Waziri aiagiza OSHA kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yenye ajali,magonjwa mengi
HomeHabari

Waziri aiagiza OSHA kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yenye ajali,magonjwa mengi

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Kazi,Vijana,Ajira na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameagi...

Habari kubwa Magazetini Kenya leo July 29, 2024
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo July 28, 2024
Warembo wanaounda kundi la Tango Supreme kutumbuiza Dar usiku wa leo


Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Kazi,Vijana,Ajira na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ameagiza Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yanayoongoza kwa matukio ya ajali na magonjwa pamoja na kubainisha visababishi vyake ili kuwezesha uandaaji wa mkakati wa kudhibiti visababishi hivyo.

Ametoa agizo hilo alipokuwa akifungua kikao cha pili cha baraza la wafanyakazi wa OSHA kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kupitia bajeti ya mwaka 2021/2022.

“Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mtendaji Mkuu inaonesha taasisi yenu imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ambayo yametokana na maboresho mbali mbali ambayo yamekuwa yakifanyika na serikali ikiwemo kuondoa baadhi ya tozo ambazo zilionekana kuwa kero.Hivyo, nawaagiza kuendelea kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuweza kufikia lengo letu la kupunguza ajali na magonjwa yatokanayo na kazi na kuleta ustawi wa Taifa letu,” alieleza Mhagama.

Waziri huyo wa Nchi aliwashauri wajumbe wa kikao hicho kufanya majadiliano katika kikao hicho kwa hekima na busara na hatimaye kutoka na maazimio muhimu ambayo yatafanyiwa kazi ili kutimizi malengo ya taasisi.

Aidha, aliitaka taasisi ya OSHA kuendelea kubuni mifumo mbali mbali ya Tehama ambayo itaboresha utoaji wa huduma kwa wadau pamoja na kuweka taratibu za huduma ambazo ni rafiki kwa wadau ili kuendana na maelekezo ya serikali.

Awali wakati akimkaribisha Waziri ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika kikao hicho, Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda, amesema maboresho ambayo yamekuwa yakifanyika na serikali katika sekta ya biashara na uwekezaji ikiwemo kuondoa baadhi ya tozo, yamepelekea taasisi hiyo kupata mafanikio makubwa ikiwemo kuongeza usajili wa maeneo ya kazi kutoka 5,300 hadi 20,000 kwa kipindi kati ya mwaka wa fedha 2014/2015 na 2020/2021.

Kwa upande wao mwakilishi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Taifa, Fidelis Athuman na Mjumbe wa Baraza hilo, Joyce Mwambungu, wameipongeza serikali na uongozi wa OSHA kwa maboresho ya utendaji ambayo yamekuwa yakifanyika kutokana na ushirikishwaji wa watumishi kupitia vikao vya mara kwa mara vya baraza la wafanyakazi.

Kikao hiki ambacho ni cha pili cha baraza la nne la wafanyakazi wa OSHA pamoja na masuala mengine, kilikuwa na agenda kuu ya kupitia bajeti ya mwaka  wa fedha ujao (2021/2022).

Mabaraza ya wafanyakazi katika taasisi mbali mbali za umma yapo kwa mujibu wa Sheria Na. 19 ya Mabaraza ya mwaka 2003 ambayo iliundwa kupitia Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 1970. Lengo likiwa ni kuleta ushirikishwaji baina ya menejimenti na watumishi katika kufanya maamuzi yanayohusu utendaji wa taasisi husika.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri aiagiza OSHA kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yenye ajali,magonjwa mengi
Waziri aiagiza OSHA kufanya tathmini ya maeneo ya kazi yenye ajali,magonjwa mengi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_BtQpfdtzrZS8srQnQaRfrh_UvFOVjbRozZR581l53pfko6I1POPnF6BzvB0Te1CID7kyAsUB60ZBFyfnpnWEQcLoIeI9sXZq8VkjOun48Nret1rGIhzOCJm57JqsiR_8Q7UP4bK7NWxo/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi_BtQpfdtzrZS8srQnQaRfrh_UvFOVjbRozZR581l53pfko6I1POPnF6BzvB0Te1CID7kyAsUB60ZBFyfnpnWEQcLoIeI9sXZq8VkjOun48Nret1rGIhzOCJm57JqsiR_8Q7UP4bK7NWxo/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/waziri-aiagiza-osha-kufanya-tathmini-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/waziri-aiagiza-osha-kufanya-tathmini-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy