Serikali Yatenga Bilioni 45 Kutekeleza Anwani Za Makazi Nchini
HomeHabari

Serikali Yatenga Bilioni 45 Kutekeleza Anwani Za Makazi Nchini

 Prisca Ulomi na Projestus Binamungu, Mwanza Serikali imetenga shilingi bilioni 45 za kutekeleza mpango wa anwani za makazi na postikodi...


 Prisca Ulomi na Projestus Binamungu, Mwanza
Serikali imetenga shilingi bilioni 45 za kutekeleza mpango wa anwani za makazi na postikodi nchini kwa kujenga miundombinu ya anwani hizo kwenye halamshauri 194 nchi nzima zilizopo Tanzania Bara na Visiwani

Hayo yameelezwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wakati akiwa ziarani mkoani Mwanza kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mpango huo kwenye Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiwa ni eneo la mfano ili kujifunza kwa lengo la kufanikisha utekelezaji huo ili kuzifikia halmashauri zote 194 nchini ambapo halmashauri 184 ni za Tanzania Bara na halmashauri kumi ni za Tanzania Visiwani

“Lengo ni kuhakikisha kuwa kila mtaa unakuwa na jina lake na kila nyumba iwe na namba yake, hii inarahisisha utendaji kazi wa Serikali hata ndani ya jamii kwenye shughuli zetu za kiuchumi, tunaongelea kuwa na uchumi wa kidijitali, uchumi wa kidijitali hauwezekani bila kuwa tumekamilisha mfumo huu wa anwani za makazi, tunamshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupatia shilingi bilioni 45 ndani ya Wizara yangu kwa zoezi hili tu,” amesema Dkt. Kijaji

Ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuwafikia wananchi kule walipo ili mwananchi anapopata tatizo, iwe ameunguliwa na moto pale alipo ni rahisi kuwapigia zimamoto na kuwaarifu mtaa na nyumba ulipo, au una mgonjwa unahitaji huduma ya gari ya wagonjwa, unaawarifu wanakufikia na kwa mwananchi aliyeagiza mzigo au kifurushi kutoka nje ya nchi hana sababu ya kwenda posta kufuata mzigo bali mzigo wako utaletwa mpaka ulipo ili wananchi watumie muda wao mwingi kujiletea maendeleo yao

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kazi hii ya utekelezaji wa anwani za makazi nchini nzima utatekelezwa na wananchi wenyewe waliopo kwenye maeneo hayo na itatoa ajira kwa wananchi hao na ametoa rai kwa wananchi kuwa tayari kujitokeza kutekeleza mpango huu wa anwani za makazi na postikodi

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa wananchi wana kiu ya kujulikana kwa kuwa sasa mitaa yao ina majina na nyumba zao zina namba ambapo mwananchi analetewa mzigo wake pale alipo kwa kuwa sasa anatambulika mahali anapoishi

Diwani wa Nyamagana, Biko Kotecha akizungumza kwa niaba ya wananchi wake ameipongeza Serikali kwa utekelezaji wa mpango wa anwani za makazi kwa kuwa mradi huu una tija kwa wananchi, wananchi wake wamefurahi kwa kuwa mwananchi akipata ajali anaeleza moja kwa moja mahali alipo na anapata huduma

Mwenyekiti wa Kamati ya Wataalam wa Anwani za Makazi na Postikodi, Hlamashauri ya Jiji la Mwanza ndugu Moses Seleki amesema kuwa jumla ya nyumba 108,000 zimefungwa namba za nyumba, nguzo 5,800 zimewekwa zenye vibao vya majina ya mitaa na nyumba 98,000 zimeingizwa kwenye mfumo wa anwani za makazi wa simu ya mkononi



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yatenga Bilioni 45 Kutekeleza Anwani Za Makazi Nchini
Serikali Yatenga Bilioni 45 Kutekeleza Anwani Za Makazi Nchini
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgyrkyv9oJ99a5sk-jI2fU4JCnPRfSoZnFpmSZQJrYz8wxDB3zob9MzlHzFvN0nkGwBcreBtzkKzh5PtO0Lp9IeE9WmMxW12DefweLgWj8hqIVL4rp0_TEzrqJyb4LTj3wCA1_3zjDt60YHHxPFNIOMhvSsw2UAgcKDpyXSMjteODmXD3QTJE03sQEurA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgyrkyv9oJ99a5sk-jI2fU4JCnPRfSoZnFpmSZQJrYz8wxDB3zob9MzlHzFvN0nkGwBcreBtzkKzh5PtO0Lp9IeE9WmMxW12DefweLgWj8hqIVL4rp0_TEzrqJyb4LTj3wCA1_3zjDt60YHHxPFNIOMhvSsw2UAgcKDpyXSMjteODmXD3QTJE03sQEurA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-yatenga-bilioni-45-kutekeleza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-yatenga-bilioni-45-kutekeleza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy