Abu Dhabi Yaahidi Kuendelea Kuipiga Jeki Tanzania Kimaendeleo
HomeHabari

Abu Dhabi Yaahidi Kuendelea Kuipiga Jeki Tanzania Kimaendeleo

 Na Benny Mwaipaja, Abu Dhabi SERIKALI ya nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu ya Abu Dhabi imeahidi kuendeleza ushirikiano katika masuala ...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 05
Rais Samia Suluhu Hassan awasili nchini Kenya
Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Mkumbo Akutana Na Wasafirishaji, Waingizaji Na Watoaji Wa Mizigo Bandarini Na Kusikiliza Changamoto Zao


 Na Benny Mwaipaja, Abu Dhabi
SERIKALI ya nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu ya Abu Dhabi imeahidi kuendeleza ushirikiano katika masuala ya kiuchumi na kijamii na Serikali ya Tanzania ili kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Ahadi hiyo imetolewa mjini Abu Dhabi, Falme za Nchi za Kiarabu na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri anayeshughulikia masuala ya Rais, Sheikh Mansour bin Zayed Al Nanyan, baada ya kupokea ujumbe maalum kutoka kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uliowasilishwa kwake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, Ikulu ya nchi hiyo.

Akizungumza baada ya mazungumzo yao ya faragha, Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alisema kuwa Sheikh Mansour ameahidi kutuma ujumbe maalum nchini Tanzania kwa ajili ya kuangalia miradi mbalimbali ya kimkakati inayotokelezwa hivi sasa na mingine mipya kwa ajili ya kutoa fedha.

Dkt. Nchemba aliitaja miradi iliyowasilishwa kwa Serikali ya Abu Dhabi kuwa ni ile ya uendelezaji wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), mradi wa Ujenzi wa Bwala la Kuzalisha Nishati ya Umeme wa Mwalimu Julius Nyerere, ujenzi wa miundombinu ya barabara, viwanja vya ndege, kilimo na uvuvi pamoja na elimu.

“Kwenye sekta ya elimu tumejenga madarasa mengi, tumejenga vituo vya afya vingi sana na vingine viko vijijini lakini hatujajenga nyumba za watoa huduma wanaotakiwa kufanyakazi kwenye maeneo hayo” alisema Dkt. Nchemba.

Aidha, alisema kuwa wamejadiliana na Mhe. Sheikh Mansour bin Zayed Al Nanyan kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo nchini zinazotokana na Tanzania kuwa lango la kibiashara kwa nchi zisizozungukwa na bahari ambazo zikitumiwa vizuri kama vile uwepo wa nishati ya mafuta na gesi, zitaifanya nchi ipae zaidi kiuchumi.

“Maeneo mengine tuliyojadiliana ni namna ya kuitumia na kuishirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa njia ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) ili kuleta faida kwa pande zote mbili na wananchi kwa ujumla” aliongeza Dkt. Nchemba.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais-Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Jamal Kassim Ali, alisema kuwa mkutano wao na Naibu Waziri Mkuu wa Abu Dhabi uliangazia pia masuala ya Zanzibar ambapo miradi kadhaa ya kimkakati inayotaka ufadhili iliwasilishwa.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Manga Pwani kwa njia ya ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi, Ujenzi wa nyumba za makazi za gharama nafuu zipatazo 10,000 kwa ajili ya watumishi wa umma pamoja na wananchi wengine na uchimbaji wa mafuta na gesi.

“Zanzibar tuna fursa kubwa katika masuala ya uchumi wa blue ikiwemo uchimbaji wa mafuta na gesi, masuala ya uvuvi na utalii na wenzetu wamepiga hatua kubwa katika maeneo hayo, tukishirikiana nao katika maeneo hayo tutapiga hatua kubwa kiuchumi na kijamii” alisema Mhe. Ali.

Aliishukuru Abu Dhabi kwa kuendeleza ushirikiano na Tanzania hususan Visiwa vya Unguja na Pemba ambapo nchi hiyo ya Kiarabu ilifadhili ujenzi wa Hospitali ya Wete-Pemba na kwa kuahidi kuwa tayari kuendeleza ushirikiano huo katika miradi mipya iliyowasilishwa kwao.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Abu Dhabi Yaahidi Kuendelea Kuipiga Jeki Tanzania Kimaendeleo
Abu Dhabi Yaahidi Kuendelea Kuipiga Jeki Tanzania Kimaendeleo
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhC7rc3wNoEtPfY-UhptJq7UsnuEGuFqntGAfrqvPLU0jBy52oCC1qsf7Zu_o8WaTMKjv2nRq5dhFa3_-0ef4KRJ7hWO27jcMNKxmo7H4hWg_m0jRZlYwTZA19jj4gE9mysSRTaFgjq2TaxYtz3B9cfBXrnfp5jMzSWIdOHR2ZZXksBQ6q9GGtkOjwBVg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhC7rc3wNoEtPfY-UhptJq7UsnuEGuFqntGAfrqvPLU0jBy52oCC1qsf7Zu_o8WaTMKjv2nRq5dhFa3_-0ef4KRJ7hWO27jcMNKxmo7H4hWg_m0jRZlYwTZA19jj4gE9mysSRTaFgjq2TaxYtz3B9cfBXrnfp5jMzSWIdOHR2ZZXksBQ6q9GGtkOjwBVg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/abu-dhabi-yaahidi-kuendelea-kuipiga.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/abu-dhabi-yaahidi-kuendelea-kuipiga.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy