Uhuru Kenyatta: Nilikuwa tayari kuachia urais ili kulinda damu za Wakenya
HomeHabari

Uhuru Kenyatta: Nilikuwa tayari kuachia urais ili kulinda damu za Wakenya

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amekiri kuwa alikuwa tayari kujiondoa katika kinyang’anyiro cha urais baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mba...


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amekiri kuwa alikuwa tayari kujiondoa katika kinyang’anyiro cha urais baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali ushindi wake wa Agosti 9, 2017.

Rais Kenyatta amesema alikuwa tayari kuchukua hatua hiyo kuzuia umwagikaji wa damu ambao ungesababishwa na machafuko ya baada ya uchaguzi.

Kiongozi huyo wa Kenya aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mamia ya viongozi wa kidini kutoka eneo la Mlima Kenya katika Ikulu ya Nairobi.

 “Mengi yamesemwa kunihusu. Baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa nilitaka kurudi Gatundu baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali ushindi wangu.

 “Ninathibitisha kwamba madai hayo ni ya kweli. Nilitaka kwenda nyumbani. Ikiwa kujiondoa kwangu kungeleta amani nchini, basi nilikuwa tayari kuondoka. Maisha ya binadamu ni muhimu kuliko wadhifa wa urais,” amasema Rais Kenyatta.

Naibu wa Rais wa Kenya, William Ruto aliwahi kuwaambia wazee wa Mlima Kenya katika kikao cha faragha kilichofanyika nyumbani kwake mtaani Karen, Nairobi, kuwa nusura ampige kofi Rais Kenyatta alipoonyesha dalili ya kutaka kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha urais mara baada ya ushindi wake kubatilishwa na Mahakama ya Juu.

Katika sauti iliyorekodiwa kisiri kutoka kwenye mkutano huo, Ruto anasikika akisema kuwa, alimlazimisha Rais Kenyatta kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba 26, 2017.

Wanasiasa wa muungano wa Azimio la Umoja wamekuwa wakitumia ufichuaji huo kumponda William Ruto katika kampeni zao, huku wakijaribu kumfanya Naibu wa Rais aonekane kama kiongozi mwenye uchu wa madaraka.

Alhamisi iliyopita, Ruto alijitetea kuwa hakuwa na nia ya kumpiga kofi Rais Kenyatta kama inavyodaiwa.

Hata hivyo Kenyatta alionekana kumshambulia Ruto kwa ‘kuwapotosha’ Wakenya kuwa “alitaka kuachana na urais ilhali wapinzani wake ndio wamekuwa wakidai kuwa alilenga kubadilisha Katiba kupitia mswada wa BBI ili asalia mamlakani”.

Rais Kenyatta amewataka viongozi wa kidini kutoka eneo la Mlima Kenya kutohadaiwa na propaganda za baadhi ya wanasiasa wakati huu Uchaguzi Mkuu unapokaribia.

Uchaguzi wa rais nchini Kenya umepangwa kufanyika Agosti 9 mwaka huu.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Uhuru Kenyatta: Nilikuwa tayari kuachia urais ili kulinda damu za Wakenya
Uhuru Kenyatta: Nilikuwa tayari kuachia urais ili kulinda damu za Wakenya
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEht4K5fFiaM3xuKophfX78TfnJfw1d2mAMp2r4KuHZREdaGieI7DyJIWd6-LcPJsK-oLVUFnA9UjDENEmzuDGdQkrYrlL9aX3Cu7em8l0VGNPW5M0rtpx7CqQua-8bdB0s1tYah4INe_Qs1Itqo8Ylw-RgIOrOyeK34KAfwOxUp3J-U3id2xIkJHzMpEQ/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEht4K5fFiaM3xuKophfX78TfnJfw1d2mAMp2r4KuHZREdaGieI7DyJIWd6-LcPJsK-oLVUFnA9UjDENEmzuDGdQkrYrlL9aX3Cu7em8l0VGNPW5M0rtpx7CqQua-8bdB0s1tYah4INe_Qs1Itqo8Ylw-RgIOrOyeK34KAfwOxUp3J-U3id2xIkJHzMpEQ/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/07/uhuru-kenyatta-nilikuwa-tayari-kuachia.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/07/uhuru-kenyatta-nilikuwa-tayari-kuachia.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy