Waziri Biteko Aitaka Bodi Ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) Kujitathimini
HomeHabari

Waziri Biteko Aitaka Bodi Ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) Kujitathimini

Tito Mselem na Steven Nyamiti, Dodoma  Waziri wa Madini Doto Biteko ameitaka Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) kuji...

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Novemba 28
Rais Samia Amedhamiria Kulinda Na Kuimarisha Afya Za Watanzania-majaliwa
Tanzania, Uswisi Kuimarisha Ushirikiano Zaidi


Tito Mselem na Steven Nyamiti, Dodoma
 Waziri wa Madini Doto Biteko ameitaka Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) kujitathimini namna ya utendaji kazi wao.

Waziri Biteko ameeleza kuwa, GST inapaswa ijitangaze ili jamii itambue kazi ya Taasisi hiyo ambapo amesisitiza shughuli zinazofanywa na Taasisi hiyo lazima zitambulike ndani na nje ya nchi.

“Taasisi yoyote inayokua, ikiwa Taasisi inayosubili matukio yaiibue, basi Taasisi hiyo maisha yake ni mafupi, mimi naiona hatari ya GST, utendaji kazi wa Taasisi hii bado hauridhishi ninatamani kuiona GST ikizungumzwa” amesema Biteko.

Waziri Biteko amesema kuwa, Uti wa Mgongo wa Sekta ya Madini ni GST ambao ndio watafiti wa madini nchini ambapo amewataka wajumbe wa Bodi ya GST wabuni mikakati madhubuti itakaiyoboresha Taasisi hiyo ili kuifanya GST ijiendeshe yenyewe.

Aidha, Waziri Biteko ameongeza kuwa, anatamani kuona mabadiliko ya Sekta ya Madini nchini yanaenda sambamba na ukuaji wa Taasisi ya GST.

“Kiu yangu ni kuiona GST inakua na inajiendesha yenyewe ikiwa ni pamoja na kuongeza mapato zaidi tofauti na ilivyo sasa,” amesema Waziri Biteko.

Pia, Waziri Biteko amesema, GST inatakiwa ijitangaze ndani na nje ya nchi ambapo ameitaka Bodi hiyo ishiriki kikamilifu katika Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta Madini utakaoanza Februari 21 mpaka 24, 2021 ili kutumia fursa hiyo kujitangaza kimataifa.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila ameipongeza GST kwa kushiriki uchunguzi wa upatikanaji wa madini ya Urenium Mvomero Mkoani Morogoro ambapo mpaka sasa matokeo ya tafiti hizo yametoka na yapo katika hatua ya kujadiliwa

Awali, akifungua Mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya GST Prof. Justinian Ikingula alianza kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuiwezesha GST kutimiza majukumu yake.

Akifafanua juu ya uwezeshaji huo Prof. Ikingula alisema kuwa serikali imeipatia GST kiasi cha Shilingi bilioni 3.3 ambazo zimewezesha GST kununua vifaa mbalimbali vya maabara ikiwa ni pamoja na ununuzi wa magari sita ambayo yatarahisisha utendaji kazi wa Taasisi hiyo.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya GST, Prof. Ikingula alieleza Kuwa GST imeshiriki katika tafiti mbalimbali za jiosayansi kama vile utafiti katika mji wa serikali (Mtumba), Mradi wa Ujenzi wa reli ya mwendokasi pamoja na mradi wa Bwawa la uzalishaji umeme lijulikanalo kwa jina la (Mwalimu Nyerere Hydro Power).


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Biteko Aitaka Bodi Ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) Kujitathimini
Waziri Biteko Aitaka Bodi Ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) Kujitathimini
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhhn277uhwMDE_NpCcrlocnx9gyXvURcmG32DkkHeKIzZLdgp_YxquXHiJkFbFduZpE-pkwST1fRE0Evc3lf2FuWfqNgFgW_ft16jTg6xrWfPfxR7OzPcoBxCq7TKK4LUA7Bw1OkV47mj7p/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhhn277uhwMDE_NpCcrlocnx9gyXvURcmG32DkkHeKIzZLdgp_YxquXHiJkFbFduZpE-pkwST1fRE0Evc3lf2FuWfqNgFgW_ft16jTg6xrWfPfxR7OzPcoBxCq7TKK4LUA7Bw1OkV47mj7p/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/waziri-biteko-aitaka-bodi-ya-taasisi-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/waziri-biteko-aitaka-bodi-ya-taasisi-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy