KUMBE SIMBA WAMEYEYUSHA BILIONI 1 KIMATAIFA, WAKIFUNGWA WANAAMBULIA PATUPU
HomeMichezo

KUMBE SIMBA WAMEYEYUSHA BILIONI 1 KIMATAIFA, WAKIFUNGWA WANAAMBULIA PATUPU

  I MEFAHAMIKA  kuwa Simba imetumia  kitita cha shilingi bilioni  moja katika hatua ya  makundi ya Ligi ya  Mabingwa Afrika msimu huu. Si...

AZAM FC WAANIKA MIPANGO YAO
FEI TOTO: MAMBO MAZURI YANAKUJA MSIMU UJAO
KAGERE AOMBA KUONDOKA SIMBA, YANGA WAANDAA MKATABA

 IMEFAHAMIKA kuwa Simba imetumia kitita cha shilingi bilioni moja katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu.

Simba tayari imefuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo mikubwa Afrika baada ya kuwafunga AS Vita mabao 4-1 mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, Aprili 3.

 

Timu hiyo imefuzu hatua hiyo ya makundi ikiwa inaongoza katika msimamo Kundi A, ikiwa na pointi 13 ikiwa imebakisha mchezo mmoja pekee dhidi ya Al Ahly utakaopigwa leo Ijumaa huko Cairo, Misri.


Taarifa zimeeleza kuwa Simba imetumia Sh 1Bil iliyotumika kwa ajili ya kuwapa bonasi wachezaji na benchi la ufundi.

 

Mtoa taarifa huyo alisema kuwa bonasi hiyo imetumika kwa ajili ya kuwaongezea morali na hali ya kujituma kwa wachezaji wake ili kufanikisha ushindi.

Aliongeza kuwa bonasi hiyo imehusisha michezo ya kimataifa pekee tofauti na Ligi Kuu Bara ambayo huko ipo bajeti nyingine inayojitegemea.

 

“Michuano ya kimataifa ina umuhimu wake, hivyo imetengwa bajeti maalum kwa ajili ya bonasi ya wachezaji wetu ambayo imetengwa katika makundi mawili.

 

“Makundi hayo kama timu ikifanikiwa ushindi kuna kiwango cha pesa ambacho wachezaji na benchi la ufundi, endapo timu ikipata ushindi na sare lakini timu ikifungwa hawapati bonasi.

 

“Hivyo hadi timu yetu inafanikiwa kufuzu robo fainali tumetumia kiwango cha Sh 1Bil kama sehemu ya bonasi kwa wachezaji na benchi la ufundi na hiyo ni katika kuwaongezea morali na hali ya kujituma,” alisema mtoa taarifa huyo.

 

Mshauri wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba Crescentius Magori hivi karibuni alizungumzia hilo la posho la wachezaji na kusema kuwa: “Hilo la posho lipo katika mikataba yetu kati ya wachezaji na uongozi.

 

“Hivyo wachezaji wetu tumewawekea utaratibu wa kuwapatia posho katika kuongeza morali ya ushindi pale wanapoipatia timu matokeo mazuri ya ushindi, hivyo hilo lipo katika timu yetu.”



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KUMBE SIMBA WAMEYEYUSHA BILIONI 1 KIMATAIFA, WAKIFUNGWA WANAAMBULIA PATUPU
KUMBE SIMBA WAMEYEYUSHA BILIONI 1 KIMATAIFA, WAKIFUNGWA WANAAMBULIA PATUPU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNAcMP7P5pEFplgn_NzD7PjctUZIKLBV_bRdNn2IgjSEwwivLB-WXkvlvhqwLli0K5o0LoTFZJK1xCvr_KrU_6siBWJN1DN3hEXPSWjPNkFuceG8n1p9de1VB602omkosK7TfsgpN5CjFW/w640-h426/Bwalya+v+AS+Vita.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNAcMP7P5pEFplgn_NzD7PjctUZIKLBV_bRdNn2IgjSEwwivLB-WXkvlvhqwLli0K5o0LoTFZJK1xCvr_KrU_6siBWJN1DN3hEXPSWjPNkFuceG8n1p9de1VB602omkosK7TfsgpN5CjFW/s72-w640-c-h426/Bwalya+v+AS+Vita.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/kumbe-simba-wameyeyusha-bilioni-1.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/kumbe-simba-wameyeyusha-bilioni-1.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy