Kamishna Mkuu TRA Awapongeza Wanamichezo Kwa Kuibuka Washindi Shimmuta
HomeHabari

Kamishna Mkuu TRA Awapongeza Wanamichezo Kwa Kuibuka Washindi Shimmuta

Na Mwandishi wetu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania amewapongeza watumishi wa Mamlaka hiyo ambao ni wanamichezo kwa kuibuka wa...

Serikali Yatoa Maagizo Kwa Wamiliki Viwanda Vya Chuma Nchini
Sekretarieti Ya SADC Ya Utatu Yakutana Kwa Dharura
Wizara ya Afya yaanza utekelezaji wa maboresho huduma za matibabu kwa Wazee


Na Mwandishi wetu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania amewapongeza watumishi wa Mamlaka hiyo ambao ni wanamichezo kwa kuibuka washindi katika michuano ya SHIMMUTA iliyokuwa ikitimua vumbi hivi karibuni Mkoani Morogoro kwa kutwaa vikombe vitano vya ushindi katika michezo mbalimbali.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya wanamichezo hao Bw. Kidata alisema kuwa, juhudi ambazo wamezifanya watumishi hao ni kielelezo cha kuwa na nidhamu na ushirikiano siyo tu katika majukumu yao ya kikazi bali hata baina yao wenyewe.

“Ushindi huu mliouleta unaonyesha dhahiri kwamba mnazingatia maadili ya msingi yanayotuongoza ambayo ni Weledi, Uwajibikaji na Uadilifu kwa sababu bila mambo haya matatu msingefanikiwa kuja na ushindi huu mkubwa, ninawapongeza sana,

Napenda kuwapa taarifa nzuri wanamichezo wote kwamba, nimetoa maagizo ya kufanya matengenezo ya uwanja wetu wa mazoezi uliopo eneo la Kurasini hapa Dar es Salaam na nimetoa maelekezo kwamba ifikapo Mwezi Juni, 2022 nikabidhiwe uwanja huo ili mpate uwanja mzuri wa kufanyia mazoezi,” alisema Bw. Kidata.

Katika mapokezi hayo Kamishna Mkuu Kidata alikuwa na mgeni wake Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato ya Uganda (URA) Bw. John Musinguzi ambaye aliitembelea TRA kwa ajili ya kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Kamishna Mkuu wa TRA kuhusu masuala ya ushirikiano wa kimkakati hususani katika suala zima la ukusanyaji mapato ya Serikali.

Pamoja na kuwapongeza wanamichezo hao, Kamishna Mkuu huyo wa URA amesema kwamba, watafanya mazungumzo ili iandaliwe mechi ya kirafiki kati ya TRA na URA kwa lengo la kuimarisha afya ya mwili na kuongeza mahusiano mema baina ya ofisi zetu mbili.

“Hongereni kwa ushindi ambao mmeupata ila ningependa zaidi watumishi wa TRA wafanye mechi ya kirafiki na watumishi wa URA ili kujenga ushirikiano na kuimarisha afya zetu,” alisema Bw. Musinguzi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Michezo wa TRA, Bw. Zahor Salum amemshukuru Kamishna Mkuu na menejimenti nzima ya TRA kwa kuwaruhusu, kuwaamini na kuwawezesha kushiriki michuano hiyo ya SHIMMUTA ambapo ameongeza kuwa bila kuwezeshwa na uongozi huo wasingeweza kupata ushindi huo mnono.

Mashindano ya SHIMMUTA ya mwaka huu yalianza tarehe 13 Novemba na kuhitimishwa tarehe 27 Novemba, 2021 yakishirikisha taasisi 44 za Serikali ambapo katika mashindano hayo, TRA imeibuka kidedea katika michezo mitano ambayo ni mpira wa miguu, bao, draft – Wanaume, draft – Wanawake pamoja na mchezo wa karata.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kamishna Mkuu TRA Awapongeza Wanamichezo Kwa Kuibuka Washindi Shimmuta
Kamishna Mkuu TRA Awapongeza Wanamichezo Kwa Kuibuka Washindi Shimmuta
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiEZt5638HL7BH04JhKzbuZgZgg825xSajdlLa4PpvOyYwgBsbcrPk3ITjS1_7rkmBZzkCwJKvMnD5YA0bNj2qj_xSxVu7uAiQcl_-pCYC-bKu_RUgX3gyUcTEPosS2jkf4YzhwE_-P1A-lIVinTT1TycUWjGS95qT_lEld62B6kV-s1yFVcWx_-fjMgA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiEZt5638HL7BH04JhKzbuZgZgg825xSajdlLa4PpvOyYwgBsbcrPk3ITjS1_7rkmBZzkCwJKvMnD5YA0bNj2qj_xSxVu7uAiQcl_-pCYC-bKu_RUgX3gyUcTEPosS2jkf4YzhwE_-P1A-lIVinTT1TycUWjGS95qT_lEld62B6kV-s1yFVcWx_-fjMgA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/kamishna-mkuu-tra-awapongeza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/kamishna-mkuu-tra-awapongeza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy