TGNP Mtandao Yawanoa Watendaji wa Serikali Juu ya Ukatili
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akiwasilisha mada katika semina kwa watendaji wa Serikali kuhusiana na changamoto za kesi za ukatili wa kijinsia.
HomeHabariKitaifa

TGNP Mtandao Yawanoa Watendaji wa Serikali Juu ya Ukatili

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akiwasilisha mada katika semina kwa watendaji wa Serikali kuhusiana na changamoto ...

Leo ndo leo, mbabe kujulikana
Watahiniwa kidato cha nne kuanza mitihani rasmi
Marekani yacharuka escrow;Tanzania yakosa mabilioni ya MCC, ni Dola 450 milioni



Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.

IMG_0022
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.



Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akiwasilisha mada katika semina kwa watendaji wa Serikali kuhusiana na changamoto za kesi za ukatili wa kijinsia.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akiwasilisha mada katika semina kwa watendaji wa Serikali kuhusiana na changamoto za kesi za ukatili wa kijinsia.
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.


MTANDAO wa Jinsia Tanzani TGNP umekutanisha baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria kujadili changamoto ya masuala ya sheria na sera katika kesi za ukatili wa kijinsia.
Semina hiyo kwa watendaji wa Serikali pia ilijadili nafasi za watendaji wa Serikali katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia ngazi ya jamii na kutoa mapendekezo ya baadae kukabiliana na changamoto hizo

Akizungumza katika semina hiyo akiwasilisha mada, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi alisema mfumo dume umeathiri jamii hivyo matendo mengi yanayofanywa kwa wanawake na wanaume kutegemeana na mtazamo wa jinsi zao na kuwa katika upendeleo zaidi na siyo katika nafasi ya usawa katika jamii.
“…Huu ni mfumo wala si mwanamke au mwanamme, ila ni mfumo unaohodhi madaraka, maamuzi, rasilimali nk.
Wengi huhusisha na ubabe, uonevu na ukatili ambapo katika mazingira halisi ubabe unafanywa sana na wanaumme,” alisema Bi. Liundi.
Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi (CRC) cha TAMWA, Glagness Munuo akiwasilisha mada katika semina hiyo
Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi (CRC) cha TAMWA, Glagness Munuo akiwasilisha mada katika semina hiyo
Aidha alisema lipo pengo la kijinsia tofauti; kitabia, ubora au kwa kiasi ya kutendewa kati ya wanaume na wanawake, na mara nyingine wasichana na wavulana kuhusiana na fursa za rasilimali/mali/huduma mahitaji, nafasi na mahitaji ya msingi katia jamii.

“…Majukumu ya kijinsia ni mitizamo inayojengeka katika familia/jamii kuhusu shughuli/majukumu ya wanawake na wanaume ambapo shughuli/majukumu fulani yanaoneka ni ya wanawake na mengine ni ya wanaume. Mitazamo hii inajengeka na kuathiriwa na umri, mila na tamaduni, dini, mazingira na mabadiliko ya kiuchumi, na kisiasa; kukua kwa maendeleo, sera za kijamii na kiuchumi…,” alisema

Aliongeza kuwa licha ya wanawake na wanaume wote wanashiriki katika shughuli za uzalishaji lakini kazi na shughuli azifanyazo mwanamke hazionyeshi matokeo yake waziwazi kama zile azifanyazo mwanaume katika jamii hali inayosababisha kupuuzwa kwa mchango wake katika jamii.
“…Mwanaume anakuwa na kazi ambazo nyingi ni rasmi kama vile uongozi na majukumu yake, na vile vile kufanya kazi zenye hadhi ya juu ukilinganisha na mwanamke anayefanya kazi nyingi za kuhudumia

Majukumu haya ni zile kazi ambazo wanajamii wanazifanya ili kuhakikisha upatikanaji na kuwepokwa vitu muhimu katika kuendeleza jamii, kwa mfano huduma za pamoja kama vile maji, huduma ya afya, elimu,” aliongeza Mkurugenzi huyo.
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watendaji wa Serikali kutoka idara za mahakama, maofisa wa Dawati la Jinsia na Watoto la Jeshi la Polisi pamoja na wanasheria walioshiriki katika semina hiyo iliyofanyika Double View Hoteli jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mratibu wa Kituo cha Usuluhishi (CRC) cha TAMWA, Glagness Munuo akiwasilisha mada katika semina hiyo alisema ukatili wa kijinsia ni jambo ambalo linawanyima uhuru wanaume, wanawake na watoto kufurahia haki za msingi za kibinadamu na kufanya wapendayo.

Aliongeza kuwa ukatili wa kijinsia unatokana na tofauti za kijinsia na baadhi ya mila na desturi potofu ambazo husababisha kuwepo kwa tofauti za kijinsia katika ngazi mbalimbali za jamii. Aidha alibainisha kuwa ukatili wa kijinsia unaendelea kufichwa kwa sababu unaonekana kuwa ni kitendo cha siri ambacho mtu mwingine hastahili kukifahamu.

Hata hivyo kutokana na kuwepo wanaharakati na vyombo vya habari suala la ukatili wa kijinsia kuliweka bayana inaeleweka zaidi kwa watu. Aliyataja madhara ya vitendo vya ukatili kuwa ni pamoja na wahusika kujeruhiwa vibaya, ulemavu, kifo, magonjwa ya zinaa na Ukimwi Matatizo ya afya ya uzazi. Mengine ni pamoja na Mimba kuharibika kwa akinamama, Hofu, Kutokwa na damu nyingi, Mimba zisizotarajiwa.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: TGNP Mtandao Yawanoa Watendaji wa Serikali Juu ya Ukatili
TGNP Mtandao Yawanoa Watendaji wa Serikali Juu ya Ukatili
http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2015/01/IMG_0050.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/tgnp-mtandao-yawanoa-watendaji-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/tgnp-mtandao-yawanoa-watendaji-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy