Stars maboresho mapya yatajwa
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij
HomeMichezoKitaifa

Stars maboresho mapya yatajwa

  Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij KOCHA wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars M...

Zaidi ya vijana 500 wakamatwa Tanzania
YANGA HII SASA SIFA! YAINYONGA POLISI 4-0 KOMBE LA MAPINDUZI
VIJANA WATATU WALIOTAKA KWENDA IKULU WAISHIA RUMANDE DAR!
KOCHA wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars Mart Nooij ameteua kikosi cha wachezaji 26 wa timu ya taifa ya maboresho kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya kirafiki dhidi ya Rwanda ‘Amavubi’ itakayopigwa kwenye uwanja wa CCM, Kirumba Januari 22, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana wakati akitangaza kikosi hicho kocha Nooij alisema kati ya wachezaji hao 10 ambao wanatoka katika mikoa ya Kanda ya Ziwa wataweka kambi Mwanza na wengine 10 wanaotoka Dar es Salaam wataweka kambi nyingine kabla ya kwenda Mwanza Januari 19 kuungana na wengine kwa ajili ya kambi ya pamoja.

“Mechi hiyo ni muhimu kwetu kwani wachezaji ambao watafanya vizuri tutawapandisha kucheza katika kikosi kikubwa,” alisema Nooij.
Wachezaji walioteuliwa ni Aishi Manula, Benedict Tinoko, Miraji Adam, Andrew Vicent, Michael Gadiel, Emmanuel Semwanda, Joram Mgeveke, Edward Charles na Adam Salamba.
Wengine ni Aboubakary Mohammed, Hassan Dilunga, Hussein Malombe, Shiza Ramadhani, Omari Nyenje, Kelvin Friday, Alfred Masumbakenda, Salim Mbonde, Atupele Green, Rashid Mandawa, Manyika Peter, Salum Telela, Hassan Banda, Mohammed Hussein, Said Ndemla, Said Makapu na Simon Msuva.

Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Vedastus Lufano, kiingilio kwenye mechi hiyo kitakuwa Sh 20,000 kwa viti maalumu (VIP), viti vya kawaida Sh 10,000 na mzunguko ni Sh 3,000.
Lufano aliwataja baadhi ya wachezaji wa Amavubi wanaotarajia kutua jijini Mwanza Januari 21 kwa ndege ya Rwanda Air, ni Marcel Nzarora, Olivier Kwizera, Sotel Kayomba, Ismail Nshutiyamagala , Emery Basiyenge na Michel Rushengoga.

Wengine ni Fitina Ombolenga, Janvier Mutijima, Haruna Niyonzima, Tean Baptista, Mugiraneza Savio, Nshuti Dominique, Patrick Sibomano, Jean Claude, Zagabe Andrew, Buteara Ernest , Sugira Danny, Ushengimana Betramed Iladukunda na Blenvue Mugenzi.
Lufano aliongeza kuwa taarifa iliyotumwa TFF kutoka Rwanda, Amavubi itaongozana na viongozi wake Stephen Costan, Vincent Mashami, Ibrahim Mugisha, Moussa Hakizimana, Nuhu Assouman, Boume Mugabe, Piere Baziki na Mkuu wa Msafara Bandora Felician.

Awali, Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF Boniface Wambura alisema mechi hiyo ni sehemu ya programu ya Kocha Mart Nooij kuiandaa timu hiyo kwa ajili ya mechi za mchujo za kuwania kufuzu kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN). Mechi za mchujo za michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Rwanda zinaanza Mei mwaka huu
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Stars maboresho mapya yatajwa
Stars maboresho mapya yatajwa
http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/nooij19_300_157.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/stars-maboresho-mapya-yatajwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/stars-maboresho-mapya-yatajwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy