ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti
HomeHabariKitaifa

ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti

Baada ya chama hicho kuzinduliwa rasmi, nguvu yake imeelekezwa katika kujijenga na kujiimarisha zaidi,” Mwenyekiti wa ACT-Tanzan...

Chadema yajiengua UKAWA>>> Angalia yaliyojiri
CHEKI PICHA NA VIDEO ZA YANGA WAKIKABIDHIWA UBINGWA WA LIGI KUU NDANI YA UWANJA WA TAIFA
WABUNGE WAMTIMUA TENA WAZIRI NYALANDU


Baada ya chama hicho kuzinduliwa rasmi, nguvu yake imeelekezwa katika kujijenga na kujiimarisha zaidi,” Mwenyekiti wa ACT-Tanzania,  Anna Mghwira 
Chama cha ACT- Tanzania, kimesema hakina muda wa kufanya siasa za chuki na malumbamo dhidi ya vyama vingine vya siasa, badala yake kinajipanga vizuri na kuandaa mazingira ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao.
Mwenyekiti wa chama hicho Anna Mghwira, aliliambia gazeti hili mwishoni mwa juma kuwa, baada ya chama hicho kuzinduliwa rasmi Machi 29 mwaka huu,  nguvu yake sasa imeelekezwa katika kujijenga na kujiimarisha.
Alisema katika kujiimarisha, chama hicho kinatafuta wanachama, kwa kuwa kinatambua kuwa ni mtaji wa kujihakikishia ushindi katika uchaguzi mkuu, pamoja na kuandaa wagombea  kwa kuangalia uwezo wao kadri watakavyojitokeza.
“Mimi mwenyewe ni miongoni mwa wagombea ubunge, nitagombea Jimbo la Singida mjini na naamini kwamba nitaweza kupata nafasi hiyo kwa sababu ninafahamika kule ni nyumbani nilikozaliwa . Nimesoma huko, nimekulia huko na najua changamoto zinazotukabili wakazi wa kwetu na jinsi nitakavyoshiriki kukabiliana nazo nikiwa mbunge,”
Mghwira alieleza kuwa chama hicho kinajiimarisha, huku kikitambua kuwa kina wajibu wa kuendeleza ushirikiano na vyama vingine vya siasa, badala ya kujitenga na kuendesha shughuli zake kama kisiwa.
Mwenyekiti huyo, alitolea mfano siku ya uzunduzi wa chama hicho akisema kuwa kulikuwa na watu wengi kutoka vyama mbalimbali ambao walitaka kurudisha kadi za vyama hivyo hadharani na kuchukua kadi za ACT, lakini walisitisha shughuli hiyo kuepuka uhasama.
“Kuwa vyama tofauti haina maana kwamba tuwe maadui, kulikuwa na wanachama wapya siku ya uzinduzi (wa ACT) walitaka kuonyesha hadharani wanavyorudisha kadi za vyama vyao vya awali hatukuwapa nafasi hiyo, kwa sababu hatuoni kuwa hilo ni jambo la kuvutia kwetu,” alisema.
Kwa mujibu wa Mghwira siku hiyo walipokea wanachma wapya 2,000 na bado wanaendelea kupokea wanachama wengine kutoka vyama mbalimbali vya siasa lakini kwa siri.
Ingawa  Mghwira hakutaja watu, asilimia kubwa ya viongozi wa kitaifa wa chama hicho, akiwamo Zitto Kabwe ambaye sasa ni Kiongozi Mkuu wa chama hicho na Katibu Mkuu  Samson Mwigamba  na Profesa Kitila Mkumbo, wamejiunga na chama hicho baada ya kufukuzwa na vyama vyao.
“Pia katika kuonyesha nia yetu ya kuhitaji ushirikiano mwema wa kisiasa tuliwaalika viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani, ikiwemo Chadema na CUF,” alisema.  Alisisitiza kuwa Profesa Ibrahimu Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) ni miongoni mwa wasomi  na viongozi wa vyama vingine vya siasa walioalikwa kutoa mada katika uzinduzi wa chama hicho, lakini alipata udhuru hivyo hakufika.
“Hata hivyo tulifarijika kuona shughuli yetu ya uzinduzi wa chama ikifanyika vizuri na kwa amani,” alisema.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti
ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3g-kDR78n4L4Ax5Lqk2PvCKEJRq5wlxToPTfTkP2xFiUo296JqeVk0fisqNOXW72V8OwLZ3I_3iSUW5hzv7Pq6y4mIYPLcnnuf8HC3taTAt1vxvt_3fiec8G0HNQzGu0VlQfeCczoMS9a/s1600/act.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi3g-kDR78n4L4Ax5Lqk2PvCKEJRq5wlxToPTfTkP2xFiUo296JqeVk0fisqNOXW72V8OwLZ3I_3iSUW5hzv7Pq6y4mIYPLcnnuf8HC3taTAt1vxvt_3fiec8G0HNQzGu0VlQfeCczoMS9a/s72-c/act.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/04/act-tunajipanga-kushiriki-uchaguzi-mkuu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/04/act-tunajipanga-kushiriki-uchaguzi-mkuu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy