UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kwamba mchezo wao wa marudio dhidi ya Rivers United hautakuwa mwepesi ila wamejipanga kuweza kufanya vizuri...
UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kwamba mchezo wao wa marudio dhidi ya Rivers United hautakuwa mwepesi ila wamejipanga kuweza kufanya vizuri.
Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi ina kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Rivers United kwenye mchezo wa marudio.
Mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika unatarajiwa kuchezwa nchini Nigeria Septemba 19.
Katika ule mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkapa, ubao ulisoma Yanga 0-1 Yanga hivyo kazi kubwa ipo kwenye kupindua matokeo ugenini.
Ofisa Habari wa Yanga, Haji Manara amesema:"Tunajua mechi za ugenini zina visa na mikasa mingi, tumejipanga na tumejiandaa na hilo na ndiyo maana tulituma watu imara wakufanya maandalizi yote kabla ya timu kufika.
Ni Senzo Mbatha ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Yanga kwa muda aliweza kutangulia nchini Nigeria na kwa sasa yupo huko akisubiri kuwapokea Yanga.
Mbatha ameweka wazi kuwa kila kitu kinakwenda sawa licha ya changamoto za soka la Afrika ambazo huwa hazikosekani.
Credit: SALEH JEMBE
Please subscribe to get all sports news instantly
COMMENTS