NAWAKUMBUSHA WACHEZAJI WAZALENDO, WAKATI UMEWADIA SIO MWISHONI
HomeMichezo

NAWAKUMBUSHA WACHEZAJI WAZALENDO, WAKATI UMEWADIA SIO MWISHONI

MOJA ya timu ambayo imekuwa gumzo katika usajili wake kwa  ajili ya msimu ujao ni Mtibwa Sugar ya Turiani mkoani  Morogoro. Gumzo linato...


MOJA ya timu ambayo imekuwa gumzo katika usajili wake kwa ajili ya msimu ujao ni Mtibwa Sugar ya Turiani mkoani Morogoro.


Gumzo linatokana na Mtibwa Sugar kuonekana wamebadilika na kuachana na ule mfumo wa kusajili wachezaji makinda ambao wamekuwa wakiwakuza na baadaye kufaidika kwa kuwauza katika klabu mbalimbali nchini.


Safari hii, Mtibwa Sugar wanaonekana wameamua “kazikazi”, maana wanasajili kikosi kwa ajili ya kushindana katika Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho. Hata kama watakuwa wameanza ligi vibaya lakini kuna nafasi ya kufanya vizuri.


Ligi ndiyo imeanza, ni mapema sana kusema nani kashinda aukashindwa kufanya vizuri kwa kuwa ligi inazunguka kwa muda mwingi sana.



Inawezekana Mtibwa watakuwa tofauti na mbele watafanya vizuri. Kikubwa kinahitajika ni kuendelea kurekebisha kila kinachoonekana kilikuwa si sahihi.


Tuachane na Mtibwa Sugar, ninachotaka kulenga zaidi ni kwamba tumeona Ligi Kuu Bara ndio imeanza na mengi yanaanza kutengenezwa na majibu yatapatikana siku ya mwisho ambako kila mtu atakuwa akipiga hesabu zake.


Wachezaji wazalendo wameshindwa kufanya vizuri katikamsimu uliopita na hakika wageni walitawala kwa kiasi kikubwa na wakapata mafanikio makubwa kwa kiasi kikubwa.


Vigumu kuelezea kwa wepesi, mfano ukiona mfungaji bora ni John Bocco lakini utaona karibu yake waliofunga mabao mengi zaidi ni wageni na hata waliofanya vizuri katika ligi kuu zaidi ni wageni.


Wageni ndio wachezaji wameipa sifa Ligi Kuu Bara kwa kuuzwa kwa bei kubwa zaidi wakitokea Simba na Yanga. Na unaona wale waliouzwa wameuzwa katika ligi kubwa zaidi Afrika za Morocco na Misri.


Idadi ya wazalendo ni zaidi ya asilimia 80 kwa wageni walio katika ligi kuu lakini jiulize kwa nini mafanikio yao yanakuwa ni makubwa kwa zaidi ya asilimia 90 zaidi ya wazawa ambao ni wengi zaidi.


Hata katika vikosi vya Yanga, Simba na Azam FC, wageni ndio wanatawala zaidi katika vikosi vya kwanza. Jiulize, hatuna wazawa wenye uwezo kama hao wageni wanaotokea Zambia, Mali au DR Congo hata Burundi tu!


Basi huu ndio wakati mwafaka wa wachezaji wazalendo kuanza kujipima na wajue utakapofika mwisho wa msimu kutakuwa na suala la hesabu nini kimepatikana.


Kama huu ndio mwanzo na ndio ligi imeanza, wachezaji wazalendo wanapaswa kujua umefikia wakati wa kubadilisha mwenendo na kushindana. Ligi ndio imeanza na hii iwe kuanzia mechi ya kwanza badala ya kusubiri mwishoni.


Isije ikawa mwisho kabisa ndio linaanza suala la hesabu kwamba vipi inawezekanaje wageni wanaendelea kutamba.


Hakuna ubishi, kama mfungaji bora akawa mzalendo tena, beki bora, kiungo bora, kipa bora na ikiwezekana hata watoa pasi au waliookoa wawe wazalendo kwa kuwa wingi wao wanaweza kuonyesha huo ubora.


Lazima wachezaji wazalendo wajue ligi yao ni sehemu yao ya kuwasaidia kupanda na kufanikiwa kufanya vizuri na ikiwezekana kupata nafasi ya kwenda mbele kimaendeleo.


Wazawa wanapaswa kuona haya au aibu na haya mambo ambayo yanawafanya waonekane wa kawaida sana.


Ushindani sahihi ni sehemu ya kuwafanya watu wakue zaidi,wafanikiwe na wasonge zaidi na ikiwezekana wafanye bora zaidi. Wapi wazawa watafanya vizuri zaidi ya hapa kwao. 

Na kama watasubiri mwishoni mwa msimu ufike, basi kila msimu utaishia wao wakiwa wanaburuza mkia.

Imeandikwa na Saleh Ally



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: NAWAKUMBUSHA WACHEZAJI WAZALENDO, WAKATI UMEWADIA SIO MWISHONI
NAWAKUMBUSHA WACHEZAJI WAZALENDO, WAKATI UMEWADIA SIO MWISHONI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpYuvjg8sCnUMHui5Cdlyctve8mA9OKaD0b6IZ7VBHzWZA1zVh7aXqVyQ2coAtAwz4FYFOLxLNOYjL9Q0s8KDrI_Y2P7Aen7e6RvpAirq2lnH6SYSWROv8D-DSb3rlQo0uFflZVo441Q5o/w640-h640/240816451_508034437131835_7214412164532954239_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpYuvjg8sCnUMHui5Cdlyctve8mA9OKaD0b6IZ7VBHzWZA1zVh7aXqVyQ2coAtAwz4FYFOLxLNOYjL9Q0s8KDrI_Y2P7Aen7e6RvpAirq2lnH6SYSWROv8D-DSb3rlQo0uFflZVo441Q5o/s72-w640-c-h640/240816451_508034437131835_7214412164532954239_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/nawakumbusha-wachezaji-wazalendo-wakati.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/nawakumbusha-wachezaji-wazalendo-wakati.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy