Waziri Mbarawa :Sijaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Abiria La Mwanza
HomeHabari

Waziri Mbarawa :Sijaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Abiria La Mwanza

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), kumleta mhan...

Wabunge 50 kutua ACT. Je unawajua? Bofya hapa kuwaona
ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti
Shambulio Garissa:Washukiwa 5 wakamatwa


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), kumleta mhandisi mara moja kwenye mradi wa jengo la abiria linaloendelea kujengwa katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza.

Amesema jengo hilo la abiria linalojengwa kwa gharama ya takribani shilingi Bilioni 11 halijakidhi viwango vya kimataifa na kuna makosa mengine yanayohitaji watalaam zaidi kuweza kushauri namna gani ifanyike ili ikidhi viwango hivyo.

Prof. Mbarawa amesema hayo jijini Mwanza wakati alipofika kukagua ujenzi wa jengo hilo unaoendelea ambao mpaka sasa umefikia asilimia 85 na kutoridhishwa na mradi huo ambapo amesisitiza kuwa mradi huo umekosa vigezo vya kimataifa vinavyosimamiwa na Shirika la Kimataifa la Anga (ICAO).

“Mwenye dhamana ya viwanja vya ndege sio Mkoa wala Halmashauri bali ni TAA, nashangaa kusikia hakuna mhandisi anayesimamia jengo hili kutoka kwao hivyo basi naagiza watoke Dar es Salaam waje kusimamia hili jengo ili tupate thamani ya fedha na viwango vinavyostahili, hatutaki kufanya makosa alafu badae tuje tulaumiane”, amesema Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa majengo yanayostahili kujengwa katika viwanja vya ndege vya kimataifa ni tofauti na majengo mengine kwani yana viwango vyake vinavyostahili ambapo hapa havikufatwa.

“Tunatakiwa kujenga jengo liatakalodumu miaka 20 hadi 30 hatuwezi kujenga hivi hivi tu hapa tulipofikia wataalam waje waangalie nini kiboreshwe ili jengo likidhi mahitaji”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Aidha, Prof. Mbarawa ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuboresha viwanja vingi vya ndege hapa nchini na hiki Kiwanja cha Ndege cha Mwanza kinatarajiwa kuwa cha Kimataifa hivyo lazima fedha zinazotolewa thamani yake ionekane na kupitishwa kwa viwango vya Shirika la Kimataifa la Anga (ICAO).

“Sisi kama Serikali tutahakikisha fedha zinaletwa ila mwisho wa siku tunahitaji kuona thamani ya fedha na kila anayehusika asimame kwenye eneo lake”, amesema Prof. Mbarawa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel, ameeleza kuwa Mkoa imekwishaunda timu ya watalaam na tayari wameshaleta specification, michoro sahihi na kazi zinanedelea za kuboresha jengo hilo ili likidhi viwango vinavyostahili.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi wa Miundombinu wa mkoa huo, Mbunifu Majengo Chagu Nghoma, amemueleza Waziri kuwa jengo hilo la abiria litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria laki nne kwa mwaka, 

Ameongeza kuwa jengo litakuwa na ukumbi wa abiria wa ndani, wa kimataifa, ukumbi wa abiria mashuhuri, migahawa na maduka, ofisi mbalimbali za TRA, Uhamiaji, Afya, Polisi, Maliasili, Watumishi mbalimbali pia litakuwa na eneo la kuegesha magari takribani 320. 

Ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza ulianza mnamo tarehe 19/09/2021 na unatarajiwa kukamilika mwakani 2022.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mbarawa :Sijaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Abiria La Mwanza
Waziri Mbarawa :Sijaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Abiria La Mwanza
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgIPadjR8JjD0EGhH4hEH5SVq6kIwZ5EybC5OSIGtHjwx1f3MdvmjtIiahOHkHfD8PVffhzIWrT5ctdjpQMFwjTY_Hqj98Le-czXiMPI9RJ0CG5meqLcDS54vcp6C9W-SUIME6Ki_C1675ojD-aYyHK9nNIOJDBpAlS1wBA3IsQR6thT5txsAld3msOKg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgIPadjR8JjD0EGhH4hEH5SVq6kIwZ5EybC5OSIGtHjwx1f3MdvmjtIiahOHkHfD8PVffhzIWrT5ctdjpQMFwjTY_Hqj98Le-czXiMPI9RJ0CG5meqLcDS54vcp6C9W-SUIME6Ki_C1675ojD-aYyHK9nNIOJDBpAlS1wBA3IsQR6thT5txsAld3msOKg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mbarawa-sijaridhishwa-na-ujenzi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mbarawa-sijaridhishwa-na-ujenzi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy