Waziri Bashungwa Atoa Onyo Kwa Wanaotumia Vibaya Mitandao Ya Kijamii
HomeHabari

Waziri Bashungwa Atoa Onyo Kwa Wanaotumia Vibaya Mitandao Ya Kijamii

Na Eleuteri Mangi- WHUSM, Arusha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa ameonya watumiaji wa mitandao ya ...

Serikali Yakaribisha Wadau Utekelezaji Mpango Wa Taifa Wa Maendeleo
Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato
Serikali Yazihakikishia Kampuni Za Uswisi Mazingira Salama Ya Biashara, Uwekezaji


Na Eleuteri Mangi- WHUSM, Arusha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa ameonya watumiaji wa mitandao ya kijamii kinyume na Kanuni ya Maudhui Mtandaoni za 2018 ambazo zinawazuia watumiaji wa mitandao hiyo kutokutumia lugha za kuudhi/matusi na kutokusambaza taarifa za uongo au za upotoshaji.

Waziri Bashungwa amesema hayo jana  jijini Arusha wakati wa kongamano la fursa kwa wanamuziki lililoandaliwa na Taasisi ya kijamii inayoshughulika na wanamuziki (TAMUFO) ambalo jukumu lake ni kuhamasisha maendeleo, kupambana na umaskini, ujinga na maradhi na kuwa na usawa katika mgawanyo wa mapato yanayotokana na muziki kwa wanamuziki.

Ikumbukwe Julai 17, 2020, Serikali ilichapisha mabadiliko ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni kwenye gazeti la Serikali kupitia gazeti Na.29 Toleo la 101 ambayo yalitolewa kupitia notisi Na. 538 yanabadilisha baadhi ya Kanuni za Maudhui Mtandaoni za mwaka 2018 ili kuhakikisha zinalinda maslahi ya watumiaji wa mitandao hiyo bila kuleta taharuki zisizo za lazima katika jamii.

Aidha, Waziri Bashungwa amewataka Watanzania kuendelea kuliombea taifa hatua itakayowasaidia wananchi kuendelea kuwa na afya bora ili kupambana dhidi ya magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza.

Akiongea na wasanii pamoja na wadau waliohudhuria kongamano hilo, Waziri Bashungwa amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha kila msanii ananufaika na kazi yake pamoja na kuongeza pato la taifa.

“Nimetoa maelekezo kwa Chama Haki Miliki (COSOTA) wakamilishe mfumo utakaosaidia kutambua kazi za wasanii zinapotumika kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wahakikishe kila redio, TV, mabasi, baa ama kumbi za starehe ambao utatambua na kusaidia kukusanya mapato ambayo yatrasaidia wananamuziki kunufaika na kazi zao,” alisema Waziri Bashungwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Arusha Iddi Hassan Kimanta amesema mkoa huo upo salama na wasanii kutoka ndani na nje ya mkoa huo wanakaribishwa kufanya kazi zao za Sanaa ili kujiongezea vipato vyao na taifa kwa ujumla.

Naye Katibu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), Stella Joel na Mwimbaji wa Muziki wa Injili Nchini Tanzania amesema Taasisi hiyo inashirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuwapatia wansanii bima ambazo ni mkombozi wa afya zao pindi wanapopata matatizo ya kiafya.

Aidha, taasisi hiyo imewawezesha wanamuziki na wanajamii wapatao 2,014 kupata elimu ya afya na vipimo kutoka kwa Madaktari Bingwa wa Hospitali za Apollo India na Canada kupitia Excellent International Services Ltd (EIS), Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa Dodoma, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mt. Meru Arusha, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe na Hospitali ya Wilaya ya Karatu kupitia makongamano yaliyoambatana na uelimishaji na uchangiaji wa damu salama.

Kongamano hili la fursa ni la  nne kufanyika mkoa wa Arusha ambapo hadi sasa jumla ya Kongamano la 27 yamefanyika, kati ya makongamano hayo, yapo yaliyofanya katika mikoa mbalimbali  ikiwemo Dar es salaam, Arusha, Dodoma, Njombe, Mwanza, Morogoro na Iringa.


 



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Bashungwa Atoa Onyo Kwa Wanaotumia Vibaya Mitandao Ya Kijamii
Waziri Bashungwa Atoa Onyo Kwa Wanaotumia Vibaya Mitandao Ya Kijamii
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJJCJk4dZdm3leLyCafi8NDrtjc24cvWFFFWi4-VoGKEF-BYk8ogb6w6YH8_PW8kybreRG78lpMnJ6DB4rmKOponTBlO5CwWVF33SQIfMKvI4aLbisTvk5sqpiBdyAXD2KKI4zbGuy7fPK/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJJCJk4dZdm3leLyCafi8NDrtjc24cvWFFFWi4-VoGKEF-BYk8ogb6w6YH8_PW8kybreRG78lpMnJ6DB4rmKOponTBlO5CwWVF33SQIfMKvI4aLbisTvk5sqpiBdyAXD2KKI4zbGuy7fPK/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/waziri-bashungwa-atoa-onyo-kwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/waziri-bashungwa-atoa-onyo-kwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy