Wakerwa shilingi kushuka thamani
Tanzania Sh.
HomeHabariBiashara

Wakerwa shilingi kushuka thamani

Tanzania Sh.                                                                            VS U.S Dollar Dar es Salaam. Wasomi...

RC Tabora Atoa Onyo Kwa Wavamizi Waliobaki Katika Hifadhi Ya Msitu Wa Isawima Wilayani Kaliua
Prof. Kabudi Atembelea Miradi Ya Kimkakati Inayotekelezwa Na Serikali Mkoani Kigoma
Kaze Afutwa Kazi Yanga



                                                                           VS
U.S Dollar

Dar es Salaam. Wasomi nchini wamezungumzia kuhusu kupanda kwa thamani ya Dola ya Marekani dhidi ya Shilingi ya Tanzania na kusema kunasababishwa na kuongezeka kwa uagizaji wa bidhaa kutoka nje na kusababisha fedha nyingi kutafutwa ili kulipia bidhaa hizo.


Bidhaa hizo ambazo huingizwa nchini hulipiwa kwa dola, hivyo ukusanyaji fedha nyingi huhitajika ili kukidhi bei zinazoelekezwa na wafanyabiashara wa nje. Hii husababisha kuwa na uhitaji mkubwa wa dola kuliko shilingi.


Thamani ya shilingi dhidi ya Dola ya Marekani jana iliuzwa kwa Sh1,813 katika maduka ya kubadilishia fedha. Hata hivyo kwa viwango vya Benki Kuu (BoT), dola iliuzwa kwa Sh1,768.


Mkuu wa Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDBS), Profesa Winieaster Andasom alisema taifa linakabiliwa na tatizo kubwa la uagizaji bidhaa nyingi kutoka nje kuliko zile zinazouzwa nje.


Alisema ili uchumi wa taifa ukue na thamani ya shilingi iwe na nguvu, lazima Watanzania waongeze uwezo wa kuuza bidhaa zao nje na kwa fedha za kigeni. Aliongeza kuwa kitendo cha uagizaji bidhaa kwa wingi kutoka nje kinafanya matumizi ya shilingi kudidimia na kupoteza thamani.


Aliitaka Serikali kuagiza bidhaa muhimu tu kama mashine, mafuta na zana ambazo hazizalishwi nchini. Lakini bidhaa nyingine kama mazao ya chakula na sukari, alisema hamna haja ya kuagiza kutoka nje. Profesa Andasom pia alibainisha kuwa thamani ya shilingi inaporomoka, kutokana na mfumuko mkubwa wa bei.


Alisema wananchi ndiyo waathirika wakubwa kunapotokea na mfumuko wa bei na maovu mengi huongezeka katika jamii.


Naye Profesa Humphrey Moshi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisisitiza kuwa uagizaji wa bidhaa nje ya nchi kuliko zinazozalishwa nchini kunayanufaisha mataifa mengine kwa sababu wanauza kwa thamani ya fedha yao.


Profesa Moshi aliongeza kuwa njia pekee ya kutatua tatizo hilo ni kuweka mikakati ya kuboresha kilimo ili mazao mengi yauzwe nje. Alisema ni muhimu kuwa na kilimo kisichotegemea mvua, badala yake kuwe na kilimo cha umwagiliaji.


Waziri wa Fedha na Uchumi, Saada Mkuya alikiri kupanda kwa Dola ya Kimarekani na kusema kuwa, “hili liko wazi kwamba bidhaa zinazoingizwa nchini kutoka nje ya nchi ni nyingi kuliko zinazozalishwa nchini kwenda nje ya nchi.”


Aliongeza: “Kinachotakiwa ili dola isiendelee kupaa ni kuhakikisha tunazalisha bidhaa zenye ubora ili ziende kwa wingi nje ya nchi na hapo tutaweza kupambana na kupanda kwa dola.”
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Wakerwa shilingi kushuka thamani
Wakerwa shilingi kushuka thamani
http://images.delcampe.com/img_large/auction/000/186/042/176_001.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/wakerwa-shilingi-kushuka-thamani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/wakerwa-shilingi-kushuka-thamani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy