Waliovujisha Mitihani ya Utabibu Wizara Ya Afya Kuchukuliwa Hatua Kali
HomeHabari

Waliovujisha Mitihani ya Utabibu Wizara Ya Afya Kuchukuliwa Hatua Kali

Na WAMJW-MOROGORO Serikali kupitia Wizara ya Afya itawachukulia hatua wote watakaobainika walihusika katika kuvujisha mtihani wa kitaal...

Wizara Ya Mambo Ya Nje Kuendelea Kutoa Elimu Kuhusu Fursa Zitokanazo Na Eneo Huru La Biashara La Afrika
Tanzania Yapendekeza Mkakati Wa Pamoja Kupambana Na Ugaidi, Majanga AU
Membe Arudi Rasmi CCM....Shaka Aongoza Mapokezi na Kumkabidhi Kadi ya Uanachama


Na WAMJW-MOROGORO
Serikali kupitia Wizara ya Afya itawachukulia hatua wote watakaobainika walihusika katika kuvujisha mtihani wa kitaaluma wa mwaka wa pili wa matabibu pindi tu ripoti ya uchunguzi itakapokamilika na kuwasilishwa.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima wakati akizindua kituo cha Elimu masafa kilichopo Mkoani Morogoro.

“Serikali imeunda kamati ya uchunguzi iliyoshirikisha vyombo vyote, wakiwemo polisi na vyombo vyote vingine vinavyohusika na kuchunguza tuhuma kama hizi, ripoti ipo hatua za mwisho kukamilika, itasomwa wazi… maana wahalifu hao walichokitafuta watakipata…” Amesema Dkt. Gwajima.

Ameendelea kusema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Afya itachukua hatua hizo kwa kufuata Sheria, Kanuni na miongozo bila kuonea yoyote ili iwe fundisho kwa wengine wanaofanya vitendo hivi ambavyo ni kinyume na taratibu na Sheria  za nchi.

Mbali na hayo Dkt. Gwajima amesema kuwa, lengo la kufungua kituo hicho kwa njia ya mtandao ni kupunguza gharama za mafunzo na kuwafikia walengwa wengi zaidi katika kuendeleza ujuzi wao wa fani ya afya.

Hata hivyo ameyaelekeza Mabaraza kwa kushirikiana na Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kuyatambua mafunzo haya na kuhamasisha wataalamu wao kutumia mfumo huo wa mafunzo kwa njia ya kimtandao ili kujiendeleza na kukuza ujuzi wao.

“Ninayaelekeza Mabaraza kwa kushirikiana na Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kuyatambua mafunzo haya na  kuhamasisha wataalamu wao kutumia mfumo huo wa mafunzo kwa njia ya kimtandao ili kujiendeleza na kukuza ujuzi wao.”Amesema Dkt. Gwajima.

Aidha, Dkt. Gwajima amesema kuwa, mafunzo kwa njia hii ya elimu masafa yatapunguza gharama na kusaidia kukabiliana na upungufu wa watumishi wa afya uliopo kwa kuwawezesha kujiendeleza kitaaluma wakiwa kwenye vituo vyao vya kazi.

Kwa upande mwingine amewaomba wadau mbalimbali wa maendeleo kusaidia  kuboresha miundombinu ya kituo hiki ikiwemo maabara ya kisasa, hosteli kwa wanafunzi, madarasa, kumbi za mikutano na nyumba za wafanyakazi.

“Niwaombe wadau mbalimbali wa maendeleo kusaidia  kuboresha miundombinu ya kituo hiki ikiwemo maabara ya kisasa, hosteli kwa wanafunzi, madarasa, kumbi za mikutano na nyumba za wafanyakazi.”Amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Wizara ya Afya Dkt. Saitore Laizer amesema kuwa, Ujenzi wa kituo hiki umezingatia lengo na kitatumika kikamilifu ili tuweze kufikia malengo yaliyokusudiwa ambapo watumishi watapata fursa ya kujiendeleza wawapo maeneo yao ya kazi na kuongeza ufanisi kazini.

Aliendelea kusema kuwa, Mfumo huu umerahisisha utoaji wa mafunzo kwa watumishi wengi waliopo maeneo mbaimbali ya kutolea huduma, huku akiweka wazi kuwa, kutokana na changamoto ya UVIKO-19 mfumo huu umekuwa ukitumika kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa mafunzo ya ngazi ya kati nchini.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waliovujisha Mitihani ya Utabibu Wizara Ya Afya Kuchukuliwa Hatua Kali
Waliovujisha Mitihani ya Utabibu Wizara Ya Afya Kuchukuliwa Hatua Kali
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhA7bQv1IdLZcI1ybCeOvIPXdhYQHmu4H49cCJLNuDtMRGWFIgFdFE-otdDhmOjFxsfjFQ0d-mtpgSMipqRtvXu3lIB38_q1Rq9xc2aT6nQ75he1-hsVw4wA3aryDjzLwyC-eMQbmjWeFOtaVGN80YUsZkM1xr4k_86rACB78b67PE-X8U9_E78r6SgrQ=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhA7bQv1IdLZcI1ybCeOvIPXdhYQHmu4H49cCJLNuDtMRGWFIgFdFE-otdDhmOjFxsfjFQ0d-mtpgSMipqRtvXu3lIB38_q1Rq9xc2aT6nQ75he1-hsVw4wA3aryDjzLwyC-eMQbmjWeFOtaVGN80YUsZkM1xr4k_86rACB78b67PE-X8U9_E78r6SgrQ=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/waliovujisha-mitihani-ya-utabibu-wizara.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/waliovujisha-mitihani-ya-utabibu-wizara.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy