Rais Samia Asikia Kilio cha Bei ya Mafuta....Atoa Maelekezo Mazito
HomeHabari

Rais Samia Asikia Kilio cha Bei ya Mafuta....Atoa Maelekezo Mazito

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza mkakati wa kubana matumizi ya Serikali katika bajeti ya matumizi ili kupata fedha za kupunguza makali...


Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza mkakati wa kubana matumizi ya Serikali katika bajeti ya matumizi ili kupata fedha za kupunguza makali ya ongezeko la bei ya mafuta linalosababisha kuongezeka kwa bei za bidhaa na huduma nchini.

Rais Samia ameyasema hayo jana Jumatatu Mei 9, 2022 katika taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari akisema Serikali imesikia kilio cha wananchi cha kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.

“Katika mwaka wa fedha unaoanza Julai mwaka huu tutachukua hatua mbalimbali za kikodi kuweka ahueni kwa wananchi.

“Hata hivyo, kutoa nafuu za kupanda kwa bei za mafuta hakuwezi kusubiri hadi mwaka huu wa fedha, nimeamua kwa hiyo wananchi waanze kupata nafuu kuanzia tarehe Mosi Juni.

Nimeelekeza kwamba, Serikali tujibane na tujinyime ili kupata fedha kutoka kwenye matumizi ya kawaida ya Serikali ili ziende kutoa nafuu za bei ya mafuta kuelekea mwaka wa fedha,” amesema Rais Samia.

Amemwagiza Waziri wa Nishati kutoa ufafanuzi kesho Bungeni kuhusu hatua hiyo, huku akimwelekeza Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba kutoa ufafanuzi wa kodi katika mafuta.

Amesema ongezeko la bei ya mafuta limetikisa nchi zote duniani, tajiri na masikini, zenye kuzalisha mafuta na zenye kuagiza na kwamba Tanzania haijasalimika.

“Novemba mwaka jana nilielekeza tupunguze tozo zinazotozwa na taasisi mbalimbali. Hatua hiyo ilisababisha Serikali kupungukiwa kwa mapato yake kwa kiasi ccha Sh102 bilioni.

Pamoja na hatua hizo bado nafuu haikupatikana kutokana na kasi ya kupanda bei,” amesema.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Samia Asikia Kilio cha Bei ya Mafuta....Atoa Maelekezo Mazito
Rais Samia Asikia Kilio cha Bei ya Mafuta....Atoa Maelekezo Mazito
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb6LpB1OHIcYZzGOmbSnlD-yV-17N5K1KW6Z5FsMsvoKydMpzz4KBBNPBTiRHqgqaXXZhjb_pKfsKCla-eQug9lOEjoRViD-Xcug-_nuqmPpAe8GEGWoqp538nZ-hrX6YeWpW6f1kf4wqS7FXpe4mo6L5Q3ELUlvkRsKdUTo8GFxdxOdE5mkTKtLtijA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb6LpB1OHIcYZzGOmbSnlD-yV-17N5K1KW6Z5FsMsvoKydMpzz4KBBNPBTiRHqgqaXXZhjb_pKfsKCla-eQug9lOEjoRViD-Xcug-_nuqmPpAe8GEGWoqp538nZ-hrX6YeWpW6f1kf4wqS7FXpe4mo6L5Q3ELUlvkRsKdUTo8GFxdxOdE5mkTKtLtijA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/rais-samia-asikia-kilio-cha-bei-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/rais-samia-asikia-kilio-cha-bei-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy