba utaratibu wa ratiba ya mchakato wa kumpata mgombea atakayechaguliwa na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujaza nafasi ys Spika wa Bunge.
 
Amesema utaratibu huo ni kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inayotambua Spika kuwa ndio kiongozi mkuu wa Bunge na nafasi hiyo haiwezi kuwa wazi na Bunge likaendelea kufanya shughuli zake.
 
Akinukuu Katiba hiyo amesema; Ibara ya 84 (i) kutakuwa na Spika ambaye atachaguliwa na wabunge kutoka miongoni mwa watu ambao ni wabunge au wenye sifa za kuwa wabunge, atakuwa ndio kiongozi wa Bunge na atawakilisha Bunge katika vyombo na vikao vingine vyote nje ya Bunge.
 
“Ibara ya 84(viii) inasema hakuna shughuli yoyote itakayotekelezwa katika Bunge isipokuwa uchaguzi wa spika wakati wowote ambao kiti cha spika kipo wazi.
 
“Ibara ya 86(i) kimeeleza kutakuwa na uchaguzi wa spika katika kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge jipya, na katika kikao cha kwanza chochote mara baada ya kutokea kiti cha spika kuwa wazi.
 
“Kwa minajili hiyo, katika kutekeleza matakwa ya kikatiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, nichukue fursa hii kwa niaba ya chama kutangaza kwamba mchakato wa kujaza kiti cha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utatekelezwa kwa ratiba ifuatayo sambamba na vikao vya mchujo na uchaguzi wa wabunge wa CCM kabla ya kupelekwa bungeni kuendelea na utaratibu mwingine,” amesema.
 
Amesema kuanzia tarehe 10 hadi 15 zoezi la kuchukua fomu litaanza rasmi na tarehe 15 ifikapo alasiri zoezi hilo litakuwa limekamilika.
 
Amesema wale wenye sifa alizotaja wanakaribishwa kuchukua fomu katika makao makuu ya chama ofisi kuu, makao ya chama Dodom, ofisi ndogo Dar au Kisiwandui wakifika watapata maelekezo namna ya kcuhukua fomu hizo.
 
Amesema tarehe 17 Januri, 2022 Sekretarieti ya Halmashauri kuu ya Taifa itakutana kwa ajili ya kujadili wagombea na kuishauri Kamati Kuu ya Halmashuri kuu ya Taifa juu ya wagombea ambao wamejitokeza kuomba kiti hicho cha uspika.
“Tarehe 18 hadi 19 Januari kutakuwa na kazi ya kuchuja na kufanya uteuzi wa mwisho ambapo Kamati kuu ya Halmashauri Kuu itafanya kazi hiyo kwa eneo ambalo litaelekezwa.
 
“Kuanzia tarehe 21 hadi 30 Januari katika siku hizo, cocus ya chama ya wabunge wa CCM itapiga kura kumpata mgombea ambaye atakwenda bungeni kuomba kuchaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania,” amesema.
 
Amesema itategemea kama mgombea atakuwa wa CCM au vyama vingine lakini kwa upande wa CCM mchakato wake utakamilishwa na cocus ya CCM ambayo itampata mgombea mmoja atakayepelekwa bungeni.
 
“Nichukue fursa hii kuwataka watanzania wote ambao wanakidhi vigezo kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na CCM, kwamba wana nafasi na wana fursa kujaza nafasi hii,” amesema.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: CCM Yaanza Mchakato Wa Kupata Mrithi Wa Kiti Cha Spika Wa Bunge
CCM Yaanza Mchakato Wa Kupata Mrithi Wa Kiti Cha Spika Wa Bunge
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEi0WSeimy61hxyVF_Tzh1McMs-MvUHP4Zup1ptEAwzpvkPjtqiWcfVQaG3_FWlzrlroxsMfXrIMU6WJywlnF6oWxGUHmzWIX123MC0DBapJaYW8MdbO5I13udbcjItKd1FKtU_RkduCpIFzkY9wqX_sKml7GsasO1LToEh7n1fE1xc0TnQ0Zmbb1QRQmg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEi0WSeimy61hxyVF_Tzh1McMs-MvUHP4Zup1ptEAwzpvkPjtqiWcfVQaG3_FWlzrlroxsMfXrIMU6WJywlnF6oWxGUHmzWIX123MC0DBapJaYW8MdbO5I13udbcjItKd1FKtU_RkduCpIFzkY9wqX_sKml7GsasO1LToEh7n1fE1xc0TnQ0Zmbb1QRQmg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/ccm-yaanza-mchakato-wa-kupata-mrithi-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/ccm-yaanza-mchakato-wa-kupata-mrithi-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy