Dkt Mabula Aonya Wathamini Kuepuka ‘Tegesha’
HomeHabari

Dkt Mabula Aonya Wathamini Kuepuka ‘Tegesha’

  Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Wathamini nchini kue...

Majaliwa: Tanapa, Wadau Wa Utalii Shirikianeni Kuitangaza Rubondo
Serikali Yatenga Bilioni 45 Kutekeleza Anwani Za Makazi Nchini
Upatikana Wa Saruji Nchini Ni wa Kuridhisha: Prof. Mkumbo


 Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Wathamini nchini kuepuka udanganyifu maarufu kama Tegesha wakati wa kufanya uthamini wa majengo na mali kwa ajili ya ulipaji fidia katika maeneo mbalimbali.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo tarehe 7 Desemba 2021 wakati akifunga Mkutano Mkuu wa Pili wa Mwaka wa Wathamini uliofanyika mkoani Dodoma.

Alisema, ni vizuri Wathamini wakati wa kazi zao wakawa makini na kuhakikisha wanaepuka udanganyifu wa aina yoyote ukiwemo ule wa Tegesha alioueleza kuwa  ulijitokeza sana katika  uthamini uliofanyika Mgodi wa North Mara-Nyamongo.

⁰"Kuweni makini wakati wote mnapokuwa uwandani na kuepuka udanganyifu kama uliofanyika North Mara-Nyamongo, mmea unapandwa usiku na unafanyiwa uthamini na kusababisha serikali kupoteza fedha na mchezo huu umefanyika sana, wote mnajua yaliyotokea tusingependa kama Wizara yajirudie " alisema Dkt Mabula.

Aliwaasa watumishi wote wa sekta ya ardhi na fedha wanaofanya kazi na Wathamini kuwa waaminifu ili wasiwashawishi wathamini kujiingiza kufanya kazi zisizozingatia uadilifu, sheria, kanuni na taratibu na kueleza kuwa ukiukwaji maadili unaleta sintofahamu ama kusababisha malalamiko yasiyo ya lazima kutoka kwa wateja.

Hata hivyo, Dkt Mabula aliitaka bodi ya Usajili Wathamini nchini kupunguza vikwazo vya usajili ambapo aliitaka kuharakisha zoezi la usajili kwa wale wote waliotimiza vigezo na kueleza kuwa, ucheleweshaji wowote unaofanyika unawakosesha haki katika utumishi ikiwa ni pamoja na kipanda vyeo.

Kwa sasa zaidi ya Wathamini 200 waliopewa mafunzo ya uthamini wanafanya mitihani ya usajili ya Bodi kwa ngazi mbalimbali ambapo baadhi yao wanakamilisha makala za utafiti ili kupata usajili kamili wakiwemo Wathamini wa Ofisi za Mikoa na Halmashauri.

Kupitia mkutano huo Mkuu wa Pili wa Wathamini, Naibu Waziri Dkt Mabula aliitaka Bodi ya Wathamini kusimamia kwa karibu makampuni yote ya uthamini ili yafanye kazi kwa weledi huku akisisitiza zile kesi zinazopelekwa kwenye bodi hiyo na Wizara kutolewa ufumbuzi mapema.

Akigusia kiasi cha fedha shilingi bilioni 50 zilizotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Ardhi kwa ajili ya mradi wa Kupanga, Kipima na Kumilikisha (KKK) katika halmashauri mbalimbali nchini Dkt Mabula aliwataka Wathamini kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kuzingatia maadili wakati wote wa kutekeleza mradi huo katika halmashauri.

Kwa upande wake Kaimu Msajili wa Bodi ya Wathamini nchini Joseph Shewiyo alimuahidi Naibu Waziri Dkt Mabula kuwa, Bodi yake itahakikisha inasimamia maadili kwa Wathamini pamoja na kusimamia makampuni yote ya uthamini ili yafanye kazi kwa weledi.

“Mhe Naibu Waziri Bodi inaahidi kuyafanyia kazi mambo yote uliyotuagiza ikiwemo kusimamia maadili kwa Wathamini pamoja na kuhakikisha Makampuni ya Uthamini yanafanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na weledi” alisema Shewiyo.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Dkt Mabula Aonya Wathamini Kuepuka ‘Tegesha’
Dkt Mabula Aonya Wathamini Kuepuka ‘Tegesha’
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhggEUu_w7rGdAlQ3uHWXUn9j_p6ojPRRH0QN4LG8JWKIrzjI1uamkRwmhTqCv5rdnKTpnCjmC4Qr-yoZzE0feM1EfArUA9kKczXSl8lz6yhfgU86G4rOdSykPWHHof0nXWFBgSKRTmZXZnJG3KX6sNU73p5zkVmdYC7trJpNMjUSY1t36InrP5zI2FiA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhggEUu_w7rGdAlQ3uHWXUn9j_p6ojPRRH0QN4LG8JWKIrzjI1uamkRwmhTqCv5rdnKTpnCjmC4Qr-yoZzE0feM1EfArUA9kKczXSl8lz6yhfgU86G4rOdSykPWHHof0nXWFBgSKRTmZXZnJG3KX6sNU73p5zkVmdYC7trJpNMjUSY1t36InrP5zI2FiA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/dkt-mabula-aonya-wathamini-kuepuka.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/dkt-mabula-aonya-wathamini-kuepuka.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy