KOCHA WA REAL MADRID ZIDANE KUTIMKA MAZIMA
HomeMichezo

KOCHA WA REAL MADRID ZIDANE KUTIMKA MAZIMA

  TAARIFA zilizoripotiwa na vyombo vya habari vya Hispania zinaeleza kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amethibitish...


 TAARIFA zilizoripotiwa na vyombo vya habari vya Hispania zinaeleza kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Real Madrid, Zinedine Zidane amethibitisha kuwa ataondoka klabuni hapo mara baada ya kumalizika kwa msimu huu hata kama atachukua ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania LaLiga.

 

Madrid ambao walisepa na ushindi mbele Granada na kufanikiwa kuondoka na pointi tatu kwa kuifunga bao 4-1 wakiwa ugenini, kwa sasa wapo katika nafasi ya pili ya msimamo wa La Liga wakiwa na pointi 78 nyuma ya Atletico Madrid ambao wana pointi 80 na michezo miwili imesalia kumalizika kwa ligi hiyo.


Zidane (48) akiwa Madrid ameshinda mataji mawili ya La liga na mataji matatu ya UEFA Champions League kwa misimu minne ambayo ameitumikia klabu hiyo lakini ameamua kuondoka klabuni hapo baada ya mechi yao ya mwisho ya ligi dhidi ya Villarreal itakayopigwa Mei 23, Santiago Bernabeu.

 

Zidane atakuwa chagua la kwanza la Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa iwapo watafanya mabadiliko ya kocha baada ya Fainali za Euro zinazotarajiwa kuanza Juni 11.


Rais wa Madrid, Florentino Perez yupo katika wakati mgumu kusaka mbadala wa Zidane ambapo inaelezwa anataka kumpandisha Kocha Raul kuchukua mikoba ya Zizzou ama atamchukua tena kocha Max Allegri.

 

Zidane amesema anahisi hayuko kwenye moyo wa Perez na hata kama atachukua taji la La Liga kwa mara ya tatu, rekodi ambayo atakuwa ameiweka ya kurudisha kombe la La Liga kwa misimu miwili mfululizo.

 

Zidane ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya kutofautiana na mchezaji wake, beki kisiki Marcelo raia wa Brazil baada ya kumuacha katika kikosi chake kilichocheza na Granada huku ikielezwa kuwa wawili hao hawana mahusiano mazuri klabuni hapo kwa sasa.


Marcelo atamaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu huu. Marcelo anasema Zidane amekuwa mtu wa kukosoa sana katika mazoezi wakati akizungumza na timu yake kuhusu ushindi wa mechi zake, lakini pia alizungumza mbele ya meneja wa timu kuhusu kuamua kumuacha Marcelo na kumchukua kinda wa miaka 19, Miguel Gutierrez kuanza.

 




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KOCHA WA REAL MADRID ZIDANE KUTIMKA MAZIMA
KOCHA WA REAL MADRID ZIDANE KUTIMKA MAZIMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4onO7Z1W1o83QrOhrTbtHHdaddnRZ7efB8QskWrLtnn_Lw7Pu09gmBkVZ6CI4B4U4SA4aZxnlYLcWcJcQl-Uu3_F0-2baj5T1nrRjlMKVRxYN7OL90lQmBbh7_zTXWt4F3u4N3qYJ3ZYn/w640-h424/Zide+kichwa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4onO7Z1W1o83QrOhrTbtHHdaddnRZ7efB8QskWrLtnn_Lw7Pu09gmBkVZ6CI4B4U4SA4aZxnlYLcWcJcQl-Uu3_F0-2baj5T1nrRjlMKVRxYN7OL90lQmBbh7_zTXWt4F3u4N3qYJ3ZYn/s72-w640-c-h424/Zide+kichwa.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/kocha-wa-real-madrid-zidane-kutimka.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/kocha-wa-real-madrid-zidane-kutimka.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy