KOCHA WA YANGA ATAKA MECHI TATU KUWAWAKE FITI VIJANA WAKE
HomeMichezo

KOCHA WA YANGA ATAKA MECHI TATU KUWAWAKE FITI VIJANA WAKE

  M ARA  baada ya  kikosi chake  kuingia kambini,  Kocha Mkuu wa  Yanga raia wa  Tunisia, Nasreddine Nabi ameomba  michezo mitatu ya kiraf...


 MARA baada ya kikosi chake kuingia kambini, Kocha Mkuu wa Yanga raia wa Tunisia, Nasreddine Nabi ameomba michezo mitatu ya kirafiki kabla ya kurejea katika Ligi Kuu Bara na Kombe la FA.

 

Timu hiyo tayari imeanza mazoezi kwenye Uwanja wa Avic Town, Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Ruvu Shooting utakaopigwa Juni 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

 

Michezo ya ligi na Kombe la FA, hivi sasa imesimama ili kupisha kambi ya timu ya taifa, Taifa Stars inayojiandaa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Malawi utakaopigwa Juni 5, mwaka huu.


 Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh amesema kuwa kocha huyo ameomba michezo hiyo kwa ajili ya kutengeneza fitinesi ya wachezaji wake.


Saleh amesema kuwa, muda wowote huenda wakatangaza timu watakazocheza nazo mara baada ya kikao cha viongozi wa benchi kukutana na kujadiliana.

 

Aliongeza kuwa kati ya timu ambazo watakazocheza nazo ipo yao ya vijana U20 itakayochezwa kwenye Uwanja wa Avic Town na lengo kocha kupata nafasi ya kuiona timu ya vijana.

 

“Ngumu kwa timu kukaa wiki mbili bila kucheza mechi za kirafiki wakati tukiwa katika mashindano, hivyo wakati muda huu ligi imesimama kocha amependekeza tucheze michezo ya kirafiki.

 

"Lengo ni kutengeneza fitinesi na utimamu wa mwili ili ligi itakapoanza, basi wachezaji wake wawe tayari kwa ajili ya mapambano.


“Zipo baadhi ya timu ambazo tutacheza nazo michezo ya kirafiki lakini kwa kuanza huenda tukacheza na timu yetu ya vijana ya U20 hapa kwenye Uwanja wa Avic Town,” amesema Saleh.


Tayari mchezo wa kwanza umeshawekwa wazi ambao ni dhidi ya African Lyon unaotarajiwa kuchezwa Juni 6,2021, Uwanja wa Azam Complex.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KOCHA WA YANGA ATAKA MECHI TATU KUWAWAKE FITI VIJANA WAKE
KOCHA WA YANGA ATAKA MECHI TATU KUWAWAKE FITI VIJANA WAKE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjO3JH8MDoxLUCatI8zv0yQ98ZZi75MqQjCUTRkNHb75EZ6GWqBRyg86dUqfL3QfYZ3ZJt_qG2qNqe7zvPAbF0HW7M_ziNY7b581_bYKER-JzfNYXPdqPMo5RouAxP-ndW0C7i1X9WAb-o_/w640-h606/yangasc-194917261_858418654755099_8729649926297399667_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjO3JH8MDoxLUCatI8zv0yQ98ZZi75MqQjCUTRkNHb75EZ6GWqBRyg86dUqfL3QfYZ3ZJt_qG2qNqe7zvPAbF0HW7M_ziNY7b581_bYKER-JzfNYXPdqPMo5RouAxP-ndW0C7i1X9WAb-o_/s72-w640-c-h606/yangasc-194917261_858418654755099_8729649926297399667_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kocha-wa-yanga-ataka-mechi-tatu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kocha-wa-yanga-ataka-mechi-tatu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy