Biden atangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa kijeshi Myanmar
HomeHabari

Biden atangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa kijeshi Myanmar

Rais wa Marekani Joe Biden ametangaza kuidhinisha amri ya kiutendaji ya kuwawekea vikwazo vipya wahusika wa mapinduzi ya kijeshi ya Myanm...


Rais wa Marekani Joe Biden ametangaza kuidhinisha amri ya kiutendaji ya kuwawekea vikwazo vipya wahusika wa mapinduzi ya kijeshi ya Myanmar na kusisistiza kurejeshwa demokrasia na kuwaachia viongozi wa kiraia.

Rais wa Marekani Joe Biden ametangaza kuidhinisha amri ya kiutendaji ya kuwawekea vikwazo vipya waliohusika na mapinduzi ya kijeshi nchini Myanmar na kurejelea wito wake wa kurejeshwa demokrasia pamoja na kuwaachia viongozi wa kiraia.

Biden amesema amri hiyo itawezesha utawala wake "kuwawekea vikwazo haraka viongozi wa kijeshiambao walihusika na mapinduzi, maslahi yao ya kibiashara sambamba na jamaa zao wa karibu". Rais Biden ameongeza kuwa wiki hii Marekani itabainisha awamu ya kwanza ya wale wataoguswa na vikwazo hivyo na vilevile inawazuia majenerali nchini Myanmar kuweza kuzifikia mali zenye thamani ya dola bilioni 1 katika fedha za serikali ya Myanmar zilizoko Marekani.

"Wakati maandamano yakiongezeka, unyanyasaji dhidi ya wale wanaodai haki zao za kidemokrasia haukubaliki na tutaendelea kuupinga. Watu wa Burma wanapaza sauti zao, na ulimwengu unaangalia. Tutakuwa tayari kuweka hatua za ziada na tutaendelea kushirikiana na washirika wetu wa kimataifa kuhimiza mataifa mengine yajiunge nasi katika juhudi hizi. "

Mapinduzi ya kijeshi ya Februari mosi ambayo yalimuondoa mamlakani kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia Aung San Suu Kyi, yalitokea chini ya wiki mbili baada ya Biden kuapishwa

Nchi za magharibi zimelaani mapinduzi hayo, lakini wachambuzi wanasema kwamba jeshi la Myanmar halitoweza kutengwa kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, wakati kukiwa na uwezekano mkubwa wa China, India na mataifa jirani ya Kusini mwa Asia na Japan kutokata mahusiano na taifa hilo kutokana na umuhimu wake.

 

Credit:DW



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Biden atangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa kijeshi Myanmar
Biden atangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa kijeshi Myanmar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj723RObS-hVgkgmjOEqyOal5jLSQXzhtfV-VpsfJc93urS-dZiRW7rCHmnBbSqRHH2Zgw9RVHG57RYYoS8Ic8V6UKaatOosgq9-BDRjkB5ycQuiQdUxDpgRvuOaPByHnMLs7BXKKZMPMF6/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj723RObS-hVgkgmjOEqyOal5jLSQXzhtfV-VpsfJc93urS-dZiRW7rCHmnBbSqRHH2Zgw9RVHG57RYYoS8Ic8V6UKaatOosgq9-BDRjkB5ycQuiQdUxDpgRvuOaPByHnMLs7BXKKZMPMF6/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/biden-atangaza-vikwazo-dhidi-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/biden-atangaza-vikwazo-dhidi-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy