Serikali Yazindua Ajira App Kuondoa Vitendo Vya Rushwa Kwenye Mchakato Wa Ajira
HomeHabari

Serikali Yazindua Ajira App Kuondoa Vitendo Vya Rushwa Kwenye Mchakato Wa Ajira

Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa a...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 26
Diwani Wa Kawe Aliyedaiwa Kutoweka ,akutwa Kwa Mwanamke Tabata
Majaliwa Asimamisha Kazi Mkurugenzi Wa Jiji, Maafisa Watano Arusha


Na. James K. Mwanamyoto-Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezindua “Ajira Portal Mobile App” itakayotumiwa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kuendesha mchakato wa ajira Serikalini ambao utaondoa vitendo vya rushwa na upendeleo kwa waombaji wa ajira.

Akizindua portal hiyo jana jijini Dodoma, Mhe. Mchengerwa amesema portal hiyo itasaidia kuwapata watumishi wenye sifa stahiki na wazalendo watakaolitumikia taifa kwa weledi, uadilifu na wataolifikisha taifa kwenye uchumi wa kati wa juu.

Mhe. Mchengerwa amesema, mfumo huo wa maombi ya kazi kupitia simu ya kiganjani umelenga kuwapunguzia adha mbalimbali walizokuwa wakikutana nazo waombaji wa fursa za ajira ikiwemo upatikanaji wa taarifa zinazohusu ajira serikalini na mchakato wake.

“Mfumo huu ukitumika vizuri, ninaamini waombaji wa ajira wataweza kufanya maombi ya ajira popote walipo mijini na vijijini, kwani mfumo unamuarifu muombaji uwepo wa nafasi.

Mhe. Mchengerwa amewahamasisha waombaji wa ajira serikalini kuanza kutumia mfumo huo ambao utapunguza changamoto nyingi walizokuwa wakikabiliana nazo kabla ya uwepo wa mfumo huo.

Akimkaribisha Mhe. Mchengerwa kuzungumza na Watendaji na wadau wa ajira, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi ameipongeza Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa kutekeleza maelekezo ya Mhe. Mchengerwa ya kuwataka kuanzisha mfumo utakaorahisisha mchakato wa ajira kwa waombaji wa ajira serikalini.

“Nakumbuka katika kikao chako cha kwanza uliporipoti ofisini, ulikuwa na maono ya kufanya mchakato wa ajira kuwa wa kidijitali na kuelekeza mfumo huo uundwe ili kurahisisha mchakato wa ajira Serikalini, na hatimaye leo unazindua rasmi mfumo huo,” Mhe. Ndejembi ameongeza.

Aidha, Mhe. Ndejembi amesema maono ya Mhe. Mchengerwa yanaenda sambamba na utekelezaji wa azma ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akisisitiza mara kwa mara kufanya maboresho ya utoaji wa huduma katika taasisi za umma kupitia TEHAMA.

Akitoa neno la utangulizi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema kukamilika kwa mfumo huo wa Ajira App ni hatua kubwa iliyofikiwa na ofisi katika kurahisisha mchakato wa ajira serikalini kwa kutumia TEHAMA.

Ili kuhakikisha Sekretarieti ya Ajira inautumia mfumo huo ipasavyo, Dkt. Ndumbaro ameiomba Bodi ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma iliyozinduliwa hivi karibuni kushirikiana na watendaji wa Sekretarieti ya Ajira katika usimamizi wa mfumo huo ili uwe na manufaa kwa umma.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake, Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Exavier Daudi amesema huduma hiyo ya Mobile App itaongeza wigo wa upashanaji habari za ajira na kuokoa fedha ambazo waombaji walikuwa wakizitumia kulipia huduma za mtandao kwa wafanyabiashara wa huduma hizo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yazindua Ajira App Kuondoa Vitendo Vya Rushwa Kwenye Mchakato Wa Ajira
Serikali Yazindua Ajira App Kuondoa Vitendo Vya Rushwa Kwenye Mchakato Wa Ajira
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjnaza0KY58Wi5PTsGMvAAOmAb6OmbUzjTYWGBcruAUhVqC09_joX65Mux9jOTPw4sTytVcCFn5wgDmePEnUxz0olEpes8NosZ-LP3e5Dj1uxrKeapjVqL2hgU2EVwTHP37VTCu8LjoQPl1EPhy1h4Owpm8zbwWQAdkdXhTjvc0dDYZhFxrLInbgZOHTg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjnaza0KY58Wi5PTsGMvAAOmAb6OmbUzjTYWGBcruAUhVqC09_joX65Mux9jOTPw4sTytVcCFn5wgDmePEnUxz0olEpes8NosZ-LP3e5Dj1uxrKeapjVqL2hgU2EVwTHP37VTCu8LjoQPl1EPhy1h4Owpm8zbwWQAdkdXhTjvc0dDYZhFxrLInbgZOHTg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/serikali-yazindua-ajira-app-kuondoa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/serikali-yazindua-ajira-app-kuondoa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy