IGP Sirro Aionya CHADEMA na Wanaokusudia Kufanya Vurugu
HomeHabari

IGP Sirro Aionya CHADEMA na Wanaokusudia Kufanya Vurugu

Jeshi la polisi nchini limetoa onyo kwa mtu au kikundi cha watu watakaojaribu kuhamasisha mikusanyiko isiyo rasmi au kuandamana kwa namna...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Keo June 4
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo June 3
AUDIO : Killy – Roho


Jeshi la polisi nchini limetoa onyo kwa mtu au kikundi cha watu watakaojaribu kuhamasisha mikusanyiko isiyo rasmi au kuandamana kwa namna yoyote.

Akizungumza na wanahabari leo Jumatatu Agost 2,2021 Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Sirro amesema tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA  Freeman Mbowe na wenzake ziko chini ya mamlaka ya mahakama.


Mbowe na wenzake watatu, wanakabiliwa na mashtaka mbalimbali ikiwemo la kupanga njama za ugaidi na uhujumu uchumi, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Sirro amewaonya wale wote wanaokusudia kufanya maandamano tarehe 5 Agosti 2021, siku ambayo kesi hiyo itatajwa tena kutokufanya hivyo kwani “kuvamia mahakama ni sawa na kuvamia kambi ya jeshi.”

"Jeshi la polisi halitegemei mtu au kikundi cha watu kwa namna yoyote kutoa shinikizo kwa mamlaka ya mahakama au kwa mtuhumiwa Freeman Mbowe aachiwe "amesema Sirro.

"Jeshi la polisi linatoa onyo kwa mtu au kikundi cha watu kitakachojaribu kuhamasisha mikusanyiko isiyo rasmi au kuandamana au namna yoyote ile kutoa shinikizo lolote,"amesema.

“Chadema wanasema mwenyekiti wao (Mbowe) ameonewa, wanavyoona wao hawezi kufanya hivyo, sasa kama Mbowe ni mkweli na amamuamini Mungu waende wakamuulize jambo hili unasemaje.”

“Lakini kabla ya uchaguzi nilisema kuna watu wamepanga kuhakikisha uchaguzi haufanyiki, nilisema kuna watu wamepanga kulipua visima vya mafuta na nilisema wamepanga kuua viongozi na nilisema tutawakamata,” amesema Sirro

“Habari ya yeye wajue ni binadamu, anaweza kufanya makosa, tumempeleka mahakamani tuiache mahakama itimize wajibu wake.” amesema Sirro
 

Sirro amewataka viongozi wa dini na taasisi nyingine ziache kusema Mbowe anaaonewa na badaala yake wasubiri mahakama iamue.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: IGP Sirro Aionya CHADEMA na Wanaokusudia Kufanya Vurugu
IGP Sirro Aionya CHADEMA na Wanaokusudia Kufanya Vurugu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieA3wyk18l4c3gd2SbtOMWqjxa7KaJDFx_A1ymrpKz2Q3lRiHJvF-UI_6cLog76g__LTyntarVBLaRtzKtJX6D79f96buT0M2nBPwG8Fs-ISUy2b4qA1SxRN6vFKxyjBqQnX_QTecdxTGf/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEieA3wyk18l4c3gd2SbtOMWqjxa7KaJDFx_A1ymrpKz2Q3lRiHJvF-UI_6cLog76g__LTyntarVBLaRtzKtJX6D79f96buT0M2nBPwG8Fs-ISUy2b4qA1SxRN6vFKxyjBqQnX_QTecdxTGf/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/igp-sirro-aionya-chadema-na.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/igp-sirro-aionya-chadema-na.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy