FERDINAND HATA HAELEWI KINACHOISUMBUA LIVERPOOL
HomeMichezo

FERDINAND HATA HAELEWI KINACHOISUMBUA LIVERPOOL

RIO Ferdinand beki wa zamani wa Manchester United na mchambuzi wa masuala ya michezo amesema kuwa bado anajiuliza kuhusu anguko la Klabu y...


RIO Ferdinand beki wa zamani wa Manchester United na mchambuzi wa masuala ya michezo amesema kuwa bado anajiuliza kuhusu anguko la Klabu ya Liverpool kwa msimu huu chini ya Kocha Mkuu, Jurggen Klopp.

Liverpool imekuwa kwenye mwendo wa kusuasua msimu huu baada ya msimu uliopita kuwa bora na iliweza kutwaa taji la Ligi Kuu England ambalo kwa sasa inaonekana wazi kwamba inalipoteza kwa kuwa ipo nafasi ya sita na pointi zake 52 vinara wakiwa ni Manchester City na pointi zao ni 74.

Klopp ameondolewa kwenye Champions League na Real Madrid baada ya kushindwa kupindua meza kwenye robo fainali ya pili pale Uwanja wa Anfield ubao uliposoma Liverpool 0-0 Real Madrid, mchezo wa kwanza walipoteza kwa kufungwa mabao 3-1 ugenini.

Beki huyo amesema kuwa bado haelewi ambacho kinaisumbua Liverpool kwa sasa anadhani labda wachezaji wamekuwa wakicheza chini ya kiwango ama majeruhi yanaitesa timu hiyo kwa sasa.

"Kuna maswali ambayo tumekuwa tukijiuliza kwamba kwa nini Liverpool imekuwa inafanya namna hii, labda inaweza kuwa sababu ya aina ya mbinu za mwalimu Klopp? Amekuwa na timu kwa miaka minne , mitano hivi hivyo anawajua wachezaji wake.

"Labda kuna mambo ambayo hayapo sawa itakuwa ni msimu mbaya tu ama kukosa wachezaji wake muhimu kikosini kwa kusumbuliwa na majeraha? 

Kwa sasa Liverpool yenye mshambuliaji Mohamed Salah inapeleka nguvu kwenye Ligi Kuu England ili kutetea taji lao.




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: FERDINAND HATA HAELEWI KINACHOISUMBUA LIVERPOOL
FERDINAND HATA HAELEWI KINACHOISUMBUA LIVERPOOL
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZXKIb0El9sWuome4i4HeBIkCKPM95_Cx7GQEQLFJ18ORU5gTxSqpMYec9x1Izfu_23N4Lb7dhCWoQ_MvPwRKNbozqxMz-LFjq0bS4CSLNnc8f2N-kK79jAlyOzN1YnAQBX00L_wNhy7Or/w640-h428/Salah+huzuni.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZXKIb0El9sWuome4i4HeBIkCKPM95_Cx7GQEQLFJ18ORU5gTxSqpMYec9x1Izfu_23N4Lb7dhCWoQ_MvPwRKNbozqxMz-LFjq0bS4CSLNnc8f2N-kK79jAlyOzN1YnAQBX00L_wNhy7Or/s72-w640-c-h428/Salah+huzuni.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/ferdinand-hata-haelewi-kinachoisumbua.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/ferdinand-hata-haelewi-kinachoisumbua.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy