Maadili Sio Kazi ya Viongozi wa Dini Tu – Prof. Willy Komba
HomeHabari

Maadili Sio Kazi ya Viongozi wa Dini Tu – Prof. Willy Komba

Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) imetoa rai kwa walimu nchini kuzingatia maadili katika utumishi wao kwani kazi ya ualimu bila maadili ha...

RC Makalla: Hakuna Panya Road Atakaesalimika Dar es Salaam
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo May 03
Rais Samia Atoa Msaada Wa Vyakula Kusherekea Sikukuu Ya Eid El Fitr


Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) imetoa rai kwa walimu nchini kuzingatia maadili katika utumishi wao kwani kazi ya ualimu bila maadili haijakamilika.

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu, Prof. Willy Komba ameyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na Waandishi wa Habari juu ya maadili ya kazi ya Ualimu.

Prof. Komba amesema kuwa elimu kwa ujumla wake imejikita katika maadili hivyo, bila maadili hakuna elimu kwani inawezekana kwenda shule hadi elimu ya juu lakini kama mtu hana maadili atakuwa amesoma lakini hajaelimika.

“Elimu inaenda sambamba na maadili, tunachoona kinachoendelea madarasani, Walimu wetu wengi wanajikita zaidi katika kutoa maarifa kulingana na somo analofundisha lakini suala la maadili wamewaachia viongozi na walimu wenye vipindi vya dini, hii sio sawa kwani kazi ya ualimu ikiweka maadili pembeni inakuwa haijakamilika”, alisema Prof. Komba.

Prof. Komba amefafanua makosa mazito yaliyokithiri kwa Walimu ikiwemo utoro, kugushi vyeti, uhusiano wa kimapenzi, ukaidi na ulevi ambapo kati ya mwaka 2020 hadi 2021, jumla ya makosa ya walimu yalikuwa 1,795 ambapo kwa mwezi Julai hadi Septemba, 2021 makosa ya walimu yalikuwa 184.

Amesisitiza kuwa, adhabu zote zinazotolewa kwa Walimu zinaendana na Kanuni na Tararibu za Tume na kwamba Tume hiyo inajitahidi kutenda haki hivyo, kwa wale ambao hawaridhiki na maamuzi wanaruhusiwa kukata rufaa kwa Kamati ya Nidhamu ya Wilaya, Tume pamoja na kukata rufaa kwa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Prof. Komba amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kibali cha kuwapandisha madaraja walimu 126,346 pamoja na kurekebisha mishahara yao kwa wakati.

Vile vile amewashukuru Walimu kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kutoa elimu na kusimamia miradi mbalimbali ya sekta ya elimu kwani pamoja na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo bado viwango vya ufaulu vinaongezeka.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Maadili Sio Kazi ya Viongozi wa Dini Tu – Prof. Willy Komba
Maadili Sio Kazi ya Viongozi wa Dini Tu – Prof. Willy Komba
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhfxOgNnV9ywlFShkVxUpvbx6N5aVfL1RS_4wWfS0J3_ZElp68VcDJGCmRCCgMvqaPl0TFja5NjsMc2aTIO1n1D-x6E2mhmWBA-GePQvS0mH9CfOqqucsjKZGRCPNATn2sPOUGBpR1ukTL4bQ9H2kGbmTxR8q7SrOZn6jQMqy0g1EEXrdKdsPqsh9bUMQ=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhfxOgNnV9ywlFShkVxUpvbx6N5aVfL1RS_4wWfS0J3_ZElp68VcDJGCmRCCgMvqaPl0TFja5NjsMc2aTIO1n1D-x6E2mhmWBA-GePQvS0mH9CfOqqucsjKZGRCPNATn2sPOUGBpR1ukTL4bQ9H2kGbmTxR8q7SrOZn6jQMqy0g1EEXrdKdsPqsh9bUMQ=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/maadili-sio-kazi-ya-viongozi-wa-dini-tu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/maadili-sio-kazi-ya-viongozi-wa-dini-tu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy