Tanzania Yapokea Msaada Wa Dawa, Vifaa Tiba Kutoka Nchini Misri
HomeHabari

Tanzania Yapokea Msaada Wa Dawa, Vifaa Tiba Kutoka Nchini Misri

Na. Wizara ya Afya – Dar es Salaam Serikali kupitia Wizara ya Afya imepokea msaada wa dawa pamoja na vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh: M...


Na. Wizara ya Afya – Dar es Salaam

Serikali kupitia Wizara ya Afya imepokea msaada wa dawa pamoja na vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh: Mil. 864 vitavyosaidia katika kupambana dhidi ya magonjwa mbalimbali kutoka katika Serikali ya Misri.

Msaada huo umetolewa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es salaam kupitia kwa Balozi Misri nchini Tanzania Mhe. Mohamed Gaber Abouelwafa na kupokelewa na katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi kwa niaba ya Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya.

Akipokea msaada huo, Prof. Makubi amesema, msaada huo umeletwa baada ya ziara ya kikazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutembelea nchini Misri mnamo mwezi November mwaka jana (2021).

“Tunamshukuru sana Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Tanzania pamoja na Serikali ya Misri kwa kushirikiana na Tanzania hasa katika kuboresha Sekta ya Afya kwa kusaidia mahitaji mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.”Amesema Prof. Makubi.

Aidha Prof. Makubi amesema msaada huo utaenda kuwasaidia wananchi wenye uhitaji katika vituo mbali mbali vya kutolea huduma za afya nchini.

Kwa upande wake Balozi wa Misri nchini Tanzania Mohamed Gaber Abouelwafa amesema kujitoa kwa Serikali ya Misri, kusaidia Sekta ya Afya ni kutokana na jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan katika kuwaletea maendeleo wananchi, ikiwemo kuboresha Sekta ya Afya nchini kwa kupambana dhidi ya magonjwa.

“Serikali ya Misri itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kusaidia Maendeleo ya Watanzania, hasa katika kuboresha Sekta ya Afya, hii inatokana na nia njema ya Mhe. Rais Samia katika kuleta maendeleo kwa wananchi, hususan katika kuboresha Sekta ya afya.” Amesema Mhe. Balozi Abouelwafa.

Kwa uongozi makini chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali ya Misri imetoa ahadi kuendelea kusaidi Sekta ya Afya nchini kwa kuendelea kuleta Dawa pamoja na vifaa tiba kwaajili ya kupambana dhidi ya Magonjwa mbalimbali.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Tanzania Yapokea Msaada Wa Dawa, Vifaa Tiba Kutoka Nchini Misri
Tanzania Yapokea Msaada Wa Dawa, Vifaa Tiba Kutoka Nchini Misri
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiUzCDxCx_1v7EoeE85veddzRgDqAQOdmFe9_fbdUeiAcyEJFZkTVRU-oIc-RZqcxCjrBshX12VCWfq0vOHtFvv_zY5pEYyKKmAGTCZTV9jCURt8AALsYGjE5drCzQuxGVsBBcezyEkHZtmv_G3p4BjyUQb5pEUXTgY01j3Ahrnt0TfN9dhRvBKHj-n2g=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiUzCDxCx_1v7EoeE85veddzRgDqAQOdmFe9_fbdUeiAcyEJFZkTVRU-oIc-RZqcxCjrBshX12VCWfq0vOHtFvv_zY5pEYyKKmAGTCZTV9jCURt8AALsYGjE5drCzQuxGVsBBcezyEkHZtmv_G3p4BjyUQb5pEUXTgY01j3Ahrnt0TfN9dhRvBKHj-n2g=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/tanzania-yapokea-msaada-wa-dawa-vifaa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/tanzania-yapokea-msaada-wa-dawa-vifaa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy