Serikali Yasisitiza Kutowarejesha Kwenye Utumishi Wa Umma Watumishi 15, 538 Walioghushi Vyeti
HomeHabari

Serikali Yasisitiza Kutowarejesha Kwenye Utumishi Wa Umma Watumishi 15, 538 Walioghushi Vyeti

 Na. James K. Mwanamyoto-Arusha Serikali imesisitiza kutowarejesha kwenye Utumishi wa Umma Watumishi 15,538 walioondolewa kazini kwa kug...

Habari kubwa Magazetini Kenya leo October 1, 2024
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo October 1, 2024
Amuua mwenzake kisa Sh 200


 Na. James K. Mwanamyoto-Arusha
Serikali imesisitiza kutowarejesha kwenye Utumishi wa Umma Watumishi 15,538 walioondolewa kazini kwa kughushi vyeti au kutoa taarifa za uongo katika kumbukumbu zao rasmi za kiutumishi kuwa wana elimu ya kidato cha nne.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana jijini Arusha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema, msimamo wa Serikali wa kutowarejesha watumishi hao waliobainika kughushi vyeti uko palepale.

“Ninasisitiza kuwa, hakuna msamaha wowote uliotolewa na Serikali kuwarejesha watumishi waliokosa uadilifu kwa kughushi vyeti au kutoa taarifa za kiutumishi zisizo sahihi,” Mhe. Mchengerwa amefafanua.

Aidha, Mhe. Mchengerwa ameuarifu umma kuwa, Serikali imewaondoa pia watumishi hewa 19,708, hivyo kuiwezesha Serikali kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 19 ambazo zinatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Akizungumzia watumishi waliorejeshwa kazini baada ya kuondolewa kwenye Orodha ya Malipo ya Mishahara, Mhe. Mchengerwa amesema, mwaka 2004 Serikali ilitoa Waraka uliobainisha kwamba watumishi wote watakaoajiriwa kuanzia tarehe 20 Mei, 2004 walitakiwa kuwa na elimu ya Kidato cha Nne ikiwa ni utekelezaji wa matakwa ya Sera ya Ajira na Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na Kanuni za Utumishi wa Umma.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, katika utekelezaji wa matakwa hayo, mwaka 2017 wakati wa zoezi la uhakiki wa vyeti na watumishi hewa ilibainika baadhi ya watumishi wenye elimu ya Darasa la Saba waliajiriwa bila ya kuwa na cheti cha ufaulu wa elimu ya Kidato cha Nne. Hivyo, watumishi hawa waliondolewa kazini kutokana na kukosa sifa kwa mujibu wa Miundo ya Utumishi ya Kada zao.

Amesema katika zoezi hilo, baadhi ya Waajiri waliwaondoa kwenye Orodha ya Malipo ya Mishahara kimakosa watumishi wasiokuwa na elimu ya Kidato cha Nne walioajiriwa kabla ya tarehe 20 Mei, 2004. Kutokana na makosa hayo, mwaka 2018 Serikali kupitia Waajiri na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliwarejesha kazini na kuendelea kuwalipa mishahara jumla ya watumishi 4,380 walioondolewa kwenye Orodha ya Malipo ya Mishahara kimakosa. Idadi hii inajumuisha Watendaji wa Kata, Watendaji wa Mtaa na Watendaji wa Kijiji wapatao 3,114.

Pamoja na kuwarejesha watumishi tajwa, Mhe. Mchengerwa amesema Serikali pia ilitoa msamaha wa kuwarejesha kazini watumishi walioondolewa kazini kwa kukosa sifa ya elimu ya Kidato cha Nne na baadaye wakajiendeleza na kupata sifa tajwa hadi kufikia mwezi Desemba, 2020. Msamaha huu uliwahusu watumishi waliojipatia vyeti vya elimu ya Kidato cha Nne ambao hawakudanganya katika taarifa zao kuwa wana elimu ya Kidato cha Nne au hawakubainika kughushi vyeti.

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mhe. Mchengerwa kuzungumza na Waandishi wa Habari, Katibu Mkuu-UTUMISHI, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema lengo la Mhe. Mchengerwa kuzungumza na Vyombo vya Habari ni kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya mitandao ya kijamii kuwa Serikali imeamua kuwarejesha kazini watumishi walioghushi vyeti na walioajiriwa kwa cheti cha darasa la saba ambao walishindwa kujiendeleza ili kupata sifa stahiki hadi kufikia mwezi Desemba, 2020 kama Serikali ilivyoelekeza.

Ameongeza kuwa, Ofisi yake iliwaandikia waajiri wote barua tarehe 7 Mei, 2021 kuelekeza namna ya kuhitimisha suala la hilo ambalo waathirika wamekuwa wakiibua hoja nyingi ambazo tayari Serikali ilishazitolea maamuzi.

Dkt. Ndumbaro amesema upotoshwaji unaendelea kufanywa licha ya Mhe. Waziri Mkuu, Msemaji wa Serikali na Mhe. Mchengerwa mwenyewe kutoa ufafanuzi wa suala hili hivi karibuni, hivyo Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ameona ni vema akazungumza tena na Vyombo vya Habari ili kulielezea kwa kina suala hili na hatimaye jamii ielewe hatua zilizochukuliwa na Serikali na msimamo wake.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yasisitiza Kutowarejesha Kwenye Utumishi Wa Umma Watumishi 15, 538 Walioghushi Vyeti
Serikali Yasisitiza Kutowarejesha Kwenye Utumishi Wa Umma Watumishi 15, 538 Walioghushi Vyeti
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgCFdzotOOax_4hcjmtGDZ41WV2U7iLVo8QtwzWb1CaKfea-5F7hLnvcSTBX9DRD8Z3ZUiSZlPGx3iUcstx1d5FLTH0D6wq4Brb0HHXRrNZTeFaVD0U2GUuXy5YvfFteEADOcg-1kkg6DmcdyHGo6AEV30igfLtWD25hD7PHtOV9Gi0IudNiQVAkQ-Juw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgCFdzotOOax_4hcjmtGDZ41WV2U7iLVo8QtwzWb1CaKfea-5F7hLnvcSTBX9DRD8Z3ZUiSZlPGx3iUcstx1d5FLTH0D6wq4Brb0HHXRrNZTeFaVD0U2GUuXy5YvfFteEADOcg-1kkg6DmcdyHGo6AEV30igfLtWD25hD7PHtOV9Gi0IudNiQVAkQ-Juw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/serikali-yasisitiza-kutowarejesha.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/serikali-yasisitiza-kutowarejesha.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy