Waziri Mkuu Majaliwa awaonya waamuzi mpira wa Miguu
HomeHabari

Waziri Mkuu Majaliwa awaonya waamuzi mpira wa Miguu

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka waamuzi watakaochezesha mashindano ya mpira wa miguu ya jimbo la Ruangwa wawe makini na wajiepush...

Uadilifu Kuwezesha Ukuaji Wa Uchumi Wa Blue
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 10
Serikali yatangaza ajira mpya 6, 649 za Ualimu na Afya

 


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka waamuzi watakaochezesha mashindano ya mpira wa miguu ya jimbo la Ruangwa wawe makini na wajiepushe na vitendo vya rushwa.

“Waamuzi msiingize maslahi binafsi wala msijiingize kwenye rushwa kutoka timu yoyote, tunahitaji michezo hii ichezwe kwa jitihada za wachezaji wenyewe.”

Ametoa agizo hilo jana (Alhamisi, Agosti 19, 2021) alipokabidhi vifaa vya michezo kwa timu nane zilizofikia hatua ya robo fainali. Mashindano yalihusisha timu 38 kutoka katika jimbo hilo.

Vifaa alivyovitoa ni jezi na mpira mmoja kwa kila timu, kombe ambalo litagawiwa kwa timu itakayoibuka mshindi wa kwanza katika fainali zinazotarajiwa kufanyika Agosti 30, 2021.

Amesema lengo la kutoa vifaa hivyo ni kuwahamasisha vijana wanaopenda mpira wa miguu waweze kucheza kwa bidii na kuongeza tija. Amesema kwa sasa mpira wa miguu ni ajira.

Amewataka viongozi Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Ruangwa (RUDIFA) wasimamie vizuri mashindano hayo ili kuwawezesha vijana wanaoshiriki waweze kutimiza malengo yao.

Waziri Mkuu amesema mbali na kuleta afya na ajira kwa washiriki michezo pia ina tabia ya kuwaunga watu pamoja na kuwawezesha kujadili shughuli za maendeleo.

Mheshimiwa Majaliwa ameahidi kuunga mkono mipango inayofanywa na RUDIFA ili kuhakikisha sekta ya michezo inakuwa na mafanikio na kuwawezesha vijana wengi kujiajiri.

“Vijana wa Ruangwa jengeni wivu na mjitume sana ili muweze kupandisha viwango vyenu vya uchezaji na hatimaye muweze kupata nafasi ya kucheza katika vilabu vinavyoshiriki ligi kuu.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa RUDIFA Yussuf Mpame, amesema mashindano hayo ni muhimu kwa maendeleo ya mpira wa miguu wilayani Ruangwa kwani uwepo wake unafaida kubwa sana.

Aidha, Mwenyekiti huyo ametumia fursa hiyo kumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Ruangwa kwa msaada anaoutoa katika maendeleo ya michezo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mkuu Majaliwa awaonya waamuzi mpira wa Miguu
Waziri Mkuu Majaliwa awaonya waamuzi mpira wa Miguu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJG_OJcL9AzSj-AE6Pt6guLMn758MVUZ65rSzVpg9QnEvWeKnlIN_AKa0tAwzJn_tDQvKWDR1oFuSKCC0Q9QcLLQkL-EDOGjsqAS9ysjCEHZW-EiTLuACn3w4S9oe4mjZ7M0m222rzv5Lc/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJG_OJcL9AzSj-AE6Pt6guLMn758MVUZ65rSzVpg9QnEvWeKnlIN_AKa0tAwzJn_tDQvKWDR1oFuSKCC0Q9QcLLQkL-EDOGjsqAS9ysjCEHZW-EiTLuACn3w4S9oe4mjZ7M0m222rzv5Lc/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/waziri-mkuu-majaliwa-awaonya-waamuzi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/waziri-mkuu-majaliwa-awaonya-waamuzi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy