Dkt. Nchemba: Tanzania Kuendelea Kuwekeza Kwenye Sekta Ya Elimu
HomeHabari

Dkt. Nchemba: Tanzania Kuendelea Kuwekeza Kwenye Sekta Ya Elimu

Na Benny Mwaipaja, Dubai SERIKALI ya Tanzania imeihakikishia Jumuiya ya Kimataifa kwamba itaendelea kuwekeza rasilimali fedha kwa ajil...


Na Benny Mwaipaja, Dubai

SERIKALI ya Tanzania imeihakikishia Jumuiya ya Kimataifa kwamba itaendelea kuwekeza rasilimali fedha kwa ajili ya kuendelea elimu ili kuwa na jamii iliyoelimika kwa ajili ya kuimarisha rasilimali watu watakaochangia maendeleo ya nchi.

Ahadi hiyo imetolewa mjini Dubai na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kwenye kilele cha mkutano unaohusu uwekezaji kwenye sekta ya elimu katika karne ya 21 hasa baada ya janga la ugonjwa wa UVIKO-19 kuzitikisa nchini nyingi duniani.

Dkt. Nchemba amesema kuwa Serikali itaendelea kuongeza Bajeti ya Sekta ya Elimu kila mwaka kadri rasilimali fedha inavyopatikana na kuiomba jumuiya ya kimataifa kuchangia juhudi hizo za Serikali.

Alisema kipaumbele cha Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anayetakiwa kwenda shule anapata elimu bila vikwazo kwa kutoa elimu bila malipo huku akiboresha mazingira ya shule nchini kote.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alisema kuwa nchini Tanzania kuna utashi wa kisiasa wa kuendeleza elimu ambapo bajeti ya elimu imekuwa ikiongezeka kila mwaka na mpaka sasa imefikia zaidi ya asilimia 17 na kwamba huenda siku zijazo ikafikia asilimi 20 ya bajeti yote ya Serikali.

Mkutano wa masuala ya elimu ujulikanao kama WirED umewashirikisha wadau mbalimbali kutoka duniani kote ambapo hoja mbalimbali za kuboresha elimu, ikiwemo kuwawezesha vijana, na kuimarisha masuala ya teknolojia yamejadiliwa kwa kina katika mkutano huo.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Dkt. Nchemba: Tanzania Kuendelea Kuwekeza Kwenye Sekta Ya Elimu
Dkt. Nchemba: Tanzania Kuendelea Kuwekeza Kwenye Sekta Ya Elimu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhU2dLWkii_hW2_9Vci7FHy1VfiC96EVo4nlZdeM7rANsiKweKaX4UoOwNRz86gvmw9HxM2VY9JokFw5ZClDS4HbjlZsHk3CTmIkE-P_KTHl6jKw0U5AtUYI1PfiefDGhTOYmysCh56foQCsqmeKEeFzcIroyGnDtveSyPoF9mMIusZI89CJuCAXLOwow=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhU2dLWkii_hW2_9Vci7FHy1VfiC96EVo4nlZdeM7rANsiKweKaX4UoOwNRz86gvmw9HxM2VY9JokFw5ZClDS4HbjlZsHk3CTmIkE-P_KTHl6jKw0U5AtUYI1PfiefDGhTOYmysCh56foQCsqmeKEeFzcIroyGnDtveSyPoF9mMIusZI89CJuCAXLOwow=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/dkt-nchemba-tanzania-kuendelea-kuwekeza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/dkt-nchemba-tanzania-kuendelea-kuwekeza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy